Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 8/15 uku. 31
  • Je! Wewe Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Mikaeli Yule Mwana-Mfalme Mkuu Asimama
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Badiliko la Utawala Karibuni!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kuwatambua Waabudu wa Kweli Katika Wakati wa Mwisho
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 8/15 uku. 31

Je! Wewe Unakumbuka?

Je! wewe umepata kwamba makala za karibuni za Mnara wa Mlinzi zimekuwa zenye thamani yenye mafaa? Basi ona ikiwa unaweza kukumbuka yafuatayo:

◻ Inamaanisha nini kutiwa alama ya wokovu na mwanamume wa kiunabii mwenye kidau cha wino cha mwandishi katika njozi ya Ezekieli? (Ezekieli 9:2-6)

Inamaanisha kwamba mmoja amejitoa mwenyewe wakfu kwa Mungu ili kufanya mapenzi yake, amebatizwa kama mwanafunzi wa Yesu Kristo, naye amevaa utu kama wa Kristo.—4/15, kurasa 11, 12.

◻ Unabii wa Biblia unatumikia makusudi gani?

Mambo ya unabii yanajulisha ukweli kuhusu Mungu, mapenzi yake, na viwango vyake vya adili. Yanaelewesha wazi uhusiano wa wanadamu na Yehova ili kurudisha wanadamu katika upatani pamoja na kusudi Lake, kuongoza kwenye utimizo kamili walo. (Isaya 1:18-20; 2:1-5; 55:8-11)—5/1, ukurasa 5.

◻ Ni njaa gani yenye kufisha inayoenea katika dunia nzima leo?

Ni njaa ya kiroho ya, “kuyasikia maneno ya [Yehova, NW]. (Amosi 8:11)—5/1, kurasa 10, 11.

◻ “Woga wa Yehova” ni nini? (Mithali 1:7, NW)

Ni hofu inayofaa ya kutofanya lisilompendeza yeye kwa sababu tunathamini fadhili za upendo na wema wake. Pia, unamaanisha kukubali kwamba Yehova ndiye Hakimu Mkuu Zaidi Sana na Mwenye Nguvu Zote, kumtumainia yeye kabisa kabisa, na kuchukia yaliyo mabaya machoni pake,—(Zaburi 2:11; 115:11; Mithali 8:13) —5/15, ukurasa 28.

◻ Ni miongozo gani inayoonyeshwa katika 1 Timotheo 5 kuhusu kuwatunza watu wazee-wazee?

Ingawa washiriki wa jamaa wana daraka la kwanza, matatizo ya walio wazee-wazee yanahangaisha kundi lote; utunzaji wao lazima upangwe vizuri; utunzaji wa namna hiyo unawekewa mpaka kwa wale tu ambao kweli wana uhitaji.—6/1, kurasa 9, 10.

◻ Yehova amewasafisha watu wake wakati wa miaka 69 iliyopita katika njia gani kubwa nne?

(1) Kitengenezo; (2) kushiriki katika huduma ya shambani; (3) nuru yenye kuongezeka ya ukweli; (4) kuyaondoa mazoea machafu. —6/15, kurasa 17-20.

◻ Ni katika njia gani mbili neno “-simama” linatumiwa kuhusiana na Mikaeli katika Danieli 12:1?

Mikaeli anaelezwa kuwa ‘amesimama upande wa wana wa watu wako.’ Kristo Yesu amekuwa akitumia mamlaka kwa habari hii juu ya watu wake duniani tangu 1914 alipotawazwa akiwa Mfalme anayetawala wa Ufalme wa Mungu. Pia Danieli anasema hivi: “Wakati huo Mikaeli atasimama.” Hii inaelekeza kwenye utawala wake ukiingia katika hali mpya ambayo katika hiyo atatenda katika njia yenye kutokeza ili kuokoa watu wa Danieli. Hivyo, hawataangamizwa kabisa na serikali za kibinadamu za “wakati wa mwisho” kwa sababu ya mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini. (Danieli 11:40-45)—7/1, kurasa 18, 19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki