Utangazaji—Mambo Ambayo Unaweza Kutimiza
KWA miaka kadha ukurasa wa nyuma wa Mnara wa Mlinzi umekuwa na utangazaji wa vitabu vya Kibiblia. Hivi majuzi, barua moja kutoka Georgia, U.S.A., ilisifu matangazo hayo. Mwanamke mwenye kuandika alieleza kwamba mume na mke ambao yeye na mumeye wanajifunza nao wamejibu majulisho hayo na kujipatia, miongoni mwa vichapo vingine, kanda-kaseti za Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Baadaye, wao walinunua kile kitabu Hadithi za Biblia chenyewe. Mwenye kuandika anaeleza tokeo ambalo kitabu hiki kimekuwa nalo juu ya mume na mke hao:
“Wao wamepewa mandhari-nyuma ya kihistoria kutoka Adamu na kuendelea ambayo juma ili hili ilitokeza kuweza kwao kuona jamii za wanadamu wa rangi tofauti-tofauti kwa maoni yanayofaa. Baada ya kusoma maandiko machache, kama vile Matendo 17:26 na Mwanzo sura 10, na kurejeza kwenye historia ya mwanadamu kutoka kitabu Hadithi za Biblia, Jim alionelea hivi: ‘Mimi nilisema sikuwa na maoni ya ubaguzi hapo mbele, lakini kwa mara ya kwanza, usiku wa leo mimi naweza kusema kwa ukweli kwamba siwabagui.’ “
Mwenye kuandika alimalizia: “Kwa kweli, matangazo yenu yameongoza kwenye ukuzi mwingi wa kiroho katika muda mfupi.”
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kina masimulizi ya Kibiblia 116 ambayo yanampa msomaji wazo juu ya mambo ambayo Biblia inasema hasa. Wewe unaweza kupokea kanda-kaseti hizo au kile kitabu Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au vyote viwili, kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyo hapa chini.
Tia alama katika kimoja au vyote viwili vya visanduku vinavyofuata:
[ ] Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, ile pakiti ya rangi ya kahawia ikiwa na kanda-kaseti nne za Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Mimi nawapelekea Kshs. 150 (Tshs. 560).
[ ] Nipelekeeni Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia chenye picha, na kurasa 256, nami nawapelekea Kshs. 40 (Tshs. 150). Tafadhali lipa mchango ulio sahihi.