Ukumbusho Aprili 12
“Vilevile, yeye alichukua mkate mmoja, akatoa shukrani, akauvunja, na akawapa, akisema: ‘Huu maana yake ni mwili wangu ambao utatolewa kwa ajili ya ninyi. Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi. Pia, kikombe kwa njia ile ile baada ya wao kula chakula cha jioni, yeye akisema: ‘Kikombe hiki kinamaanisha lile agano jipya kwa uwezo wa damu yangu, ambayo ilamwagwa chini kwa ajili yenu.’”—Luka 22:19, 20, NW.
Mashahidi wa Yehova wanakualika uwepo kwa ajili ya kushika mwadhimisho huu wa Ukumbusho wa maana sana. Mwaka huu tarehe kwenye kalenda yetu inayolingana na ile siku aliyokufa Yesu ni Jumapili, Aprili 12, baada ya jua kutua. Mnaweza kuhudhuria jioni hiyo kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu na nyumbani kwako. Onana na Mashahidi wa Yehova wa kwenu ujue saa barabara.