Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 4/1 kur. 3-4
  • Wakati Ulikuwa Umeenda Sana Kuliko Walivyofikiri!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati Ulikuwa Umeenda Sana Kuliko Walivyofikiri!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Yeremia Nabii wa Hukumu za Mungu Asiyependwa na Wengi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kitabu Cha Biblia Namba 26—Yeremia
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yeremia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • “Siwezi Kunyamaza Kimya”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 4/1 kur. 3-4

Wakati Ulikuwa Umeenda Sana Kuliko Walivyofikiri!

MWAKA, 609 K.W.K. Mahali, Yerusalemu. Msemaji, Yeremia nabii. Yeye alitabiri uharibifu kwa ajili ya jiji lake takatifu lililopendwa, Yerusalemu, uharibifu ambao ungekuja kwa sababu Wayahudi walikuwa wamegeuzia Yehova kisogo chao na wakajitumbukiza katika ibada ya miungu bandia. Walijitia katika ibada ya ngono za upujufu katika mahali-mahali pa juu, wakatoa matoleo ya kinywaji kwa miungu ya kipagani, wakaabudu jua na mwezi na nyota, wakachoma ubani kwa Baali, na kudhabihu watoto wao kwa Moleki.—1 Wafalme 14:23, 24; Yeremia 6:15; 7:31; 8:2; 32:29, 34, 35; Ezekieli 8:7-17.

Machoni pao Yeremia alikuwa mpiga yowe la maafa, mshupavu, mnung’unikaji dhidi ya kila kitu na kila mtu. Kwa miaka 38 Yeremia alikuwa amekuwa akiwaonya; kwa miaka 38 wakaaji wa Yerusalemu walikuwa wamekuwa wakimdhihaki. Kufikia wakati huo, watu walikuwa wamekuwa wakipuuza Yehova, wakisema yeye hakuwa nguvu ya kuhangaikiwa. Walisema hivi: “BWANA [Yehova, NW] hatatenda mema, wala hatatenda mabaya” na, “BWANA [Yehova, NW] ameiacha nchi hii, naye BWANA [Yehova, NW] haoni.”—Sefania 1:12; Ezekieli 9:9.

Manabii Yeremia na Ezekieli walikuwa wamekuwa wakihubiri uharibifu wa Yerusalemu, lakini hakuna kilichokuwa kimetendeka. Hivyo basi Waisraeli waliondolea mbali wazo la kwamba njozi hiyo ingetimizwa katika siku yao, wakisema hivi: “Siku hizo zinakawia na maono yote hayatimizwi.” Lakini Yehova alijibu hivi: “Siku hizo ni karibu . . . Maana mimi ni BWANA [Yehova, NW]; mimi nitanena, na neno lile nitakalolinena litatimizwa; wala halitakawilishwa tena; maana katika siku zenu, Ewe nyumba iliyoasi, nitalinena neno hilo na kulitimiza.”—Ezekieli 12:22-25.

Katika 609 K.W.K. wakati ulikuwa umefika wa Yehova kutimiza neno lake. Baada ya Yeremia kuwa akivumisha lile onyo kwa karibu makumi manne ya miaka, jiji la Yerusalemu lilizingirwa na majeshi ya Kibabuloni. Miezi kumi na minane baadaye kuta zilipenywa, hekalu likachomwa, na watu walio wengi wakapelekwa uhamishoni Babuloni. Kama ilivyotabiriwa, jiji liliharibiwa kwa upanga na njaa kuu na ugonjwa wa kipuku.—2 Wafalme 25:7-17; 2 Nyakati 36:17-20; Yeremia 32:36; 52:12-20.

Yeremia alisema kweli. Watu hao walikosea. Wakati ulikuwa umeenda sana kuliko walivyofikiri! Njozi haikuwa kwa ajili ya miaka ya mbali. Ilikuwa kwa ajili ya siku yao.

Hii si historia tu. Lililotendeka kwa Yerusalemu lilikuwa la kiunabii. Lilitangulia kuwa kivuli cha jambo fulani lenye kuja. Jumuiya ya Wakristo ya kisasa huchukua jina la Kristo na kudai kuwa katika uhusiano wa agano pamoja na Mungu; hata hivyo yeye hutembea katika nyayo za wakaaji wa Yerusalemu la zamani. Sana-sana, makanisa ya Jumuiya ya Wakristo hufundisha mafundisho ya kipagani, yamechafuliwa na ukosefu wa adili katika ngono, hutetea mipango ya kisiasa, huunga mkono vita vya ulimwengu, hukubali kwa moyo fundisho la mageuzi ya binadamu na kumweka kando Mungu aliye Muumba, huangalia tu bila kujali kutolewa kwa mamilioni ya watoto ambao hawajazaliwa ili wawe dhabihu juu ya madhabahu ya kujifaidi kwa watu binafsi, na kwa ujumla huchagua kufuata falsafa za kibinadamu, wakidai kwamba Biblia ni hekaya tu na hadithi ya mapokeo.

Kama vile watu wa Yerusalemu walivyodhihaki Yeremia, ndivyo Jumuiya ya Wakristo hudhihaki Mashahidi wa Yehova leo. Onyo la Mashahidi juu ya uharibifu unaokuja kwenye Har–Magedoni hupuuzwa kuwa lisilofaa kitu. ‘Mungu hapendezwi na dunia,’ yasema Jumuiya ya Wakristo. ‘Acheni yeye aendeshe mambo ya mbinguni; sisi ndio tutaendesha mambo ya dunia. Na ikiwa Har–Magedoni itakuja, haitakuwa katika kizazi chetu. Sisi tumewahi kusikia hadithi hiyo hapo kwanza. Sisi hatutadanganyika!’

Je! jambo hili litakuwa ni mrudio wa historia? Je! utakuwa ni wakati mwingine ambapo mamilioni watagundua kwamba wakati ulikuwa umeenda sana kuliko walivyofikiri?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki