‘Shauri Katika Kitabu Lilisaidia’
Ndivyo kijana mmoja kutoka Maryland, U.S.A., aandika kwa habari ya kile kitabu Questions Young People Ask—Answers That Work. “Mimi nilikisoma kitabu chote kwa siku mbili,” asema, “nami sikuweza kuacha kuwaambia watu juu yacho.
“Nilipata kwamba sura ya 6, ‘Kwa Nini ni Vigumu Sana Kupatana na Ndugu na Dada Yangu?,’ ilinisaidia kwa sababu nyakati nyingine mimi huhisi kidogo nikimwonea wivu dada yangu mkubwa. Lakini niling’amua kwa haraka kwa kusoma kwamba hainipasi kuhisi wivu kwa sababu yeye ana haki fulani ambazo sikuwa nazo. Ilipoelekea twakaribia kubishana, nilitumia shauri katika kitabu hicho. Lilisaidia! Sasa uhusiano wenye nguvu zaidi unajengeka kati ya dada yangu nami.”
Kukua katika nyakati hizi zenye taabu si rahisi. Vijana wanaelekeana na hali nyingi mpya na lazima wafanye maamuzi mazito. Je! Yanipasa kunywa vileo? Kukubali dawa za kulevya? Ni mwenendo gani wafaa pamoja na mtu wa ile jinsia tofauti? Vijana wanahitaji majibu yanayosaidia. Twahisi kwamba wewe pamoja na watoto wako mtanufaishwa sana na kichapo hiki chenye picha za kuvutia, cha kurasa 320. Pokeeni nakala moja kwa kujaza na kutupelekea hati hii. Ni Kshs. 20/= (Tshs. 150/=; RWF 100)
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu cha kurasa 320, chenye jalada gumu Questions Young People Ask—Answers That Work. Mimi nawapelekea Kshs. 20/= (Tshs. 150/=; RWF 100).