Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/15 kur. 21-23
  • Sierra Leone—Kufukua “Almasi” Zayo Zenye Thamani Kabisa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sierra Leone—Kufukua “Almasi” Zayo Zenye Thamani Kabisa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Watafutaji Watendaji wa Ukweli
  • Kuitikia Usaidizi Wenye Saburi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/15 kur. 21-23

Sierra Leone—Kufukua “Almasi” Zayo Zenye Thamani Kabisa

KATIKA mwaka 1462, kikundi cha mabaharia hodari Wareno kilijisukuma kwenye pwani ya Afrika Magharibi kufikia kilometa 890 kaskazini ya ikweta. Wao hawakuogopeshwa na hadithi za mapokeo kwamba kuna bahari yenye giza iliyojaa madubwana yaliyosemekana kuwa kusini ya Morocco. Tena, hawakukubali ile imani yenye kuwako sana kwamba jua liliwaka joto jingi sana karibu na ikweta hivi kwamba bahari kuu ilichemka.

Sawa na vile mabaharia hao walivyotumainia, meli zao za mbao hazikuwaka kwa miali ya ghafula, wala hawakuona madubwana yasiyo na vichwa ya hadithi zile za mapokeo. Badala ya hivyo, walipata fuo nzuri zenye mchanga mweupe, kule mbele yazo kukiwa na milima mirefu ya rangi kolevu ya kijani-kibichi, iliyojaa misitu. Na wakati mvua za kitropiki zilipogharikisha dunia na umeme ukawaka kwa nguvu angani, radi ilinguruma na kututuma katika milima hiyo kwa mngurumo kama wa hayawani mkubwa sana. Kwa kupendeza, mabaharia hao walipaita mahali hapo Sierra Leone—“Milima ya Simba”!

Kadiri miaka ilivyopita, wanadamu walijifunza kwamba utajiri wa Sierra Leone haukuwa uzuri wayo wa mazingira tu. Pia kulikuwako madini: chuma, bokzati, rutili, kromati, platinamu, na dhahabu. Lakini ulipofika 1930 ndipo kukawa na ugunduzi uliofanya ulimwengu wa kibiashara uliangalie kwa makini bara hili dogo sana. Almasi zilipatikana! Ugavi wa johari hizi zenye thamani ukawa mwingi, ukavuta maelfu ya wachimbuzi wa madini.

Watu fulani wameokota kihalisi almasi kutoka usoni pa nchi. Mwanamke mmoja alipata almasi kubwa akiwa anafua nguo zake katika kijito. Mwanamume mmoja alifukua johari ya karati 153 akiwa anapanda viazi vitamu shambani. Hata hivyo, kwa sehemu kubwa, kupata mawe haya ya thamani kubwa kumetaka jitihada kubwa. Kwa kielelezo, almasi fulani huwa zimezikwa kwa kina kirefu katika ardhi, zikiwa zimelala katika kimbaleti, namna fulani ya jiwe. Kuzipata huhusisha kuchimba, kulipusha, kupondaponda, na kuchaguachagua. Pia hutaka ujuzi, maarifa, na saburi.

Ingawa shughuli nyingi za kuchimba almasi huendelea hadi leo hii, utafutaji wa johari za namna tofauti—almasi za thamani kubwa zaidi—umekuwa ukiendelea katika Sierra Leone kuanzia 1915. Katika mwaka huo, mwanamume mmoja jina lake Alfred Joseph aliondoka Barbados akasafiri kwenye bara hili kwa melistima. Hapa akaanza kazi ya “uchimbuzi wa madini,” si wa almasi, bali wa watu wenye kutamani kutumikia Mungu wa kweli “katika roho na kweli.” (Yohana 4:24) Utafutaji huu uliendeshwa katika njia ile ile ulivyoendeshwa na Wakristo wa karne ya kwanza—“peupe na nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20, NW) Miaka saba baadaye, Alfred Joseph aliungwa katika kazi hii na William R. Brown, pia kutoka West Indies.

Kufikia mwisho wa 1923, kundi dogo lilikuwa limeanzishwa katika mji mkuu, Freetown. Kundi hilo lilitia ndani watu 14 waliobatizwa majuzi. Leo, watu mmoja mmoja 632 katika makundi 30 hushiriki kwa utendaji katika kazi ya kuhubiri wakiwa Mashahidi wa Yehova. Jitihada zao za kutafuta na kuchimbua zile ambazo zingeweza kuitwa almasi za kiroho zenye thamani kubwa za Sierra Leone zaendelea kupata mafanikio makubwa.

Watafutaji Watendaji wa Ukweli

Wanafunzi fulani wapya wa Yesu Kristo wamethibitika kuwa kama almasi yenye kuokotwa kwa urahisi kutoka kwenye uso wa nchi. Wao wamekuwa watendaji kwa kuwatafuta Mashahidi wa Yehova. Mmoja wao alikuwa mpambanywele jina lake Joan. Yeye alipigia simu makao makuu ya kwao ya Mashahidi katika Freetown na kuomba funzo la Biblia.

Ni nini kilichoharakisha Joan kupiga simu hiyo? “Mimi siwezi kukumbuka hata wakati mmoja maishani mwangu ambapo sikuwa nikitafuta Mungu,” yeye asema. “Kuanzia utoto wangu, nimejiunga na makanisa na vikundi vingi vya kidini lakini sikuweza kamwe kupata uradhi wa kiroho.

“Karibu miaka kumi iliyopita, nilipata kujua kuna Mashahidi, lakini bila sababu yoyote, nikafanyiza rai ya kwamba watu hawa walipasa kuepukwa kwa vyovyote. Wakati rafiki wa jamaa alipokuja kuwa Shahidi, nilifanya andikisho la magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Nilifanya hivyo kumfurahisha tu; sikujisumbua kamwe kuyasoma. Kwa uhakika, niliyatumia kusafisha madirisha yangu! Ndipo ikaja Amkeni! moja iliyoshika uangalifu wangu. Makala ya jalada ilihusu uhitaji wetu wa upendo. [Septemba 22, 1986, kwa Kiingereza] Niliisoma nikavutiwa kwa kina kirefu. Gazeti hilo ndilo lililonisukuma kuomba funzo la Biblia.” Joan alifanya maendeleo ya haraka sana na upesi akawa Shahidi aliyebatizwa wa Yehova.

Mtu mwingine aliyetafuta ukweli alikuwa mwanamume kijana jina lake Manso. Yeye alitaka kuwa padri na alienda kwenye seminari. Lakini alipoona unafiki wa walimu wake, alivunjika moyo na kuacha kabisa. Halafu, Manso akaanza kuhudhuria mikutano mingine ya kidini. Siku moja akiwa njiani kuzuru mjomba, aliona kitabu chenye kutangazwa na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi—Is the Bible Really the Word of God? Kilikuwa chini katika kifungu cha maji yenye matope. Kwa kuwa kichwa kilimpendeza Manso, alikitoa kitabu humo, akakikausha, na kukisoma. Huu ndio ulikuwa aliokuwa amekuwa akitafuta! Kitabu hicho kiliwatia moyo wasomaji kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme la kwao. Kwa hiyo Manso akaenda, akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi, na upesi akabatizwa. Sasa yeye atumikia akiwa mwevanjeli painia wa wakati wote!

Kuitikia Usaidizi Wenye Saburi

Hata hivyo, wanafunzi wengine wapya wamethibitika kuwa zaidi kama almasi zilizofungiwa kwa kina kirefu katika jiwe. Jitihada halisi imehitajiwa ‘kuzifukua.’ Donald, mzee Mkristo, akumbuka saburi iliyohitajiwa kusaidia mwanamke mmoja jina lake Martha. Yeye ataarifu hivi: “Ingawa mwanamke huyo alikubali kujifunza, sikuzote alitungojesha muda mrefu kabla ya kuanza. Nyakati fulani aliweka kimakusudi akiba ya kazi ambao zingaliweza kufanywa mapema kidogo. Halafu akatuomba tungoje mpaka azifanye. Nyakati fulani tulingoja kwa zaidi ya saa moja. Mwanamke huyo alitumainia sisi tungevunjika moyo na kwenda zetu, lakini kila juma tulijaribu kumaliza habari chache zenye umaana. Tokeo? Baada ya muda uthamini wake ulikua.

“Ugumu mwingine ulikuwa kumfanya Martha aende kwenye mikutano. Mimi nilikuwa nikileta Mashahidi wengine kwenye funzo lake la Biblia ili ahisi akistareheka wakati angekuja kwenye Jumba la Ufalme. Lakini yeye alikawia na akakawia sana hivi kwamba mwishowe alipokuja, alikuwa ni kama ajua kundi zima!” Saburi ikaleta matokeo. Martha sasa amebatizwa na ana msimamo mzuri katika kundi.

Hapo kwanza Pius alikinza ukweli. Kufikia wakati ambapo mume na mke wamisionari walianza funzo la Biblia pamoja naye, Pius alikuwa katika miaka yake ya 70, alikuwa mshiriki thabiti wa chama cha kisiasa, na alikuwa mwekahazina wa kanisa lake. “Alitoa ubishi mkali juu ya kila jambo tulilozungumzia,” wakasema wamisionari. “Kila juma alianza akiwa mtulivu, lakini kidato kwa kidato akawaka. Lilikuwa pigano halisi kila juma, na mara nyingi tulihisi tukitaka kukubali ushinde kwa kutamauka na kumwachilia. Jambo kubwa lililotufanya tuzidi kwenda ni kwamba sikuzote yeye alitayarisha somo kikamili.

“Baada ya karibu mwaka mmoja wa kufanya hivyo, Pius alitangaza kwamba alikuwa ameamua kufanya uchunguzi wa kujitegemea mwenyewe. Kwa kuwa alikuwa mwalimu aliyestaafu, alijua kufanya utafiti. Kila siku kwa majuma mawili, aliupanda mlima wa kwenda kwenye maktaba ya chuo kikuu, ambako alisoma sana vitabu vyenye kuieleza Biblia na vitabu vya marejezo. Baadaye alitangaza hivi: ‘Sasa mimi nasadikishwa kwamba kila jambo ambalo nyinyi mmekuwa mkiniambia ni la kweli. Mungu si Utatu, hakuna moto wa mateso, na nafsi haifi. Hata watu fulani katika kanisa langu hukiri kwamba ndivyo ilivyo.’ Baada ya hapo, Pius alifanya maendeleo ya haraka, akajiuzulu siasa na kanisa pia. Baada ya kubatizwa, alitumikia akiwa painia msaidizi, akitumia saa 60 kwa mwezi katika kazi ya kuhubiri, mara nyingi kwa kadiri ambavyo angeweza mpaka kifo chake katika 1987.

“Jambo moja ambalo hatukujua kwa muda mrefu,” wakumbuka wamisionari waliofundisha Pius, “ni kwamba mama yake alikuwa amekuwa akishiriki na Mashahidi wa Yehova. Yeye [Pius] alikumbuka kuwa alihudhuria mikutano na mama yake alipokuwa mchanga. Lakini baada ya mama huyo kufa, Pius alifuata njia yake mwenyewe. Baada ya ubatizo wake, Pius alisema hivi: ‘Majuto yangu ya pekee ni kwamba mama hawezi kuniona sasa.’ Halafu uso wake ukang’aa, naye akaongezea hivi: ‘Lakini ataniona katika ulimwengu mpya!’ “

Hadi leo hii, utafutaji wa almasi na utafutaji wa wanafunzi waendelea. Matangazo ya kuvutia husifusifu kwamba “almasi ni za milele.” Hata hivyo, mwenye kuwa na johari hiyo ya kupendeza sana hapati kuionea shangwe milele kwa sababu bila uandalizi wa Mungu wa wokovu, kifo ndilo fungu la wanadamu wote wenye dhambi. (Yohana 3:16, 17) Hivyo kazi ya Mashahidi wa Yehova katika Sierra Leone inatokeza hazina iliyo ya thamani kubwa kuliko almasi za kawaida tu: watumishi wa Mungu na wanafunzi wa Yesu Kristo! Na Neno la Yehova huahidi hivi: “Yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.”—1 Yohana 2:17.

[Ramani/Picha katika ukurasa wa 22, 23]

(Ona chapisho ili kupata maandishi yaliyopangwa kikamili)

[Picha]

Katikati ya mandhari kama hii, wapiga mbiu ya Ufalme hupata almasi za kiroho katika Sierra Leone

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki