Kitabu Hiki Kilibadili Maisha Zao
Miaka iliyopita mwanamke mmoja alipata talaka kutoka kwa mume wake. Mwishowe Steve mwana wake akawa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Steve alijaribu kuongea na mama yake juu ya imani zake bila mafanikio. Pia alienda kuona baba yake, aliyekuwa anakufa kwa kansa.
Badala ya kuongea sana, Steve aliacha tu kile kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani kando ya kitanda cha baba yake na akasema kwamba kukisoma kungemsaidia. Baba yake alisoma kitabu hicho na akaanza yeye mwenyewe kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova katika Januari 1988.
Kwa sasa, kwenye vikusanyiko vya jamaa mama ya Steve alikuwa na nafasi za kutazama utu mpya wenye kuonyeshwa na aliyekuwa mume wake. Hiyo ilimvutia sana mama huyu hata akakubali kuhudhuria mkutano mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Alianza kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, na upesi akawa akiketi kwenye mikutano hiyo pamoja na mume wake wa zamani. Mwishowe walifunga ndoa tena.
Baba ya Steve alikufa katika Septemba 1988 lakini si kabla hajaanza kushiriki katika huduma ya Kikristo. Mama ya Steve, aliyetunza baba yake wakati wa miezi ya mwisho ya ugonjwa wake, alibatizwa katika Juni 1988 na sasa ni Shahidi mwenye bidii.
Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani ni kitabu kinachotoa tumaini kwa kuelekeza kwenye majibu ya Biblia kwa matatizo ya maisha. Kimekuwa chombo chenye kubadili maisha nyingi. Pokea nakala kwa kujaza na kupeleka hati yenye anwani inayoandama.
Mimi ningependa kupokea kile kitabu cha kurasa 256 chenye jalada gumu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.