Je! Wakumbuka?
Je! wewe umefurahia kusoma matoleo kadha yaliyopita ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, ona kama unaweza kukumbuka jambo hili:
□ Tunapatwa na ugonjwa kwa sababu tumetenda dhambi fulani?
Hapana, si lazima iwe hivyo. Ugonjwa ni mmoja wa shuhuda zenye kuonyesha kwamba sisi sote tulirithi dhambi na hali ya kutokukamilika kutoka kwa Adamu. (Warumi 5:12) Lakini, dhambi ya kukusudia inaweza kufanya mtu aitende dhambi roho takatifu ya Mungu, na hilo ni jambo baya sana kuliko ugonjwa wa kimwili. (Mathayo 12:31, 32)—9/15/83, uku. 23.