Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 6/15 uku. 31
  • “Baadaye Akampa Mume Wake Kiasi Fulani Pia”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Baadaye Akampa Mume Wake Kiasi Fulani Pia”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 6/15 uku. 31

“Baadaye Akampa Mume Wake Kiasi Fulani Pia”

JE! ADAMU alikuwapo nyoka alipoongea na Hawa na kumdanganya aasi dhidi ya Mungu? Biblia haionyeshi hivyo. Mwanzo 3:6, NW, huripoti kwamba Hawa “alianza kuchukua baadhi ya tunda lao na kulila. Baadaye akampa mume wake kiasi fulani pia alipokuwa pamoja naye.” Hata hivyo, tafsiri fulani za Biblia hutoa maoni tofauti. King James Version hufasiri andiko hilo kama ifuatavyo: “Alichukua baadhi ya tunda la huo, na akala, na akampa pia mume wake akiwa pamoja na yeye; na yeye akala.”

Kitenzi cha Kiebrania kilichotafsiriwa “akampa” kimo katika wakati usiokamilika na chashirikishwa na namna maalumu ya kiunganishi “na” [Kiebrania, waw], hivyo kikionyesha mfuatano wa wakati baada ya wakati au kwa hatua hatua. Kwa hiyo, New World Translation hutafsiri mitokeo kadhaa ya neno waw, ambalo lakamatanisha mfuatano wa matukio kwenye Mwanzo 3:6, si pamoja na “na” tu bali pia pamoja na maneno mengine ya kuunganisha, kama vile “basi,” “kwa hiyo,” na “baadaye.” Hivyo New World Translation ina msingi imara kwa fasiri iliyo juu.

Je! Adamu angalikaa-kaa tu kama asiyejali maongezi kati ya mke wake na nyoka, huku akiusikiliza uwongo na uchongezi wa yule mwasi asiyeonekana aliyemwongoza nyoka? Kwa kupendeza, mwanachuo Mjeremani wa Biblia, J. P. Lange akataa wazo hilo na kueleza hivi: “Ni jambo gumu kuwazia kwamba mwanamume alikuwapo, hata kwamba alikaa kimya, wakati wa kile kitendo cha kushawishwa.” Na katika kueleza yale maneno “akiwa pamoja na yeye,” mwelezaji Myahudi B. Jacob ataja kwamba “[hayamaanishi] aliyekuwa amesimama pamoja naye (wakati wa kitendo kilichotangulia wala wakati mwanamke alipokuwa akila).”

Maongezi ya Hawa pamoja na nyoka yalifunua kwamba mume wake alikuwa amempasha habari juu ya amri ya Mungu kutokula kutokana na ule mti. (Mwanzo 3:3) Kwa hiyo akiwa kichwa cha Hawa, Adamu alikuwa ametimiza daraka hilo. Ibilisi alipuuza mpango wa Mungu wa ukichwa na kwa werevu akatumia kwa faida uhakika wa kwamba Hawa alikuwa peke yake. Baadaye mwanamke huyo alijibu hivi: “Nyoka alinidanganya, nikala.” (Mwanzo 3:13) Hawa alidanganywa kwa sababu aliamini uwongo, lakini hiyo haikutetea mkiuko wake. Kielelezo hiki chenye onyo chaeleza kwamba hatuwezi kamwe kuwa na udhuru wa kufanya kosa fulani katika macho ya Yehova.—1 Timotheo 2:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki