Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 12/1 uku. 32
  • ‘Kilisaidia Binti Zetu Wawe na Ukaribu Zaidi’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kilisaidia Binti Zetu Wawe na Ukaribu Zaidi’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 12/1 uku. 32

‘Kilisaidia Binti Zetu Wawe na Ukaribu Zaidi’

Akiandikia ofisi ya tawi ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi mwaka uliopita, mwalimu mmoja wa shule katika Murewa, Zimbabwe alisema kwamba hilo ndilo jambo lililotimizwa na Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Yeye alipokea kichapo kutoka kwa mwalimu mwenzake na akaripoti hivi:

“Nilifuata ushauri wake kuhusu jinsi ya kunufaika kabisa na kitabu hicho, kwanza nikiwa pamoja na binti yangu mchanga zaidi wa miaka 8, halafu pamoja na wengine wawili, wenye umri wa miaka 16 na 18, waliokuwa kwenye Shule ya Sekondari ya Kulala katika eneo la kwetu. Nina raha nyingi kuwajulisha nyinyi kwamba itikio ambalo limetoka kwa binti zangu wote watatu limekuwa la kutia moyo kweli kweli. Tangu wakati huo mwenendo wao wa kiadili umekuwa ukibadilika kuwa bora kwa njia yenye kuonekana wazi.” Mama huyo aliongezea hivi: “Kitabu hicho kimekuwa na mafanikio ya kusaidia binti zetu wawe na ukaribu zaidi kwa sisi, wazazi wao, kuliko wakati mwinginewo wote.”

Kichapo hiki cha kurasa 256, chenye kurasa ambazo zalingana ukubwa na gazeti hili, chaweza kupokewa kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyoambatanishwa hapa pamoja na Kshs. 60/= (Tshs. 360; RWF 250). Masimulizi 116 ya Biblia ya kitabu hiki yampa msomaji wazo fulani kuhusu mambo yaliyomo hasa katika Biblia. Hadithi hizi zimo katika utaratibu ambao matukio yalitendeka katika historia. Utaliona kuwa ni jambo lenye msaada kweli kweli katika kujifunza ni wakati gani mambo yalipotukia katika historia, kuhusiana na matukio mengine. Kitabu hiki kina picha zenye kupendeza, na kina herufi za chapa kubwa.

Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu Kitabu Changu cha Hadhithi za Biblia, ambacho kwa ajili yacho nawapelekea Kshs. 60/=

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki