Je! Wewe Ni Sanamu ya Kujiabudu Mwenyewe?
Bila kung’amua hivyo, binadamu fulani hujifanya wenyewe kuwa sanamu. Biblia hueleza kwenye Waefeso 5:5, NW: “Kwa kuwa mwajua hili, mkilitambua nyinyi wenyewe, kwamba hakuna mwasherati au mtu asiye safi au mtu mwenye pupa—ambalo lamaanisha kuwa mwabudu sanamu—aliye na urithi wowote katika ufalme wa Kristo na wa Mungu.” (Wakolosai 3:5; linganisha Wagalatia 5:19-21.) Tamaa za kimnofu zaweza kuja katikati ya mtu na Mungu. Paulo asema juu ya hao kwamba “mungu wao ni tumbo.” (Wafilipi 3:18, 19) Kwa maneno mengine, wana “mungu” mwingine kando na Yehova, wakiweka kwanza tamaa zao za kimnofu. Mwenendo kama huo unaweza kumwondoa mtu katika Ufalme wa Mungu. (1 Wakorintho 6:9, 10) Basi, kuna sababu nzuri ya kutii maneno ya mtume Paulo: “Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.”—1 Wakorintho 10:14.