Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 8/15 uku. 31
  • Hatua ya Kurudi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hatua ya Kurudi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 8/15 uku. 31

Hatua ya Kurudi

‘ALISEMA nao kwa kutumia mifano.’ Ndivyo Biblia hutoa utangulizi wa mifano mitatu ya Yesu yenye kukumbukwa inayohusu rehema—yule kondoo mmoja aliyepotea, ile sarafu ya drakma iliyopotea, na yule mwana mpotevu.—Luka 15:3-32.

Makala mbili katika Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, zilichanganua mifano hiyo na zikasaidia wasomaji waone jinsi rehema yaweza kunyooshwa leo. Wachungaji wa kiroho ndio walioelekezewa hasa katika kuchukua hatua ya kwanza ili kukutana na watu waliotengwa na ushirika lakini ambao huenda wakaitikia ziara zenye fadhili. Matokeo ya makala hizo na ya taratibu hiyo mpya yamekuwa nini?

Upesi baada ya gazeti hilo kutangazwa kwa chapa, mwanamume mmoja katika jimbo la Washington, U.S.A., aliandika hivi: “Uthibitisho wa upendo mwingi wa Yehova wenye fadhili uliwasili katika barua nilizopokea leo. Ninaketi hapa nikiwa na machozi machoni pangu na shangwe moyoni mwangu juu ya maandalizi na marekebisho yaliyoandaliwa na Aliye Juu Zaidi. Ni Mungu aliye na haki kwelikweli tu awezaye kuandaa msaada kwa ajili ya wale wenye mfano wa kondoo ambao wamepotea. . . . Naam, nimetengwa na ushirika lakini nimo njiani kurudishwa.” Katika Oktoba alirudishwa.

Namna gani zile ziara zinazofanywa na wazee wawili wa kundi? Mke Mkristo aliandika hivi: “Maneno hayawezi kuonyesha jinsi ninavyohisi. Mume wangu ametengwa na ushirika kwa miaka 13 hivi. Wazee walimtembelea, kama ilivyodokezwa na makala hiyo. Usiku uliopita kwa mara ya kwanza katika miaka mingi, alikwenda kwenye mmojawapo wa mikutano. Anajaribu sasa kugeuza maisha yake na kurudi.”

Waangalizi wasafirio wanapozuru kundi baada ya kundi, wao huona matokeo. Mwangalizi mmoja asafiriye aliandika hivi:

“Wakati Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991 lilipotangazwa kwa chapa, wengi walitaka kujua itikio lingekuwa nini kwa wazee kukutana na waliotengwa na ushirika. Jibu limekuwa la wazi sana.

“Katika mzunguko wetu, makundi manne ya mwisho ambayo nimezuru yameona kurudi kwa watu tisa kwenye Majumba ya Ufalme. Ingawa ni mmoja tu ambaye amerudishwa, wale wengine wanane wanafanya maendeleo mazuri. Wazee na makundi wanasisimuka kuona matunda ya kazi yao ngumu na hekima ya kutumia maelekezo ya kitheokrasi.

“Twashangilia katika mpango huu mzuri, wenye rehema. Kama alivyosema dada mmoja aliyerudishwa, ‘Sikuwa na ujasiri wa kurudi peke yangu, kwa kuwa nilihisi nimehukumiwa na Yehova. Lakini wazee waliponitembelea, hicho kilikuwa kitia-moyo nilichohitaji ili kurudi.’ Uchangamfu wake umetia kundi moyo sana.”

Hata ingawa wengi wanaotembelewa hawaitikii, kwa hakika mazuri yanatimizwa kwa hatua hiyo ya kwanza yenye rehema. Hivyo, kuanzia Septemba wazee katika kila kundi watapitia majina ya wale waliomo katika maeneo yao ambao wametengwa na ushirika nao watapanga kuwatembelea wote ambao wao wanahisi waweza kuitikia rehema inayotolewa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki