Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 5/1 uku. 3
  • Wakati Kifo Kichukuapo Mpendwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati Kifo Kichukuapo Mpendwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Hakika kwa Wafu
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
  • Unawezaje Kukabiliana na Magumu ya Kuwa na Wazazi Walezi?
    Amkeni!—2003
  • Wapendwa Wako Waliokufa—Je! Utawaona Tena?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Inakuwaje kwa Wapendwa Wetu Waliokufa?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 5/1 uku. 3

Wakati Kifo Kichukuapo Mpendwa

“KATIKA 1981 mama yangu aliuawa na kansa. Alikuwa mama yangu mlezi. Kifo chake kilitugonga sana mimi na ndugu yangu wa malezi. Nilikuwa na miaka 17, na ndugu yangu alikuwa na miaka 11. Mama aliniachia ukiwa mwingi. Mimi nililelewa nikiwa Mkatoliki, na kwa sababu nilikuwa nimefundishwa kwamba yuko mbinguni, nilitaka kujiua ili nikawe pamoja naye. Ndiye aliyekuwa rafiki yangu mkubwa zaidi.”—Roberta, mwenye miaka 25.

Je! imepata kuwa hivyo kwako? Ikiwa ndivyo, umejijulia mwenyewe umivu ambalo huandamana na kupoteza mpendwa. Yaonekana si haki kamwe kifo kiwe na nguvu za kuchukua mtu upendaye. Na itukiapo hivyo, wazo la kutoweza tena kuongea, kucheka, au kumshika mpendwa wako laweza kuwa gumu sana kuhimili. Na kama vile maneno ya Roberta yaonyeshavyo, umivu hilo halifutwi kwa kuambiwa kwamba mpendwa wako yuko juu mbinguni.

Ingawa hivyo, wewe ungehisije kama ungejua kwamba yawezekana kuungana upya karibuni pamoja na mpendwa wako aliyekufa, si juu mbinguni, hapana, bali papa hapa duniani chini ya hali zenye amani na uadilifu? Namna gani kama ungejifunza pia kwamba wakati huo wanadamu watakuwa na tazamio la kuona shangwe ya afya kamilifu na kwamba hawatalazimika kamwe kufa? Huenda ukasema, ‘Hiyo ni tamaa ya kuwazia-wazia mambo tu!’

Hata hivyo, huko nyuma katika karne ya kwanza W.K., Yesu Kristo alitaarifu kijasiri hivi: “Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi.” (Yohana 11:25) Hiyo ilikuwa ahadi ya kwamba wafu wataishi tena—tazamio la kusisimua kweli kweli!

Ingawa hivyo, labda unashangaa hivi: ‘Je! kuna msingi timamu wa kuamini ahadi hiyo? Nawezaje kuwa na uhakika kwamba huko si kuwazia-wazia mambo tu? Na ikiwa kuna msingi wa kuamini hivyo, huenda utimizo wa ahadi hii ukamaanisha nini kwangu na kwa wapendwa wangu?’ Makala inayofuata itazungumzia maswali haya na mengine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki