Kwa Nini Yehova Amefunua Jina Lake?
Kitabu cha maelezo kuhusu “Agano la Kale” kilichochapishwa katika Polandi katika 1964 kilijibu swali hili kwa njia yenye kuamsha sana mawazo. Chini ya muhuri wa idhini ya uchapaji kutoka Kanisa Katoliki la Roma, Dakt. Stanislaw Lach, profesa kwenye Chuo Kikuu cha Lublin, aliarifu hivi:
“Watu waliofidiwa wana daraka la kuchukua jina la Mungu mbele ya ainabinadamu.” Lilikuwa daraka la Waisraeli kufanya jitihada ili “kwamba Wasio Wayahudi wabariki jina la Jahwe [Yehova] na kwamba wasikufuru” hilo. “Jahwe lina maana . . . Ulimwengu utahukumiwa kwa kutegemea tendo-mwitikio kuelekea wale ambao huungama jina hilo.” Profesa huyo alijulisha wazi kwamba “jina Jahwe litakuwa kubwa miongoni mwa mataifa. Litatandaa kote kote ulimwenguni. Huo ndio uliokuwa ufiko wa . . . jina hilo kwa Musa.”
Ndiyo, kama vile Malaki 1:11, NW, hutoa unabii: “‘Jina langu litakuwa kubwa miongoni mwa mataifa,’ Yehova wa majeshi amesema.” Na ni nani leo wanaojulisha wazi jina hilo ulimwenguni pote ili kwamba “kila mmoja ambaye huitia jina la Yehova aokolewa”? Ni Mashahidi wa Yehova! Tendo-mwitikio la halaiki ya watu kwa hawa “watu kwa ajili ya jina Iake,” ndiyo, “wale ambao huungama jina hilo,” ni jambo la uhai na kifo kwao. Tendo-mwitikio lako wewe ni nini kwa Yehova na Mashahidi wake?—Matendo 2:21; 15:14; linganisha Malaki 3:16-18, NW.