Hazina ya Kugawana na Wengine
Hivyo ndivyo anavyohisi mwanafunzi wa miaka 15 wa shule ya Sekondari katika Ohio, U.S.A., juu ya kile kichapo cha hivi majuzi, Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Msichana huyo anaandika hivi:
“Ikiwa vitu vizuri vinachukua muda kufanyika, bila shaka ilichukua umilele kukikusanya kitabu hiki chenye picha za kupendeza kilicho rahisi kueleweka. Hicho kinaziteka kabisa fikira za mtu! Mimi najifunza sura moja kwa siku na kujikuta nikisema laiti ningalikuwa na wakati mwingi zaidi wa kutumia kujifunza kibinafsi msaada huu ulio mzuri ajabu.”
“Tayari mimi nimefanya orodha ya rafiki na walimu ambao wangefurahia kichapo hiki. Shule itakapoanza mwezi unaokuja, nitakuwa na pendeleo la kushiriki nao hazina yangu.”
Labda wewe una maoni yanayofanana na ya kijana huyo juu ya kitabu kile kipya Creation. Je! wewe unajua mtu fulani ambaye ungependa ushiriki naye hazina hiyo? Mbona usimpelekee nakala ya zawadi? Unaweza kufanya hivyo kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyopo chini, uipeleke kwetu pamoja na Kshs. 35.00 (Tshs. 100.00).
Tafadhali mpelekeeni mtu huyu nakala ya zawadi ya kile kitabu cha kurasa 256 kinachoitwa Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?, na pia barua ya kueleza kwamba hii ni zawadi kutoka kwa‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐(Jina lako). Mimi nimewapelekea Kshs. 35.00 (Tshs. 100.00)