Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 5/15 kur. 26-27
  • ‘Kununua Wakati’ Katika Italia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kununua Wakati’ Katika Italia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Manufaa ya Kitambulikana
  • Alazimishwa Kuchoma Biblia Yake
  • Mwenye Bidii Akiwa na Umri wa Miaka Sabini
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 5/15 kur. 26-27

‘Kununua Wakati’ Katika Italia

‘ENDELEENI kununua wakati unaofaa,’ mara mbili mtume Paulo aliwahimiza Wakristo wenzake walipokuwa katika Roma, Italia. (Waefeso 5:15, 16, NW; Wakolosai 4:5) Wasomaji wake katika karne ya kwanza waliitikia vizuri. Walitafuta wakati unaofaa kueneza zile “habari njema” na wakasaidia wengine wawe waabudu wa yule Mungu wa kweli.

Watumishi wa Yehova wa kisasa katika Italia, mahali ambapo Paulo aliandikia barua hizo, wangali wanaitikia vizuri shauri lake. Kama vile Wakristo wa kwanza-kwanza, wao wanatafuta njia za kuzidisha ushiriki wao katika kazi ya kuhubiri Ufalme. Wao wanapataje ‘wakati unaofaa’?

Manufaa ya Kitambulikana

Giuseppe, mhudumu wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova aliye mzee-mzee katika Roma, anakumbuka wakati ambao alikuwa na kazi ya kimwili. Yeye alihakikisha kwamba wafanya kazi wenzake wote walikuwa wanajua kwamba yeye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Utambulishi huo uliongoza kwenye wakati ‘unaofaa’ wa kushiriki kweli za Biblia. Siku moja yeye alipewa mgawo wa kumzoeza mwanamume mmoja aliyeitwa Gianni. Mara hiyo wale wafanya kazi wengine walimwambia Gianni kwamba mwalimu angekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Mara mfanya kazi huyo alipokuwa peke yake na Giuseppe, yeye alimwambia Giuseppe: “Sasa tutazungumza juu ya kazi, lakini wakati wa chakula cha mchana ninataka kujifunza jambo fulani juu ya Yehova.”

Nyakati za kipindi cha chakula cha mchana walikuwa na mazungumzo kadha. Giuseppe alimfundisha Gianni kwamba Mungu ana jina, Yehova. Yeye pia alieleza kusudi la Mungu kwa dunia. Ni jambo gani lililotokea, ingawa hivyo, wakati kipindi cha mazoezi kilipokwisha? “Mimi nilimpa namba yangu ya simu na vichapo vya Biblia,” asema Giuseppe. “Yeye alikubali vichapo lakini akasema: ‘Kama nitapata jambo katika vichapo hivi ambalo halipatani na ukweli wa Biblia, nitarudi hapa na kukuthibitisha kuwa umekosea mbele za wafanya kazi wenzako wote.’”

Miezi ikapita. Hakuna neno kutoka kwa Gianni. “Lakini ndipo,” aendelea Giuseppe, “siku moja alinipigia simu na kusema kwamba alitaka kuniona mimi. Tulikutana, naye alikuwa na orodha ya maswali. Tuliongea kwa saa kumi! Alikubali toleo langu la kujifunza Biblia kwa ukawaida.” Matokeo yalikuwa nini? Giuseppe anasema: “Yale mabadiliko yenye kufaa aliyofanya yalimvutia mkeye na mamaye sana hivi kwamba wao, pia, wakaanza kuonyesha kupendezwa na funzo la Biblia. Leo Gianni, mkeye, na mamaye wote ni watumishi waaminifu wa Yehova.”

Alazimishwa Kuchoma Biblia Yake

Mwenendo mzuri wa Kikristo pia unaongoza kwenye ‘wakati unaofaa’ wa kushiriki kweli za Biblia pamoja na wengine. Kama anavyosema mtume Paulo, mwenendo mzuri unaweza ‘kuyapamba mafundisho ya Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote.’—Tito 2:10.

Pietro, ambaye sasa ni Shahidi katika miaka yake ya mwisho-mwisho ya ishirini na kitu, alivutiwa na “mafundisho” kama hayo kwa mwenendo wa Kikristo wa mwanadarasa mwenzake. “Mimi nilikuwa katika darasa la tano,” akumbuka Pietro, “lakini ningali nakumbuka mwenendo wa kivulana yule. Ndiye peke yake aliyekataa kukaa darasani wakati wa mafundisho ya kidini.”

Siku moja Pietro alimuuliza kivulana huyo kwa nini sikuzote yeye huondoka. Kivulana huyo alieleza kwamba yeye alikuwa amepewa ruhusa ya kuondoka darasani kwa sababu yeye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kupendeza kwa Pietro kuliamshwa. Akamuuliza kivulana huyo amletee Biblia. Baada ya kusoma sehemu fulani za Biblia, “mimi nilifahamu kwamba ina ukweli,” asema Pietro. “Nikaamua kwamba nilitaka kuifuata kuanzia hapo na kuendelea. Niliichukua Biblia hiyo shuleni na kumwambia kila mtu kwamba mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wakati huo nilikuwa na umri wa miaka kumi tu.”

Matata yakaanza. Pietro anaendelea: “Yule padri aliyekuwa akiongoza mafundisho ya kidini shuleni aliwaambia wazazi wangu kwamba nilikuwa nikitumia Biblia shuleni, naye akawashauri waiharibu. Nilipokuja nyumbani, mama alijaribu kuinyakua Biblia yangu, lakini niliishikilia kwa nguvu kadiri nilivyoweza. Ndipo Mama akaanza kunipiga na kuirarua kutoka mikononi mwangu. Baada ya hapo alinilazimisha niichome Biblia yangu mwenyewe.” Pietro aliipoteza Biblia yake lakini si imani yake. Aliwaza hivi: “Mara niwapo mtu mzima, nitanunua Biblia mpya na kutoka nje kushiriki pamoja na wengine ujumbe wayo.”

Miaka miwili ikapita. Kisha Pietro akajifunza kwamba funzo la Biblia lilikuwa likiongozwa katika nyumba ya mmoja wa rafiki zake. Alihudhuria funzo hilo kwa siri. “Siku moja,” asema Pietro, “niliwaambia wazazi wangu, ‘Mimi nimeamua kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wakati huo hakuna kitu cho chote kitakachobadili nia yangu!”’ Kwa kuona azimio la mwana wao wa miaka 12, wakati huo wazazi walikubali. Pietro alianza kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme mara moja. Miaka minne baadaye yeye alibatizwa akiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Leo, miaka 18 baada ya kujifunza ukweli kwa mara ya kwanza kutoka katika Biblia kwa sababu ya mwenendo mwaminifu wa mwanadarasa mwenzake, Pietro ‘ananunua wakati unaofaa’ kwa kutumikia akiwa mhudumu wa wakati wote katika Italia.

Mwenye Bidii Akiwa na Umri wa Miaka Sabini

Mafalda, mwanamke Mkristo kutoka Livorno, ni mwingine wa mapainia wenye bidii au wahudumu wa wakati wote zaidi ya 22,000, katika Italia. Alianza kufanya kazi kama painia akiwa na umri wa miaka 56. “Kazi ya painia,” anaeleza, “inataka kwamba angalau saa 1,000 kila mwaka ziwekwe wakfu kwa kazi ya kuhubiri. Lakini kwa kuwa huo ni ujumbe wa maana, mimi natumia saa 2,000 kila mwaka nikiwa mfanya kazi painia.” Leo Mafalda ana umri wa miaka 70. Mipango yake ni nini? “Miongoni mwa Wakristo wa karne ya kwanza, kulikuwako wake wa nyumbani wenye kufanya kazi kwa bidii walioshiriki katika huduma,” yeye anasema. “Kama wao mimi nataka kuendelea kutangaza Ufalme wa Yehova. Huo ndio mradi wangu maishani.”

Kweli kweli, kuanzia vilele vya mlima wenye kufunikwa na theluji katika Alpino kaskazini mbali sana kwenye kisiwa cha Sisili cha Mediterania kule kusini, mashahidi wa Yehova wa kisasa katika Italia wanaonyesha bidii ya wenzao wa karne ya kwanza. Kila siku ya mwaka wao wanatumia, kwa wastani, zaidi ya saa 100,000 katika kazi ya kuhubiri Ufalme. Na matokeo? Mwaka jana pekee, watu wapatao 12,000 walibatizwa wakawa wahudumu walioagizwa rasmi wa Yehova. Sasa wao, pamoja na wale mashahidi wa Yehova wengine 143,000 ‘wananunua wakati unaofaa’ katika Italia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki