Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/1 kur. 26-29
  • Anguko la Babuloni Latangazwa Katika Japani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Anguko la Babuloni Latangazwa Katika Japani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Japani Yaongeza Kasi
  • Utumishi wa Painia Msaidizi
  • Siku ya Pekee ya Utendaji
  • Ushahidi wa Barabarani
  • Ugawanyaji Magazeti
  • Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/1 kur. 26-29

Anguko la Babuloni Latangazwa Katika Japani

“AMEANGUKA! Babuloni Mkubwa ameanguka, yeye ambaye alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake!” Tangazo hilo la kimalaika lenye kuchochea lilisikiwa mara ya kwanza na mtume Yohana kule nyuma katika karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu. Hata hivyo, wakati wetu, katika “siku ya Bwana,” limefanyiwa mwangwi na Mashahidi Wakristo wa Yehova huku likisikiwa na ainabinadamu yote.—Ufunuo 1:10; 14:8, NW.

Babuloni Mkubwa ndio mfumo wa ulimwenguni pote wa dini bandia, na Jumuiya ya Wakristo ndiyo sehemu yao yenye kulaumika zaidi. Muda wote wa “wakati wa mwisho,” hukumu za Yehova dhidi yake zimetangazwa kijasiri na Mashahidi wa Yehova kuzunguka ulimwengu. (Danieli 12:4) Kwa kielelezo, matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya Aprili na Mei mwaka uliopita yalikuwa na makala zenye nguvu nyingi zenye kufichua hatia ya dini bandia na uharibifu wayo unaokuja. Nakala zaidi ya milioni 50 za matoleo hayo ziligawanywa ulimwenguni pote—huo ukiwa ni ujulisho wazi wa maangamizi yatakayopata Babuloni Mkubwa!

Japani Yaongeza Kasi

Kielelezo cha idili ya Mashahidi wa Yehova kwa matoleo hayo ya pekee kilionwa katika Japani, ambayo ndiyo ngome ya sehemu ya Washinto-Wabuddha ya Babuloni Mkubwa. Katika Japani toleo la Desemba 1988 la Huduma ya Ufalme Yetu liliarifu makundi juu ya kampeni ya pekee ya utumishi wa shambani iliyopangiwa miezi ya Aprili na Mei 1989. Miito ya kuunga mkono utendaji huu wa pekee wa magazeti ilitokezwa katika matoleo yaliyofuata ya Huduma ya Ufalme Yetu, na pia kupitia barua zilizoandikwa kwa makundi na mabaraza ya wazee.

Itikio lilikuwa la kutokeza. Kwa msaada wa Yehova, wakati wa miezi miwili hiyo ya mwaka uliopita, Japani ilipokea ushahidi wa kadiri isiyopata kufanyika.

Utumishi wa Painia Msaidizi

Tangazo la Desemba 1988 lilihusisha ndani maneno haya: “Sisi twawatia moyo mwe na mradi wa kuonea shangwe upainia msaidizi wakati wa Aprili na Mei, hasa Aprili.” Wazo hili lilirudiwa katika toleo la Februari 1989 la Huduma ya Ufalme Yetu, lililohimiza akina ndugu ‘warekebishe ratiba yao ya kila siku ili wahudumu wengi waliojiweka wakfu wajiandikishe kwa wingi wa kadiri iwezekanayo wawe mapainia wasaidizi katika Aprili.’

Mashahidi walizingatia moyoni vikumbusha hivyo. Tokeo likawa nini? Kukawa na kilele cha wakati wote katika hesabu ya mapainia wasaidizi. Katika Machi 1989 hesabu ya mapainia wasaidizi ilikuwa tayari imekwisha kufikia kilele kipya cha 24,115. Lakini katika Aprili tarakimu hiyo ilikuwa imeongezeka karibu maradufu na kuwa 41,055. Lo, jitihada kubwa ajabu!

Katika makundi mengi, wahubiri wote au walio wengi walishiriki sehemu fulani ya utumishi wa wakati wote katika muda wa ile miezi miwili ya utendaji wa pekee. Mara nyingi hiyo ilihitaji kutengeneza kwingi. Mke mmoja wa kinyumbani alitia shaka kama angeweza kushiriki, kwa kuwa yeye huishi takribani meta 900 juu milimani ambako huduma za usafirishaji ni chache. Hata hivyo, alitaka kikweli kuwa painia msaidizi. Kwa hiyo wazee wakapanga kumsaidia kwa usafiri, naye, pamoja na wahubiri wengine wote katika kundi, wakaona shangwe ya kupainia kwa mwezi mmoja.

Uongozi mzuri wa wazee ulifanyiwa kielelezo katika Wilaya ya Osaka, Jiji la Takatsuki, Kundi la Otsuka lenye wahubiri 77, ambako wazee na watumishi wa huduma wote walikuwa miongoni mwa wale 73 walioshiriki namna fulani ya utumishi wa painia. Mapainia hao walikuwa ni kutia ndani pia wahubiri wachanga wote waliobatizwa ambao wangali wanahudhuria shule. Roho ya upainia iliyoonyeshwa na Mashahidi wachanga hawa ilikuwa kifananisho halisi cha ile ambayo huonwa katika makundi mengi. Kwa kielelezo, kati ya matineja 23 waliobatizwa katika Kundi La Heiwadai katika Wilaya ya Tokyo, 11 ni mapainia wa kawaida, na 11 walifanya upainia msaidizi katika Aprili. Katika kundi hilo, jumla ya wahubiri 93 walipainia mwezi uo huo.

Siku ya Pekee ya Utendaji

Toleo la Machi la chapa ya Kijapani ya Huduma ya Ufalme Yetu liliwatia moyo akina ndugu kwa maneno haya: “Kazi ya magazeti imeungwa mkono si katika Jumamosi za pili na nne tu bali pia katika kila Jumamosi ya mwezi. Bidii ambayo akina ndugu wanaonyesha ni ya kusifika. Katika Aprili kazi ya magazeti imeratibiwa pia kwa kila Jumamosi, lakini tafadhali mfanye jitihada ya pekee kuweka kando Aprili 8 iwe siku ya magazeti ili kila mtu ashiriki kazi ya magazeti siku hiyo. Ili kuvumisha onyo kwa wote watakaosikiliza, yahitajiwa kabisa kugawanya kwa mapana matoleo haya yaliyo ya wakati ufaao.”—Isaya 61:2; Ufunuo 18:4, 5.

Katika Februari Huduma ya Ufalme Yetu ya Kijapani ilikuwa imekazia kazi hii muhimu. Ilisema hivi: “Jumamosi ya pili, Aprili 8, acheni kila mmoja wa Mashahidi wa Yehova katika Japani—ambao sasa hesabu yao ni zaidi ya 130,000—ashiriki kazi ya magazeti.” Wazee walitiwa moyo kuratibu utendaji wa magazeti wa aina tofauti-tofauti wenye kuchukua siku nzima ili wengi iwezekanavyo waweze kushiriki. Siku hiyo ilifanikiwa ajabu, shukrani kwa itikio chanya la wazee na tegemezo la moyo mzima la wahubiri wale wengine. Tungeweza kusema kwamba siku hiyo kileleta kilifikiwa katika Japani katika kupiga mbiu ya hukumu za Yehova juu ya Babuloni Mkubwa.

Mathalani, katika Kundi la Ushioda, katika Jiji la Yokohama, wazee walipanga utumishi ambao ungeendelea kwa saa 13, kuanzia saa 1:00 hadi saa 2:00 asubuhi. Vyenye kuhusishwa vilikuwa vipindi viwili vya ushahidi wa barabarani, na pia wakati wa kuzuru watu ambao hapo kwanza hawakuwa wamekuwa nyumbani na wa kufanya ushahidi wa kawaida wa nyumba kwa nyumba. Wahubiri walio wengi waliweza kushiriki angalau moja ya sehemu kuu za utumishi uliopangwa, na hesabu fulani walishiriki katika karibu kila sehemu ya utendaji uliopangwa.

Utumishi wenye kuendelea ulipangwa pia katika Kundi la Jonan, Jiji la Fukuoka. Huko, mipango ilifanywa ikihusisha muda wa kuanzia saa 2:00 hadi saa 3:00 asubuhi, kukiwa na pumziko fupi tu kati ya mchana. Wakati ulihusishwa ndani wa kutoa ushahidi nyumba kwa nyumba, kuzuru eneo la kibiashara na maeneo yenye maduka, na kutembelea mahali ambapo hakuna mtu aliyekuwa amefikiwa katika ziara zilizotangulia. Mashahidi fulani katika kundi hilo waliripoti kufikia saa nane za utendaji wa kuhubiri kwa siku hiyo!

Itikio la moyo mzima la akina ndugu lilionwa katika Wilaya ya Wakayama, ambako wahubiri wote 55 katika Kundi la Kainan walishiriki katika siku hiyo ya pekee ya utendaji. Dada mmoja huko, painia wa kawaida, alijifungua siku ya Aprili 7. Je! hiyo ilimzuia kutoa ushahidi siku ya Aprili 8? Sivyo. Alitoa magazeti huko huko hospitali! Akionyesha roho kama hiyo, ndugu mmoja kutoka Wilaya ya Osaka alilazimika kushughulikia mambo fulani mahali pake pa kazi ya kimwili siku ya Aprili 8. Angeweza kushirikije katika utendaji huo wa pekee? Alifanya mahali pake pa kazi pakawa eneo lake na akajipatia maandikisho matano.

Dada mmoja katika Wilaya ya Saitama alitamani kushiriki katika utendaji wa pekee wa siku hiyo, lakini alilazimika kusafiri kilometa karibu 1,280 kwenda Jiji la Asahikawa pamoja na mume wake asiyeamini. Ingawa hivyo, yeye hakukata tamaa. Katika Asahikawa, alienda pamoja na watoto wake wadogo wawili kwenye kituo cha gari-moshi, na huko, akiwa nje ya kituo, akapata kile alichokuwa ametumainia: umati wa wahubiri kutoka kundi la huko wakiwa wamejitia katika utumishi wa shambani. Aliweza kushiriki pamoja nao katika utendaji mbalimbali wa siku hiyo.

Ushahidi wa Barabarani

Hasa Huduma ya Ufalme Yetu ya Kijapani iliwatia moyo wazee kupanga ushahidi wa barabarani uwe Aprili 8, na hiyo ikawa sehemu kubwa ya siku hiyo ya pekee. Kama ilivyotukia, kukawa na mwanguko mkubwa wa sehemu zote nchini, lakini hiyo haikupozesha idili ya akina ndugu. Walio wengi walionyesha roho ileile iliyoonwa katika dada watatu wenye vizuizi katika Kundi la Minamata, Wilaya ya Kumamoto. Japo umri wao—65, 80, na 85—waliivumilia hali mbaya ya hewa na wakawa kitia-moyo kizuri kwa wengine wa kundi hilo; pia walivuta uangalifu wa wapita-njia wengi.

Alipokuwa akifanya ushahidi wa barabarani, dada mmoja katika Kundi la Magharibi la Jiji la Kashiwa aliuliza mwanamume mmoja hivi: “Je! wewe umepata kusikia juu ya Babuloni Mkubwa?” Alipotoa matoleo ya Aprili ya magazeti, mwanamume huyo alisema, “Sipendezwi” na kwenda zake. Hata hivyo, alipokuja na kusimama penye kivuko cha reli, alikuwa akijisemea-semea, “Babuloni Mkubwa ni nini?” Ndugu mmoja mwenye kufanya ushahidi wa barabarani alimsikia kwa mbali na akatembea naye kando ya barabara, akimweleza Babuloni Mkubwa ni nini. Mwanamume huyo aliyapokea magazeti.

Makundi fulani yalikuwa hayajapata kamwe kufanya ushahidi wa barabarani. Lakini tangu Aprili 8, wameifanya kuwa sehemu ya kawaida ya utendaji wao. Na si ajabu! Ushahidi wa barabarani ni njia yenye mafanikio sana ya kuwapata watu ambao hawapatikani kwa njia nyinginezo. Dada mmoja katika Jiji la Naha, Okinawa, alijitia katika ushahidi wa barabarani nje ya jengo la ofisi ambalo Mashahidi wa Yehova hawaruhusiwi kuingia kwa kusudi la kutoa ushahidi. Aliangusha magazeti 12 katika muda wa saa moja kwa kuwafikia wenye kuingia na kuondoka katika jengo hilo.

Dada mmoja katika Jiji la Muroran, Hokkaido, alijitia katika ushahidi wa barabarani nje ya maduka makubwa katika kitovu cha jiji. Alimwambia hivi mwanamume mmoja aliyeyapokea magazeti: “Ikiwa ungependa kujifunza mengi zaidi, sisi twaweza kukuzuru nyumbani kwako.” Akampa dada huyo anwani yake, namba ya simu, ramani ya kwenda kwenye nyumba yake, na nyakati ambazo angekuwa nyumbani! Juma lililofuata dada huyo na ndugu mwingine walimzuru wakapata kwamba yeye huishi katika jengo ambalo halikuruhusiwa kwa ziara za kihuduma zenye kufanywa kikawaida na Mashahidi wa Yehova. Kwa kujisomea Biblia yeye binafsi mwanamume kijana huyo alikuwa amesadikishwa kwamba Jumuiya ya Wakristo haina upendeleo wa Mungu. Yeye alikuwa akitafuta Ukristo wa kweli na alifurahi kuanza funzo la nyumbani la Biblia lenye ukawaida.

Mhubiri wa kike katika Jiji la Kawasaki alishiriki ushahidi wa barabarani alasiri ya Aprili 8. Mwishoni mwa wakati huo aliokuwa amepanga, alinena na mtu mmoja wa mwisho, mwanamke mchanga aliyesema kwamba hapo kwanza alikuwa amejifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Lakini alikuwa amekuta upinzani kutoka kwa wazazi wake na baadaye akawa ameingia chuo kikuu na kuhamia bweni fulani. Kwa hiyo akaacha kujifunza. Hata hivyo, kwa sababu ya ushahidi wa barabarani, aliterema kuanza upya funzo lake la Biblia na tayari anahudhuria mikutano.

Ugawanyaji Magazeti

Kutokana na vile wengi waliunga mkono utendaji huo wa pekee, maangusho ya magazeti—hasa yale yenye jumbe za hukumu dhidi ya Babuloni Mkubwa—yalikuwa makubwa ajabu. Mhubiri mmoja wa kundi katika Wilaya ya Osaka aliangusha magazeti 205 katika Aprili. Katika Jiji la Kagoshima, Kundi la Mashariki, wahubiri 14 waliangusha magazeti zaidi ya mia moja kila mmoja, na kikundi cha eneo lililo peke yalo cha wahubiri 12 katika Mji wa Ogawa, Wilaya ya Ibaraki, kiligawanya jumla ya magazeti 1,388 wakati wa Aprili.

Kwa kweli, katika Japani kwa ujumla, mgazeti 3,293,266 yaliangushwa katika Aprili wa mwaka uliopita—asilimia 92 zaidi ya Aprili wa 1988! Lo, ujumbe wa hukumu za Yehova ulivuma kwa nguvu kama nini dhidi ya Babuloni Mkubwa!

Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida

Hakika, kama ilivyo katika sehemu nyingine zote za ulimwengu, Mashahidi wa Yehova katika Japani walikuwa na mtazamo chanya na bidii katika masika ya 1989. Mambo waliyoona yalitoa uthibitisho wa wazi kwamba Yehova alibariki bidii yao na akaunga mkono jitihada zao za kutangaza hukumu zake dhidi ya dini bandia. Kwa baadhi yao, haikuwa rahisi kushiriki; hata hivyo, walipiga moyo konde, na Yehova alibariki bidii yao. Wengi huishi katika eneo ambalo hufanyiwa kazi mara nyingi, lakini walionyesha roho ileile ya kufanya hima na kuwa wenye idili kama ndugu zao katika maeneo mengine. Katika visa vyote, maneno ya Isaya yalithibitika kuwa kweli: “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.”—Isaya 40:29.

Bila shaka maono yao yaliwakumbusha maneno ya mtume Paulo: “Sisi tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili uwezo unaopita ulio wa kawaida upate kuwa wa Mungu na si ule unaotokana na sisi wenyewe.” (2 Wakorintho 4:7, NW) Ndiyo, wakati mtu awekapo huduma ya Kikristo, “hazina hii,” kwanza katika maisha yake, yeye huupata “uwezo unaopita ulio wa kawaida” ambao Mungu hutoa. Yehova na aendelee kutumia watumishi wake katika Japani na katika mabara mengine yote ili kutoa ushahidi kamili kabla ya mwisho kuja.—Mathayo 24:14.

Mwaka huu, matoleo ya Aprili na Mei ya Mnara wa Mlinzi yatakazia mfululizo wa jaladani kuhusu “Nani Ataongoza Ainabinadamu Kwenye Amani?” “Amani ya Ulimwengu—Kwa Kweli Itamaanisha Nini”? “Mamilioni Ambao Sasa Ni Wafu Wataishi Tena,” na “Har–Magedoni—Lini?” Kwa nini usipange kushiriki habari hizi pamoja na jirani zako? Uwe na uhakika kwamba watu wengi iwezekanavyo wajulishwa habari njema nzuri ajabu ambazo Mungu amehifadhi katika Biblia kwa ajili ya siku yetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki