Kwa Sababu Alisali
KWENYE 1 Wathesalonike 5:17, 18, mtume Paulo alisema hivi: “Ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” Hata hivyo, je! nyakati fulani wewe hujikuta bila nia ya kushukuru unapoonea shangwe mlo fulani katika mahali pa watu wote, kama vile mkahawa? Kwa sababu ya tahadharisho la Yesu dhidi ya sala ya kujionyesha, yaeleweka kwamba mtu angetaka kuepuka kuvuta uangalifu wa kupita kiasi kwake mwenyewe. (Mathayo 6:5, 6) Hata hivyo, huenda sala yenye kutolewa kwa busara ikawa na uvutio wa kufanya mtu aangaliwe kwa njia yenye kupendeleka.
Hayo yalikuwa maono ya mhudumu mchanga mmoja anayetumikia kwenye Betheli ya Brooklyn, makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova. Alikuwa akila kiamsha-kinywa kwenye mkahawa mmoja, akipanga kwenda kwenye kundi la kwao akakutane na kikundi ambacho kingeshiriki katika utendaji wa kuhubiri Ufalme. Kiamsha-kinywa chake kilipoletwa, alitoa sala kwa njia yake ya kawaida. Alipofungua macho, aliinua kichwa akakuta mgonjezi wa kike amesimama hapo akimkodolea macho.
“Wewe unasali, sivyo?” mwanamke huyo akauliza. Alipojibu ndivyo, mwanamke huyo akasema: “Ni lazima wewe uwe u mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wazazi wangu ni wamoja pia. Mimi sikuhusika kamwe katika dini yao, lakini najua kwamba napaswa kufanya hivyo. Labda napaswa kupata andikisho kwa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Je! naweza kuyapata kutoka kwako?”
“Karibu chakula changu kininyonge,” akumbuka huyo ndugu mchanga. Hata hivyo, aliweza kuangushia mwanamke huyo maandikisho mawili na magazeti mawili ya karibuni zaidi na kupanga ziara ya kurudia—yote hayo kwa sababu alisali.