Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/15 uku. 7
  • Musa Akiwa na Pembe Kishani cha Kisanaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Musa Akiwa na Pembe Kishani cha Kisanaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Yesu Kristo Alikuwaje Nabii Kama Musa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Musa—Alionyesha Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/15 uku. 7

Musa Akiwa na Pembe Kishani cha Kisanaa

IKIWA wewe umepata kuzuru Italia, ingeweza kuwa kwamba umeona sanamu maarufu ya Michelangelo kuhusu Musa aliyeketi, ambayo sasa iko kwenye Kanisa la St. Peter katika Chains, katika Roma. Mchongo huo wa karne ya 16 huonekana wa kishani, kwa maana huonyesha Musa akiwa na pembe zenye kutokeza katika kichwa chake! Kwa uhakika, wasanii kadhaa wameonyesha Musa akiwa na pembe. Kwa nini? Je! Biblia huandaa msingi wowote kwa wazo hilo?

Tafsiri Latin Vulgate ya Biblia hutuambia kwamba kufuata mazungumzo yake pamoja na Mungu juu ya Mlima Sinai, uso wa Musa ‘ulitiwa pembe.’ (Kutoka 34:29, 30, 35; linganisha Douay Version.) Vulgate ilipata kupendwa na watu wengi katika sehemu kubwa ya Jumuiya ya Wakristo na hivyo ikaathiri jinsi maandiko yalivyoeleweka.

Hata hivyo, neno la Kiebrania lililotafsiriwa ‘ulitiwa pembe’ lina maana pia ya ‘kutokeza mionzi’ au ‘kung’aa.’ (Ona kielezichini cha Douay Version kwenye Kutoka 34:29.) Kulingana na Theological Wordbook of the Old Testament, neno hilo “huonyesha umbo la upembe (pembe) badala ya kitu chenyewe.” Na kwa maoni ya ufananisho, kwa kweli mionzi ya nuru hushabihi pembe.

Uhakika wa kwamba uso wa Musa ulitokeza mionzi unaelezeka, kwa maana utukufu wa Yehova ulikuwa ndio wapita tu. (Kutoka 33:22; 34:6, 7) Paulo huthibitisha huo kuwa ndio uelewevu sahihi, akiandika juu ya “utukufu” wa uso wa Musa, wala si wa “pembe” zake.—2 Wakorintho 3:7.

Hivyo uelewevu sahihi wa maneno ya Kibiblia huongoza katika kupata maarifa yenye kupenya ndani zaidi juu ya ripoti hiyo ya Biblia. Kwa hiyo, pembe zilizo katika sanamu maarufu ya Michelangelo kuhusu Musa ni kishani cha kisanaa tu kilichotokana na kosa la tafsiri lililosahihishwa muda mrefu uliopita.

[Hisani katika ukurasa wa  7]

Based on Short History of Art

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki