Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 10/15 uku. 3
  • Familia Yashambuliwa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Familia Yashambuliwa!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kuona Njia ya Kupata Furaha ya Jamaa
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Je, Kuna Siri ya Kupata Furaha ya Familia?
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Familia—Binadamu Wanaihitaji!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Taabu ya Familia —Ishara ya Nyakati
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 10/15 uku. 3

Familia Yashambuliwa!

“FAMILIA ndicho chama cha kibinadamu ambacho ni cha kale sana kuliko vyote. Ndicho cha maana kuliko vyote katika njia nyingi. Ndio msingi wa jamii ya watu. Mambo yote ya ustaarabu yameendelea au yakatoweka, yakitegemea nguvu au udhaifu wa maisha ya familia.”

Ndivyo ilivyosema The World Book Encyclopedia nyuma katika 1973. Hata hivyo, maneno hayo yanapochunguzwa kulingana na maoni ya leo, yanasikika kuwa yenye kutisha, karibu kuwa yenye kuonyesha wakati ujao mbaya. Miaka michache iliyopita imeshuhudia lile lililo sawa na shambulio la moja kwa moja dhidi ya maisha ya familia. Mshauri mashuhuri John Bradshaw aandika hivi: “Kuna tatizo katika familia leo. . . . Kiwango cha juu cha talaka, ghasia za matineja, utumizi mwingi mbaya wa dawa za kulevya, ngono ya kiukoo yenye kuenea sana, magonjwa yanayosababishwa na ulaji mbaya na kupigwa kihalisi ni uthibitisho wa kwamba kuna kasoro fulani kubwa.”

Kwa kweli, “uthibitisho wa kwamba kuna kasoro fulani kubwa” katika familia waweza kupatikana kotekote ulimwenguni. The Unesco Courier lilisema hivi kuhusu hali katika Ulaya: “Tangu 1965, kumekuwako ongezeko kubwa katika idadi ya talaka kotekote katika kontinenti hiyo. . . . Kumekuwako ongezeko katika idadi ya familia zenye mzazi mmoja.” Nchi zinazositawi vilevile zinaona ongezeko la taabu ya familia. Mwandikaji Hélène Tremblay aonelea hivi: “Kwa mamilioni wanaoishi katika jamii ambazo zimepata kuzoelea kwa karne kadhaa njia ya maisha ya kawaida, inayoweza kuamuliwa kimbele, isiyobadilika, leo ni wakati wa msukosuko.”

Jambo lenye kutisha zaidi ni mazingira yaliyomo katika makao mengi leo. Katika United States pekee, mamilioni kwa mamilioni ya watoto hulelewa na mzazi aliye mzoevu wa vileo. Kumekuwako pia ongezeko lenye kuchukiza katika jeuri ya familia. Katika kitabu chao Intimate Violence, watafiti Richard Gelles na Murray Straus huripoti hivi: “Waelekea zaidi kushambuliwa kimwili, kupigwa, na kuuawa na mpendwa katika nyumba yako mwenyewe kuliko kwingineko kote, au na mwingine yeyote katika jamii yetu.”

Ikiwa kuendelea kwa ustaarabu kwa kweli hutegemea nguvu ya familia, kuna sababu ya kuhangaikia wakati ujao wa ustaarabu. Hata hivyo, wakati ujao wa ustaarabu huenda usiwe jambo unalohangaikia sana. Yaelekea zaidi kwamba hangaiko lako ni juu ya lile ambalo msukosuko huo waweza kumaanisha kwa familia yako. Matokeo yatakuwa nini? Jibu kutoka chanzo chenye mamlaka huenda likakushangaza sana.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki