Muziki Ambao Unaponya
Mama mmoja kijana kutoka Iowa, U.S.A., anaeleza: “Mimi nalazimika kuandika niwaambia ninyi jinsi zilivyo za faida kubwa kwangu na jamaa yangu kanda zenu [za piano] ‘Mwimbieni Yehova Sifa.’ Kila siku, mimi namyumbisha-yumbisha mtoto wangu wa miaka mitatu ili alale. Lakini kwanza sisi tunatia moja ya zile kanda, halafu mimi natoa kitabu-cha-nyimbo na kuimba pamoja wakati kisichana hicho kinapokuwa kikienda kulala.”
Mama huyo anaendelea kusimulia uzaliwa wa mapema mno wa mtoto wake wa karibuni zaidi na tatizo kubwa la kivulana hicho kikiwa katika chombo cha kusaidia kupumua, kikilazimika kuwa na mrija ulioteremshwa katika koo lacho. Yeye anasimulia hivi: “Mimi niliwauliza wauguzi kama sisi tunaweza kuleta rekoda ya kuimbisha kanda na kanda fulani za kimuziki kwa ajili yake. Wao walisema tungeweza. Wauguzi hao walistaajabu kuona jinsi kanda hizo zilivyosaidia kivulana hicho kustarehesha fikira. Wao walitoa elezo la kwamba kila wakati ambapo yeye angeanza utukutu, jambo tu ambalo wangefanya ni kumwimbishia muziki wake. Muuguzi mmoja hata alisema: ‘Laiti sisi tungekuwa na muziki wa aina hii kwa ajili ya vitoto vyote. Ni wa kupendeza sana. Mlio ule tu ambao vitoto hivi vinasikia ni ule wa pi-pi-pi unaotoka katika vyombo vinavyoendesha utendaji wa miili yavyo.’”
Kwa kweli, wengi wamepata muziki huo kuwa wenye kuponya nafsi yao. Ile pakiti yenye sura ya kupendeza inayoitwa “Mwimbieni Yehova Sifa,” yenye kaseti nane, inapatikana kwa Kshs. 300/- (Tshs. 1100/- RWF 1500) tu. Wewe unaweza kupokea pakiti yako kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyo hapa chini pamoja na malipo yako.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, ile pakiti “Mwimbieni Yehova Sifa” pamoja na zile kanda-kaseti nane za kimuziki. Mimi nawapelekea Kshs. 300/-(Tshs. 1100/- RWF 1500)