Unaalikwa kwa Moyo Mweupe
Kifo cha mwanamume Yesu Kristo zaidi ya miaka 1,900 iliyopita kilikuwa tukio la maana zaidi katika historia. Kilifungulia sisi sote matazamio ya kufikia uhai wa milele katika hali za Paradiso. Wakati wa sherehe sahili moja, Yesu alitumia divai na mkate usiotiwa chachu kuwa mifano ya dhabihu yake ya kibinadamu yenye upendo. Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19, NW) Je! wewe utakumbuka?
Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge pamoja nao katika kufanya mwadhimisho huo wa Ukumbusho. Utakuwa baada ya jua kushuka katika tarehe inayolingana na Nisani 14 kwenye kalenda-mwezi ya Biblia. Unaweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu zaidi nawe. Tafuta kujua kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu kuhusu mahali na wakati barabara. Tarehe ya mwadhimisho katika 1992 itakuwa Ijumaa, Aprili 17.