“Kiliniamsha”
Ndivyo alivyosema mwanamke mmoja kutoka Washington State, U.S.A., kuhusu kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Alieleza hivi:
“Kwa miaka minne mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuja mlangoni pangu kwa kawaida na kuniachia magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!. Alinitia moyo nijifunze. Mwishowe akanishawishi nisome kitabu Creation, hilo tu. Akanitia moyo nisali, hilo tu. Kitabu hicho kiliondoa shaka zote, na sala iliniletea msaada kutoka kwa Yehova. . . .
“Najua sasa kwamba Mungu kwa kweli yuko. Nalijua jina lake, Yehova. Najua yeye husikiliza sala. Najua kwa sababu gani mambo yako jinsi yalivyo. Mimi nina amani, na amani yangu hukua kila juma ninapojifunza zaidi.”
Kitabu hicho, pamoja na maelezo yacho sahihi juu ya ulimwengu wote mzima na mambo yote madogo madogo yanayowezesha uhai uweko duniani yatakusisimua. Waweza kupokea nakala kwa kujaza na kupeleka hati-anwani hii yenye kuandama.
Ningependa kupokea kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?
[Picha katika ukurasa wa 32]
Wanamageuzi hutaarifu hivi: “Hakuhitaji kufikiri kwingi ili kuwazia unyoya kuwa gamba [la mnyama mtambaazi] lililogeuzwa kidogo.” Mambo ya hakika huonyesha tofauti
Mshale
Meno
Vijino
Vijijino