Nakala za Kibinafsi Zatakwa
Mama mmoja kutoka Illinois, U.S.A., aliandika hivi: “Binti yangu na mimi tumesoma hadithi kutoka kichapo chenu kilichofungwa kwa jalada gumu, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na tukazifurahia kweli kweli. Sisi tulienda kwenye maktaba ya mtaa wetu tukapata kitabu hicho na kukiazima pamoja na zile kaseti nne zenye kuambatana nacho.
“Kwenye upande wenyewe wa nyuma wa kitabu hicho yalichapwa maneno yenye kusema ‘Nakala zaidi za kitabu hiki zaweza kupatikana kwa bei ya Kshs 35/-.’ Je! bei hiyo ni sahihi? Pia, nitaagiza nakala za ziada kutoka wapi. Nakala moja ya kitabu hicho na zile kaseti nne ni pesa ngapi?”
Zile kaseti nne, kutia na pakiti ambamo zinakuwa, ni Kshs. 115.00 (Tshs. 320.00). Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, ambacho kurasa zacho zina ukubwa unaolingana na kurasa za gazeti hili, ni Kshs. 35.00 (Tshs. 100.00). Ili upate mafundisho ya Biblia yenye kutumbuiza, jipatie kitabu hiki chenye picha nzuri sana na pia ile pakiti ya kaseti zilizorekodiwa habari za kitabu hicho.
Tafadhali onyesha kwa kutia alama katika visanduku hivi mbalimbali uonyeshe kama unataka kitabu chenyewe au ile pakiti ya kanda za kaseti, au vyote viwili.
[ ] Mimi nimewapelekea Kshs. 35.00 (Tshs. 100.00) kwa ajili ya Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia [ ].
[ ] Mimi nimewapelekea Kshs. 115.00 (Tshs. 320.00) kwa ajili ya ile pakiti ya rangi ya hudhurungi yenye kanda za kaseti nne za Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia [ ].