Tukio Ambalo Wewe Hupaswi Kukosa
“Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.” Maneno hayo ya Bwana wetu, Yesu Kristo, yanayopatikana kwenye Luka 22:19, yalinenwa wakati alipoanzisha ukumbusho wa kifo chake. Kifo cha Yesu ndicho kilichofungulia wanadamu taraja la kupata uhai wa milele katika hali za kiparadiso. Kwa hiyo, kifo chake ni jambo ambalo ni lazima sisi tukumbuke.
Je! wewe utaadhimisha ukumbusho wa kifo hicho mwaka huu?
Tafadhali kubali mwaliko huu kutoka kwa Mashahidi wa Yehova ili ujiunge nao katika kukumbuka tukio hili la maana. Mwadhimisho huu utakuwa baada ya mshuko wa jua katika tarehe inayolingana na Nisani 14 katika kalenda-mwezi ya Biblia. Tia alama tarehe hiyo katika kalenda yako ili usisahau. Ni Aprili 10, 1990. Mashahidi wa Yehova wa kwenu waweza kukuambia mahali na wakati barabara ambapo tukio hili litaadhimishwa katika jumuiya yenu.