Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 9/1 uku. 10
  • ‘Vitu Vyenye Kutamanika Vyaja Ndani’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Vitu Vyenye Kutamanika Vyaja Ndani’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • “Vitu Vinavyotamaniwa” Vinaijaza Nyumba ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Acheni Wote Wamtukuze Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 9/1 uku. 10

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

‘Vitu Vyenye Kutamanika Vyaja Ndani’

MNABII Hagai aliandika maneno haya katika 520 K.W.K.: “Na mimi nitatikisa mataifa yote, na vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote ni lazima vije ndani; na mimi nitajaza nyumba hii utukufu,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Hagai 2:7, NW) “Vitu vyenye kutamanika” vya mataifa yote ambavyo vinajaza nyumba ya Yehova utukufu ni waabudu wake wanaomcha Mungu. Watu hao wenye mioyo yenye ufuataji haki wanaitikia habari njema katika Italia, hivi kwamba sasa kuna Mashahidi 166,000 wanaofundisha watu Biblia katika taifa hilo. Makasisi Wakatoliki katika Italia wanauona ukuzi wetu usio wa kawaida kuwa “tukio lenye kuendelea kutisha” ambalo ‘linawahangaisha na kuwafadhaisha.’ Acha mtafuta ukweli mmoja wa huko asimulie lililotukia kwake.

“Mimi nilikuwa mwalimu wa katekismu kwa miaka kumi, nami nilikuwa nimesadikishwa kwamba hii ndiyo njia ya kuonyesha Mungu na jirani upendo wangu. Hata ijapokuwa nilikuwa na rafiki aliyekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, sikuchukua wakati kamwe kusikiliza ujumbe wa Biblia. Hata hivyo, wakati fulani uliopita, Mashahidi waliponitembelea, mimi niliwakaribisha. Nilitaka kuwaambia wasimtembelee mama mkwe wangu tena, kwa kuwa alikuwa akihisi akiwa amevurugika. ‘Badala ya kutembelea watu wazee-wazee,’ mimi nikawaambia, ‘zungumzeni na watu kama mimi.’ Kuanzia wakati huo na kuendelea walikuja kwenye nyumba yangu, lakini wakati wowote walipogusia jambo la kimafundisho, ningewaomba waahirishe mazungumzo mpaka baadaye ili niweze kuchunguza habari hiyo.

“Niliongea na makasisi kadhaa na nikaona kwamba hawakuwa na jibu la Biblia. Mmoja wao, mmisionari, aliniambia kwamba si jambo la maana sana kuhudhuria Misa. Alisema, ‘ingawaje, kwa kielelezo katika nchi kama Brazili watu hufanya mambo mengine badala ya kwenda kwenye Misa. Jambo la maana ni kumtumikia Mungu katika njia bora ambayo mtu anaweza.’ Maneno haya yalinipa nguvu ya kukata uhusiano na Kanisa Katoliki. Kasisi mwingine alimwambia mume wangu, ambaye alikuwa Mkatoliki pia, ya kwamba ikiwa mimi nataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, anapaswa aniache mimi nifanye hivyo kwa sababu Mashahidi wa Yehova wana kasoro moja tu, ile ya kuwa wenye bidii mno. Mimi nimebatizwa karibuni tu pamoja na mmoja wa wana wangu. Mume wangu anajifunza Biblia pia na kuonyesha upendezi katika ujumbe wa Ufalme.”

Yehova anapotikisa mataifa kwa kujulisha wazi hukumu zake duniani, watu wengi wenye mbetuko wa uadilifu wanaacha mazoea ya utovu wa haki ili wafuate kanuni za Biblia. Kabla ya kujifunza ukweli, mwanamume mmoja Mwitalia aliingia katika deni kubwa akifikiri kwamba angeweza kulipa deni lake kwa pesa za mshahara wake wa kawaida na “bakshishi” za utovu wa haki alizokuwa akipokea. Alipopata maarifa ya ukweli, yeye alifanya uamuzi mgumu wa kuacha kukubali “bakshishi” za utovu wa haki. Yeye pamoja na mke wake walibatizwa na mara moja wakaanza kutumikia katika huduma ya wakati wote. Katika hospitali anamofanya kazi, mara nyingi yeye hulazimika kuvua maiti nguo, na mara kwa mara amepata zikiwa na pesa nyingi sana. Kwa kielelezo, wakati mmoja alipata lire 150,000 (karibu dola 115), na wakati mwingine lire 600,000 (karibu dola 460). Kwa kuwa mfuataji haki, yeye alirudisha pesa hizo, na hilo lilimpa fursa ya kuzungumza na wasimamizi wa kazi ya hospitali na madaktari kuhusu ukweli. Wasimamizi wa kazi ya hospitali walimpelekea barua za sifa kwa mwenendo wake wa kufuata haki na kujali madaraka yake.

Mambo haya yaliyoonwa kutoka Italia ni mifano tu ya jinsi “vitu vyenye kutamanika” vinaacha mfumo huu mbovu wenye jeuri na kuja kwenye tengenezo safi, lenye amani la Yehova kabla hajatikisa mfumo wa Shetani wa kisiasa uingie katika uharibifu katika Har–Magedoni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki