Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 9/15 kur. 24-27
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Mavuno Katika Brazili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Mavuno Katika Brazili
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Mapainia Washiriki Katika Mavuno
  • Uvutano wa Makasisi Waathiri Mavuno
  • Jitihada za Kuendelezwa Zilileta Mibaraka
  • Maisha Zageuzwa
  • Shiriki Kikamili Katika Mavuno
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 9/15 kur. 24-27

Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Mavuno Katika Brazili

“INUENI macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele.” (Yohana 4:35, 36) Maneno hayo ya kiunabii ya Yesu Kristo ni ya kweli leo katika mifiko ya mbali ya ile nchi kubwa ya Amerika Kusini ya Brazili.

Kwa miaka kadhaa Mashahidi wa Yehova katika Brazili wamekuwa wakionea shangwe maongezeko mazuri. Katika Aprili 1991, kilele cha wavunaji wa Ufalme 308,973 waliongoza mafunzo ya Biblia nyumbani 401,574. Siku ya Machi 30, 1991, jumla ya watu 897,739 walikusanyika kukumbuka kifo cha Yesu, yule aliyeanzisha kazi ya kuvuna.

Japo matokeo mazuri hayo, sehemu ya shamba ingali yangoja kuvunwa. Watu zaidi ya milioni tano huishi katika maeneo ya Brazili ambako kazi ya kuhubiri iendeshwayo na Mashahidi wa Yehova ni kidogo tu au hakuna yoyote. Ni jambo gani linalofanywa kupanua mavuno yafikie maeneo hayo?

Mapainia Washiriki Katika Mavuno

Wakati wa kipindi kimoja cha hivi majuzi cha miezi sita, ofisi ya tawi ya Watch Tower Society katika Brazili ilituma wapiga mbiu ya Ufalme wa wakati wote—mapainia wa pekee wa muda 100 na mapainia wa kawaida 97—kwenye miji 97, sana-sana katika sehemu ya mashariki ya nchi iliyo na wakaaji wengi sana. Wahubiri wa Ufalme kutoka makundi mbalimbali walijitolea pia kufanya kazi katika maeneo hayo kwa vipindi vifupi zaidi. Japo vipingamizi ambavyo ilikuwa lazima vishindwe, matokeo yamekuwa ya kuridhisha.

Kwa kielelezo, katika São João da Ponte, katika mkoa wa Minas Gerais, mapainia walimzuru mwalimu wa dini wa shule ya mahali hapo. Baada ya kuusikia ujumbe, aliagiza nakala 50 za kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako kwa ajili ya darasa lake la katekisimu. Mwalimu mwingine aliwaambia hivi mapainia wenye kuondoka: “Hampaswi kuwa mkiondoka, kwa kuwa mnafanya kazi nzuri sana hapa. Nyinyi peke yenu ndio mwezao kutoa uelezo wa wazi juu ya Biblia.”

Si kila mtu aliyefurahishwa na kazi nzuri hiyo. Mathalani, fikiria barua moja iliyochapishwa katika gazeti la mahali hapo (Diário de Montes Claros) chini ya kichwa kikuu cha ukurasa wa mbele “Padri Ashtakiwa Uchochezi wa Jeuri na Ubaguzi.” Barua hiyo ilisema: “Kanisani, [padri huyo] ana desturi ya kushutumu vikali watu wafuatao madhehebu na dini nyinginezo, hata ingawa makasisi wa hapo hawaandalii waumini mwongozo wa kutosha wa Kikatoliki na wa Kikristo juu ya Gospeli. Katika Misa, yeye ameshambulia wahudumu wa Mashahidi wa Yehova walio mjini, ingawa wao hawawatendi Wakatoliki vibaya.” Bila kuonyesha chuki hiyo, mwandikaji wa makala hiyo alihudhuria hotuba ya Biblia iliyotolewa na mapainia akiandamana na watu wengine wenye kupendezwa. Wote waliuonea shangwe mkutano huo.

Ndugu wanne kutoka Fortaleza walisafiri kwa ndege hadi Kisiwa cha Fernando de Noronha, kilometa 400 kutoka bara. Wakaaji 1,500 wa kisiwa hicho hawakuwa wamepokea ushahidi mzuri kwa muda wa zaidi ya miaka 15. Katika muda wa siku kumi akina ndugu waliangusha vitabu 50 na magazeti na broshua 245, na wakaanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani 15. Watu kumi na wawili walihudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo, uliotukia wakati wa ziara yao. Mapainia hao watumaini kwamba kwa msaada wa Yehova kazi itaanzishwa huko kwa uthabiti. Ndugu fulani wamefikiria kuhamia kisiwa hicho.

Uvutano wa Makasisi Waathiri Mavuno

Kikundi kimoja cha wahubiri wa Ufalme wa Kundi la Arpoador katika Rio de Janeiro kilijitolea kutumia majuma mawili kikihubiri katika miji kadhaa katika mkoa wa Minas Gerais, umbali wa kilometa karibu 200. Walipata upendezo kuwakuta watu wa huko wakiwa wakaribishaji-wageni na wafadhili sana. Wanaume walikuwa na desturi ya kuinua kofia zao kila wakati Mungu au jina lake, Yehova, lilipotajwa. Hata hivyo, kwa sababu ya kicho chao kwa Mungu walivutwa kwa urahisi na makasisi.

Katika mji mmoja padri alishauri watu wasisikilize Mashahidi wa Yehova wala kuhudhuria mkutano waliokuwa wakipanga kufanya. Pia aliratibu awe na Misa maalumu wakati ule ule wa mkutano, na Misa hiyo ilitangazwa kwa sauti kubwa kabisa kwenye kipaaza-sauti kilicho nje ya kanisa lake. Hata hivyo, japo jitihada zake, wakaaji 29 wa hapo walihudhuria mkutano huo, kuongezea wale wageni wenye kuzuru.

Mji jirani mmoja ulikuwa tofauti kabisa. Huko padri aliwaambia watu wasikilize Mashahidi wazurupo. Tokeo likawa kwamba 168 walihudhuria mkutano wa kwanza. Baadaye, yeye aliwaambia watoe uangalifu kwa jinsi Mashahidi wa Yehova huadhimisha Ukumbusho kwa sababu, kama alivyosema, “wao huufanya ipasavyo.” Wakati wa majuma mawili ya kazi ya kuhubiri Ufalme katika eneo hilo, vitabu 1,014 na magazeti na broshua 1,052 viliangushwa.

Jitihada za Kuendelezwa Zilileta Mibaraka

Mwezi mmoja baadaye wahubiri 34 wa Ufalme walirudi kuongoza mafunzo ya Biblia yaliyoanzishwa wakati wa ziara ya kwanza. Mzee Mkristo mwenye kuongoza aliandika hivi: “Ilisisimua kuona watu wenye kupendezwa wakitukaribisha kwa shukrani na wakiwa na machozi ya shangwe machoni pao.” Dada mmoja akumbuka kwamba mwanamke mmoja alimjia yeye na Mashahidi wengine katika mkahawa wa chakula cha mchana “akisihi, huku machozi yakiwa machoni mwake, ili sisi tuje tujifunze naye.” Bibi mwingine alijifunza mara tatu katika juma ambalo Mashahidi walikuwapo. Kila mara, alikuwa ametayarisha somo lake akingojea funzo. Bibi huyo alisema kwamba alikuwa ameanza kusali kwa Mungu wa kweli, Yehova. “Kitu hiki ndicho nimekuwa nikingojea moyoni mwangu,” akaongezea.

Baadaye, mapainia wawili waligawiwa kutunza upendezi katika eneo hilo. Kama vile katika karne ya kwanza W.K., “wale waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele [waliokuwa na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai wa milele, NW] wakaamini.” (Matendo 13:48) Na kama vile mwanamke Msamaria ambaye Yesu alitolea ushahidi kwenye kisima cha Yakobo, wao walianza kuambia wengine waliyojifunza. (Yohana 4:5-30) Leo mapainia hao 2 wana wengine 6 wakitumikia pamoja nao, na wastani wa watu 20 huhudhuria mikutano ya kila juma.

Wakiwa na idili juu ya mafanikio ya kazi hiyo maalumu, wahubiri 29 wa Kundi la Arpoador walienda kuhubiri katika mji wa Mutum, umbali wa kilometa karibu 500. “Upokezi ulikuwa wa kutokeza kweli kweli,” akasema mzee mwenye kuelekeza kikundi hicho. “Watu walio wengi walisikiliza kwa usikivu na upendezi sana hivi kwamba mafunzo ya Biblia 170 yalianzwa, nasi twahisi kwamba mengi yayo yataendelea.” Katika majuma mawili wahubiri hao walihubiri wastani wa saa 90 kila mmoja na kuwaangushia watu vipande karibu 1,100 vya fasihi. Kilele cha 181 walihudhuria hotuba za watu wote zilizotolewa na akina ndugu.

Miezi michache baadaye, kundi lilikodi nyumba nzuri katika kitovu cha Mutum ili itumiwe kama Jumba la Ufalme na kao la mapainia. Ripoti ya kwanza ambayo Sosaiti ilipelekewa na dada mapainia wawili waliogawiwa huko ilisomeka hivi kwa sehemu: “Kukiwa na mafunzo mengi sana yaliyoanzwa tayari, twahitaji mapainia wengi zaidi. Hata kwa msaada wa akina ndugu we-nye kutoka Rio de Janeiro mara moja kwa mwezi, kazi ni kubwa mno. Tisa kati ya wenye nyumba kumi waliosemwa nao watuomba turudi. Pia twahitaji msaada kuongoza mikutano.” Painia mwingine sasa amejiunga nao.

Maisha Zageuzwa

Limekuwa jambo la kutia moyo sana kuona kweli ikitia mizizi na kuzaa tunda zuri. Mtu mmoja mwenye kupendezwa aliandika hivi: “Kupata maarifa hayo ya Biblia ndilo jambo bora zaidi ambalo limeweza kunipata wakati wowote. Maisha yangu yamebadilika yakawa bora, nami sihitaji kutumia tena dawa za kunituliza. . . . Yehova na awathawabishe kwa kila jambo ambalo mmenifanyia.”

Mtu mwingine alitaarifu hivi: “Mimi nastaajabia kikweli jinsi Yehova amefungua macho yangu. Ingawa nilifiwa na nyanya yangu juma hili, sasa nina tumaini la kumwona tena. Natumaini kubatizwa, lakini nataka kutayarishwa vizuri kwanza. Yehova na awabariki kwa kuja hapa kutuonyesha ile njia nyembamba iongozayo kwenye uhai wa milele.” Bado mtu mwingine alisema hivi: “Nataka nyinyi mjue kwamba niliacha kuvuta sigareti mwezi mmoja uliopita. Nafurahia sana gazeti mlilonipelekea. Lilikuwa na mambo mema mengi kwa kuwa lilinisaidia kuacha kufanya hivyo. Kwa uhakika, mavuno yatoa sababu nzuri ya kushangilia.

Hata hivyo, mibaraka ya jinsi hiyo haikuja bila jitihada. Kwa kielelezo, wakati bibi mmoja na binti yake walipoanza kujifunza, padri wa hapo aliwaonya kwamba wakienda kwenye mikutano ya Mashahidi, yeye angewaondosha kanisani. Wakipuuza tisho hilo, walienda mikutanoni. Ndipo wakaepukwa kabisa na marafiki wa zamani, baadhi yao wakiwalaumu kuwa wameingiwa na kichaa kwa sababu “Yehova huyo” haonekani katika Biblia ya Kikatoliki. Kwa kuwa bibi huyo hakuweza kupata jina Yehova katika Biblia yake ya Kikatoliki, aliwaalika majirani wamzuru katika siku ya kujifunza kwake na mapainia. Mwanamke mmoja alikuja na fasiri yake ya Biblia ya Paulina ya Kikatoliki. Aliposoma jina la Mungu katika maelezo ya chini kuhusu Kutoka 6:3, alikubali funzo la Biblia katika nyumba yake.

Shiriki Kikamili Katika Mavuno

Kutumikia katika eneo lenye kufanyiwa kazi mara chache sana kulikuwa na tokeo gani juu ya wafanya kazi wenyewe? Mhubiri mmoja wa Ufalme alisema hivi: “Utendaji huu ulitumika kuimarisha imani yetu na uhusiano wetu na Yehova na kutusaidia tuchunguze upya mambo tupaswayo kuyapa umaana wa kwanza.” Mhubiri mwingine alitaarifu hivi: “Kipindi hicho cha siku 14 kiliongeza upendo wangu kwa ndugu zangu, ambao hutumika wakiwa familia moja yenye lengo moja: kutafuta-tafuta wasikivu wengi zaidi. Hiyo ilinifanya niwapende zaidi wale wakubalio ujumbe wetu, mara nyingi wakiwa na machozi machoni mwao, wakionyesha kiu halisi ya kuitaka kweli. Na zaidi ya yote, nilihisi upendo wa Yehova katika kutupa sisi pendeleo la kumtumikia.”

Mzee mmoja aliyeshiriki kuhubiri katika eneo lenye kufanyiwa kazi mara chache sana alionyesha tofauti iliyopo kati ya maisha huko na katika majiji makubwa. Alisema hivi: “Mimi naona tu kwamba maisha ya ndugu wengi yangeweza kutajirishwa kwa kuhamia eneo la ndani-ndani mashambani. Huku ni kama hakuna jeuri kabisa. Maisha katika miji midogo na ya ukubwa wa kadiri ni ya namna yenye kuturuhusu si kuishi tu kwa mapato madogo zaidi bali pia kufanya ushirika zaidi pamoja na ndugu zetu na kutoa wakati mwingi zaidi kwenye utendaji wa kiroho. Je! ndugu zaidi waliostaafu, vijana wenye madaraka kidogo ya familia, au ndugu ambao kazi yao huwaruhusu wahame wangeweza kulipokea kwa moyo pendeleo hili lisilo na kifani na kuleta shangwe kwao wenyewe, kwa Yehova, na kwa jirani zao?”

Ripoti hii juu ya eneo lenye kufanyiwa kazi mara chache sana katika Brazili yathibitisha kwamba mashamba ni meupe tayari kwa mavuno. Katika muda wa miaka miwili tu, kazi katika shamba hilo imetokeza makundi mapya na vikundi vilivyo peke yavyo 191. Mengi yabaki kufanywa, lakini hakika Yehova ataendelea kutoa baraka yake kwa kadiri wahubiri zaidi wa Ufalme washirikivyo katika mavuno haya yenye matunda. Je! wewe waweza kuwa na ushiriki mkubwa zaidi ndani yayo?

[Ramani/Picha katika ukurasa wa 25]

Mashahidi wenye furaha kutoka Rio de Janeiro washiriki katika mavuno

[Ramani]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

BRAZILI

[Picha katika ukurasa wa 26]

Ushahidi wa mashambani katika Minas Gerais

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki