Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/15 kur. 10-14
  • “Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza Lake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza Lake
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maneja (Msimamizi) wa Nyumba Katika Karne ya Kwanza
  • Baraza Linaloongoza la Nyumba
  • Wakati wa Kuhesabu kwa Maneja (Msimamizi) wa Nyumba
  • “Mtumwa” na Baraza Lenye Kuongoza Wakati wa Mwisho Ulipokuwa Ukikaribia
  • Uwe Mshikamanifu kwa Kristo na kwa Mtumwa Wake Mwaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Msimamizi-nyumba Mwaminifu na Baraza Lake Linaloongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara”
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/15 kur. 10-14

“Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza Lake

“Ni nani kwa kweli aliye mtumwa mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana-mkubwa wake aliweka juu ya watu wake wa nyumba, kuwapa chakula chao kwa wakati unaofaa?”—MATHAYO 24:45, NW.

1. Kwa nini Yehova ana nia ya kutoa mamlaka, naye amefanya hivyo kwa nani hasa?

Yehova ni Mungu wa utaratibu. Pia yeye ndiye Chanzo cha mamlaka yote iliyo halali. Akiwa na uhakika katika uaminifu-mshikamanifu wa viumbe wake waaminifu, Yehova ana nia ya kuwapa wengine mamlaka. Mmoja ambaye amempa mamlaka nyingi zaidi ni Mwana wake, Kristo Yesu. Kweli kweli, Mungu ‘alivitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamfanya kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kundi.’—Waefeso 1:22, NW.

2. Paulo aita kundi la Kikristo nini, na Kristo amempa nani mamlaka?

2 Mtume Paulo aita kundi la Kikristo “nyumba ya Mungu” na kusema kwamba Yesu Kristo, akiwa Mwana mwaminifu wa Yehova, aliwekwa juu ya nyumba hii. (1 Timotheo 3:15; Waebrania 3:6) Naye Kristo huwapa mamlaka washiriki wa nyumba ya Mungu. Twaweza kuona hilo katika maneno ya Yesu yaliyoandikwa kwenye Mathayo 24:45-47, NW. Yeye alisema hivi: “Ni nani kwa kweli aliye mtumwa mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana-mkubwa wake aliweka juu ya watu wake wa nyumba, kuwapa chakula chao kwa wakati unaofaa? Mwenye furaha ni mtumwa yule ikiwa bwana-mkubwa wake wakati wa kuwasili amkuta akifanya hivyo. Kweli kweli mimi nasema kwenu nyinyi, Yeye atamweka juu ya mali zake zote.”

Maneja (Msimamizi) wa Nyumba Katika Karne ya Kwanza

3. Ni nani wanaojumuika kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” na ni mtajo gani unaotumiwa kwao wakiwa mmoja mmoja?

3 Kutokana na kujifunza kwetu Maandiko kwa uangalifu, twajua kwamba kwa ujumla washiriki waliopakwa mafuta kwa roho wa nyumba ya Mungu katika wakati wowote ule wenye kuhusika hujumuika kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” “mtumishi-nyumbani,” au “maneja (msimamizi) wa nyumba.” Wakiwa mmoja mmoja, washiriki wa nyumba ya Yehova huitwa “watu wa nyumba” au “baraza la watumishi.”—Mathayo 24:45; Luka 12:42; Reference Bible, kielezochini.

4. Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu alitokeza swali gani, naye alijifananisha na nani?

4 Miezi kadhaa kabla ya kifo chake, Yesu alizusha swali hili, lililoandikwa kwenye Luka 12:42, NW: “Kwa kweli ni nani huyo aliye mtumishi-nyumbani mwaminifu, aliye na busara, ambaye bwana-mkubwa wake ataweka juu ya baraza la watumishi wake ili aendelee kuwapa kipimo chao cha magawio ya chakula kwa wakati unaofaa?” Halafu, siku chache kabla ya kifo chake, Yesu alijifananisha na mtu, aliye karibu kusafiri ng’ambo, ambaye aliita watumwa wake na kuwakabidhi mali yake.—Mathayo 25:14.

5. (a) Ni lini Yesu alipowapa wengine mgawo wa kutunza mali zake? (b) Ni mgawo gani wenye kufika mbali ambao Kristo aliwapa wale ambao wangekuwa sehemu ya maneja (msimamizi) wa nyumba yake mwenye washiriki wengi?

5 Ni lini Yesu alipowapa wengine mgawo wa kuangalia mali zake? Hili lilitukia baada ya ufufuo wake. Katika maneno yake yenye kufahamika kwenye Mathayo 28:19, 20, Kristo alimpa kwanza maneja wa nyumba mwenye washiriki wengi mgawo wenye kufika mbali wa kufundisha na kufanya wanafunzi. Kwa kutoa ushahidi “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” wakiwa mmoja mmoja, watumishi hao wangepanua shamba la kimisionari ambalo Yesu alianza kusitawisha wakati wa huduma yake ya kidunia. (Matendo 1:8, NW) Hii ilihusisha ndani kutenda kwao wakiwa “mabalozi badala ya Kristo.” Wakiwa “watumishi-nyumbani wa siri takatifu za Mungu,” wangefanya wanafunzi na kuwagawia chakula cha kiroho.—2 Wakorintho 5:20; 1 Wakorintho 4:1, 2.

Baraza Linaloongoza la Nyumba

6. Jamaa ya mtumishi-nyumbani wa karne ya kwanza ilivuviwa kimungu kuandaa nini?

6 Kwa ujumla, Wakristo waliopakwa mafuta kwa roho wangekuwa mtumishi-nyumbani, au maneja wa nyumba, aliyepewa mgawo wa kugawanya chakula cha kiroho cha wakati unaofaa kwa washiriki mmoja mmoja wa nyumba ya Mungu. Kati ya miaka 41 na 98 W.K., washiriki wa jamii ya mtumishi-nyumbani wa karne ya kwanza walivuviwa kimungu kuandika habari za kihistoria 5, barua 21, na kitabu cha Ufunuo kwa manufaa ya ndugu zao. Maandishi hayo yaliyovuviwa yalikuwa na chakula cha kiroho kizuri kwa ajili ya watu wa nyumba, yaani, wapakwa-mafuta mmoja mmoja wa nyumba ya Mungu.

7. Ni kwa kusudi gani Kristo alichagua hesabu ndogo ya wanaume kutoka kwenye jamii ya mtumwa?

7 Ingawa kwa ujumla Wakristo wote wapakwa-mafuta hujumuika kuwa nyumba ya Mungu, kuna ushuhuda mwingi kwamba Kristo alichagua hesabu ndogo ya wanaume kutokana na jamii ya mtumwa watumikie wakiwa baraza lenye kuongoza lionekanalo. Historia ya mapema ya kundi yaonyesha kwamba mitume 12, kutia na Mathiya, walikuwa msingi wa baraza lenye kuongoza la karne ya kwanza. Matendo 1:20-26, NW, hutuandalia kionyeshi cha jambo hilo. Kuhusiana na mtu wa kuchukua mahali pa Yuda Iskariote, mtajo wafanywa hapo kuhusu “cheo chake cha uangalizi” na “huduma hii na utume.”

8. Madaraka ya baraza lenye kuongoza la karne ya kwanza yalitia nini ndani?

8 Cheo cha uangalizi hicho kilitia ndani daraka la mitume la kuweka rasmi wanaume wanaofaa kwenye vyeo vya utumishi na kupanga huduma kitengenezo. Lakini kilimaanisha zaidi. Kilihusu pia kufundisha na kuelewesha wazi mambo ya mafundisho. Kwa kutimiza ahadi ya Kristo kwenye Yohana 16:13, NW, “roho ya ukweli” ingeongoza kundi la Kikristo hatua kwa hatua ndani ya ukweli wote. Kutoka mwanzo, wale waliolikubali neno kwa moyo na wakawa Wakristo wapakwa-mafuta waliobatizwa waliendelea kujitoa kwa “mafundisho ya mitume.” Kwa kweli, sababu iliyotolewa ya kuweka rasmi wanaume saba waliopendekezwa kwenye kazi iliyohitajiwa kabisa ya kugawanya chakula cha kimwili ilikuwa kwamba “wale kumi na wawili” waweze kubaki huru ‘kujitoa kwa sala na kwa huduma ya lile neno.’—Matendo 2:42; 6:1-6.

9. Ni jinsi gani baraza lenye kuongoza la mapema lilivyopunguzwa kuwa na washirika 11, lakini yaonekana ni kwa nini hesabu haikurudishwa mara hiyo kuwa 12?

9 Yaonekana kwamba kwanza washiriki wa baraza lenye kuongoza walikuwa mitume bila kutia wengine ndani. Lakini lingebaki hivyo? Karibu mwaka 44 W.K., mtume Yakobo, ndugu ya Yohana, aliuawa na Herode Agripa 1. (Matendo 12:1, 2) Kwa wazi hakuna jitihada iliyofanywa kuweka mwingine badala yake awe mtume, kama ilivyofanywa kwa habari ya Yuda. Kwa nini? Bila shaka hiyo ilikuwa kwa sababu Yakobo alikufa akiwa mwaminifu, wa kwanza wa mitume 12 kufa. Kwa upande mwingine, Yuda alikuwa mwasi mwovu na ilikuwa lazima kuweka mwingine mahali pake ili kuwe tena na hesabu 12 ya mawe ya msingi ya Israeli wa kiroho.—Waefeso 2:20; Ufunuo 21:14.

10. Baraza lenye kuongoza la karne ya kwanza lilipanuliwa wakati gani na jinsi gani, na Kristo alilitumiaje kuongoza nyumba ya Mungu?

10 Washiriki wa kwanza wa baraza lenye kuongoza la karne ya kwanza walikuwa mitume, wanaume waliokuwa wametembea pamoja na Yesu na waliokuwa wamekuwa mashahidi wa kifo na ufufuo wake. (Matendo 1:21, 22) Lakini hali hii ingebadilika. Kadiri miaka ilivyopita, wanaume wengine Wakristo walipata kimo cha kiroho wakawekwa kuwa wazee katika kundi la Yerusalemu. Kufikia mwaka 49 W.K. ikiwa si kabla ya hapo, baraza lenye kuongoza lilikuwa limepanuliwa kutia ndani hesabu fulani ya wazee katika Yerusalemu. (Matendo 15:2) Kwa hiyo muundo wa baraza lenye kuongoza haukuongozwa na sheria ngumu zilizokazwa bila badiliko, bali kwa wazi Mungu aliongoza mambo hivi kwamba ulibadilika ili kufaa hali za watu wake. Kristo, Kichwa cha kundi mwenye kutenda, alitumia hili baraza lenye kuongoza lililoongezewa ukubwa liamue mambo yenye maana ya mafundisho kuhusu kutahiriwa na kujitiisha chini ya Sheria ya Musa kwa Wakristo wasio Wayahudi. Baraza lenye kuongoza liliandika barua likieleza uamuzi walo na likatoa amri zishikwe.—Matendo 15:23-29.

Wakati wa Kuhesabu kwa Maneja (Msimamizi) wa Nyumba

11. Je! uongozi imara uliowekwa na baraza lenye kuongoza ulithaminiwa na akina ndugu, na ni nini chaonyesha kwamba Yehova alibariki mpango huu?

11 Wakristo wa mapema wakiwa mmoja mmoja na wakiwa makundi, walithamini mwongozi huu imara uliotolewa na baraza lenye kuongoza. Baada ya kundi katika Antiokia ya Siria kusoma barua iliyotoka kwa baraza lenye kuongoza, walishangilia kitia-moyo hicho, Makundi mengine yalipopokea habari hiyo na yakashika amri hizo, yalizidi kuimarishwa katika imani na kuongezeka katika hesabu siku kwa siku. Kwa wazi, Mungu alibariki mpango huo.—Matendo 15:30, 31.

12, 13. Ni matukio gani ambayo Yesu alitabiri katika mifano yake ya mina (fedha) na talanta?

12 Lakini acheni tuangalie upande mwingine wa jambo hili lenye maana kubwa. Katika kielezi chake cha fedha, Yesu alijifananisha na mwanamume wa uzawa-sharifu (mutu mwenye heshima, ZSB) aliyesafiri kwenda nchi ya mbali akajipatie mamlaka ya kifalme kisha akarudi. (Luka 19:11, 12) Kutokana na kufufuliwa kwake katika 33 W.K., Yesu Kristo alikwezwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu, ambako angeketi mpaka adui zake wawekwe kuwa kibago cha miguu yake.—Matendo 2:33-35.

13 Katika kielezi kinacholingana na hicho, mfano wa talanta, Yesu alitaarifu kwamba baada ya muda mrefu, bwana-mkubwa alikuja kufanya hesabu na watumwa wake. Kwa wale watumwa waliothibitika kuwa waaminifu, bwana-mkubwa alisema hivi: “Ulikuwa mwaminifu juu ya machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” Lakini kwa habari ya yule mtumwa asiye mwaminifu, alijulisha wazi hivi: “Hata kile alicho nacho atanyang’anywa. Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje.”—Mathayo 25:21-23, 29, 30.

14. Yesu alitarajia nini kwa watumwa wake wapakwa-mafuta?

14 Baada ya muda mrefu—karibu karne 19—Kristo alikabidhiwa mamlaka ya kifalme katika 1914, mwishoni mwa “nyakati zilizowekwa za mataifa.” (Luka 21:24, NW) Muda fupi baada ya hapo, ‘alikuja akafanya hesabu’ na watumwa wake, Wakristo waliopakwa mafuta kwa roho. (Mathayo 25:19) Kristo alitarajia nini kutoka kwao wakiwa mmoja mmoja na wakiwa jumla? Mgawo wa mtumishi-nyumbani uliendelea kama ulivyokuwa umekuwa tangu karne ya kwanza. Kristo alikuwa amewapa watu mmoja mmoja talanta—“kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake.” Hivyo, Yesu alitarajia matokeo ya kadiri. (Mathayo 25:15) Yenye kutumika hapa ni kanuni kwenye 1 Wakorintho 4:2, NW, ambayo hutaarifu hivi: “Kinachotazamiwa kwa watumishi-nyumbani ni mwanamume kupatikana mwaminifu.” Kufanyiza talanta kazi kulimaanisha kutenda kwa uaminifu kama “balozi” badala ya Kristo, kufanya wanafunzi na kuwagawia kweli za kiroho.—2 Wakorintho 5:20.

“Mtumwa” na Baraza Lenye Kuongoza Wakati wa Mwisho Ulipokuwa Ukikaribia

15. (a) Kristo alitarajia nini kwa maneja (msimamizi) wa nyumba yake mwenye ujumla wa watu? (b) Ni nini chaonyesha kwamba Kristo alitarajia jamii ya mtumwa iwe ikifanya hivyo kabla hajawasili kukagua nyumba yake?

15 Yesu alitarajia Wakristo wapakwa-mafuta kwa ujumla wawe wakitenda kana mtumishi-nyumbani mwaminifu, wakilipa baraza la watumishi wake “kipimo chao cha magawio ya chakula kwa wakati unaofaa.” (Luka 12:42, NW) Kulingana na Luka 12:43, Kristo alisema: “Mwenye furaha ni mtumwa yule, ikiwa bwana-mkubwa wake wakati wa kuwasili amkuta akifanya hivyo!” Hiyo yaonyesha kwamba kwa wakati fulani kabla ya Kristo kuwasili ili kufanya hesabu na watumwa wake waliopakwa mafuta kwa roho, wangalikuwa wakigawanya chakula cha kiroho kwa washiriki wa kundi la Kikristo, nyumba ya Mungu. Kristo alikuta nani akifanya hivyo aliporudi akiwa na mamlaka ya kifalme katika 1914 na kuanza kukagua nyumba ya Mungu katika 1918?—Malaki 3:1-4; Luka 19:12; 1 Petro 4:17.

16. Kristo alipowasili kukagua nyumba ya Mungu katika 1918, kwa nini hakupata makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yakigawa chakula cha kiroho wakati ufaao?

16 Muda mrefu wa Yesu kungojea akiwa mkono wa kuume wa Yehova ulipokaribia kikomo, kidato kwa kidato ikaonekana wazi ni nani aliyekuwa akitoa chakula cha kiroho kwa watu wa nyumba ya Kristo hata katika wakati uliotangulia 1914. Je! unafikiri yalikuwa ni makanisa ya Jumuiya ya Wakristo? Bila shaka sivyo, kwa kuwa yalikuwa yamejihusisha sana katika siasa. Yalikuwa yamekuwa vyombo vyenye nia ya kutumiwa kupanua ukoloni na walikuwa wamejaribu kila mmoja kushinda mwingine ili kuthibitisha uzalendo wao, hivyo kutia moyo utukuzo wa taifa. Upesi hiyo ikawaletea hatia nzito ya damu, yaani, walipounga mkono kwa bidii serikali za kisiasa zilizohusika katika vita ya ulimwengu ya kwanza. Kiroho, imani yao ilikuwa imedhoofishwa na Umamboleo. Hali hatari ya kiroho ilitokea kwa sababu wengi wa makasisi wao walishawishwa kwa urahisi waamini uchambuzi wa juu na mageuzi. Hakuna chakula cha kiroho chenye kulisha ambacho kingetarajiwa kutoka kwa makasisi wa Jumuiya ya Wakristo!

17. Kwa nini Kristo aliwakataa Wakristo fulani wapakwa-mafuta, na matokeo yakawa nini kwao?

17 Vivyo hivyo, hakuna chakula cha kiroho chenye kulisha ambacho kingetarajiwa kutoka kwa wale Wakristo wapakwa-mafuta waliohangaikia zaidi wokovu wao wa kibinafsi kuliko kufanyiza kazi “talanta” ya Bwana-Mkubwa. Wakawa ‘walegevu,’ wasiofaa kuangalia mali ya Bwana-Mkubwa. Kwa hiyo, walitupwa ndani ya “giza la nje,” ambako makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yangali yamo.—Mathayo 25:24-30.

18. Bwana-mkubwa alipata nani akigawia baraza la watumishi wake chakula cha kiroho wakati ufaao, na jambo gani lathibitisha hivyo?

18 Kwa hiyo, alipowasili kukagua watumwa wake katika 1918, Kristo Yesu, Bwana-Mkubwa, alipata nani akiwapa baraza la watumishi wake kipimo cha magawio ya chakula kwa wakati unaofaa? Basi, kufikia wakati huo, ni nani aliyekuwa amewapa watafutaji ukweli wenye mioyo myeupe uelewevu sahihi juu ya dhabihu ya ukombozi, jina la kimungu, kutoonekana kwa kuwapo kwa Kristo, na umaana wa 1914? Ni nani aliyekuwa amefichua ubandia wa Utatu, kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu, na moto wa mateso? Na ni nani aliyekuwa ameonya juu ya hatari za mageuzi na uwasiliano na roho? Mambo ya hakika huonyesha kwamba kilikuwa kile kikundi cha Wakristo wapakwa-mafuta kilichoshirikiana na gazeti Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence, sasa linaitwa Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova.

19. Jamii ya mtumwa mwaninifu ilikuwa imejidhihirishaje kabla ya 1918, ilikuwa imegawa vyakula vya kiroho kwa njia gani, na tangu wakati gani?

19 Katika toleo la Novemba 1, 1944, Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) ulitaarifu hivi: “Katika 1878, miaka arobaini kabla ya kuja kwa Bwana kwenye hekalu katika 1918, kulikuwako jamii ya Wakristo wenye mioyo myeupe waliojitoa kabisa waliokuwa wamejitenga na matengenezo ya utawala wa kanisa na makasisi na waliotafuta kuzoea Ukristo . . . Mwaka uliofuata, yaani, katika Julai, 1879, ili kweli alizoandaa Mungu kupitia Kristo zikiwa ‘chakula kwa wakati wake’ ziweze kugawanywa kwa ukawaida kwenye nyumba yake yote ya watoto waliojitoa kabisa, gazeti hili, Mnara wa Mlinzi, lilianza kuchapishwa.”

20. (a) Baraza Linaloongoza la ki-siku-hizi lilitokeaje? (b) (b) Washiriki wa Baraza Linaloongoza walikuwa wanafanya nini, na chini ya mwongozo wa nani?

20 Likitoa habari juu ya kusitawi kwa Baraza Linaloongoza la ki-siku-hizi, toleo la Mei 1, 1972, la Mnara wa Mlinzi lilieleza hivi: “Miaka mitano iliyofuata [katika 1884] Zion’s Watch Tower Tract Society ilianzishwa na ikatumikia kuwa ‘chombo’ cha kupatia chakula cha kiroho maelfu ya watu wenye unyofu wa moyo wanaotaka kumjua Mungu na kufahamu Neno lake . . . Wakristo waliojiweka wakfu, kubatizwa na kutiwa mafuta wakaja kushirikiana na Sosaiti hiyo katika makao makuu katika Pennsylvania. Kwamba walikuwa washiriki wa [Baraza la Waelekezi] ama sivyo, walijifanya wenyewe kupatikana kwa kazi ya pekee ya jamii ya ‘mtumwa mwaminifu mwenye [busara].’ Walisaidia katika kulisha na kuongoza jamii ya mtumwa, na hivyo ndivyo baraza [l]enye kuongoza [l]ilivyotokea. Kwa wazi hii ilikuwa chini ya uongozi wa nguvu ya utendaji isiyoonekana au roho takatifu ya Yehova. Tena, chini ya [mwelekezo] wa Kichwa cha kundi la Kikristo, Yesu Kristo.”

21. (a) Kristo alipata nani akigawanya chakula cha kiroho, na aliwathawabishaje? (b) Ni nini kilichongojea mtumwa mwaninifu na Baraza Linaloongoza lake?

21 Katika 1918, Kristo alipokagua wale waliodai kuwa watumwa wake katika 1918, alikuta kikundi cha kimataifa cha Wakristo kikitangaza kweli za Biblia kwa matumizi ndani ya kundi na nje pia katika kazi ya kuhubiri. Katika 1919 ikawa kweli kweli kama alivyokuwa ametabiri Kristo: “Mwenye furaha ni mtumwa yule ikiwa bwana-mkubwa wake wakati wa kuwasili amkuta akifanya hivyo. Kweli kweli mimi nasema kwenu nyinyi, Yeye atamweka juu ya mali zake zote.” (Mathayo 24:46, 47, NW) Hawa Wakristo wa kweli waliingia katika shangwe ya Bwana-Mkubwa wao. Wakiwa wamejionyesha kuwa ‘waaminifu juu ya vitu vichache,’ waliwekwa rasmi na Bwana-Mkubwa wawe ‘juu ya vitu vingi.’ (Mathayo 25:21) Mtumwa mwaminifu na Baraza Linaloongoza lake alikuwa katika mahali pake, tayari kwa mgawo uliopanuliwa. Yatupasa kuterema kama nini kwamba ilikuwa hivyo, kwa maana Wakristo wenye uaminifu-mshikamanifu wananufaika sana na kazi ya ujitoaji ya mtumwa mwaminifu na Baraza Linaloongoza lake!

Mambo Makuu ya Kukumbuka

◻ Ni nani Kichwa cha nyumba ya Mungu, na Huyu amempa nani mamlaka?

◻ Ni mgawo gani ambao Kristo ameipa jamii ya mtumwa kwa ujumla?

◻ Ni baraza gani jingine la ujumla lililokuwa ndani ya jamii ya mtumwa, nalo lilikuwa na wajibu gani hususa?

◻ Kristo alipowasili kukagua watu wa nyumba ya Mungu, nani alikuwa akiandalia washiriki wayo chakula cha kiroho?

◻ Baraza Linaloongoza la ki-siku-hizi lilitokeaje?

[Picha katika ukurasa wa 10]

“Mtumwa” wa karne ya kwanza alikuwa na baraza lenye kuongoza lenye mitume na wazee wa kundi la Yerusalemu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki