Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fl sura 1 kur. 4-10
  • Kuona Njia ya Kupata Furaha ya Jamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuona Njia ya Kupata Furaha ya Jamaa
  • Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • HISTORIA YATEGEMEZA MYANGO WA JAMAA
  • KUPENDEZWA KWA MUNGU NA MPANGO WA JAMAA
  • MAULIZO TUNAYOPASWA KUYAELEKEA
  • Je, Kuna Siri ya Kupata Furaha ya Familia?
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kujenga Pamoja Kijamaa kwa Ajili ya Wakati Ujao wa Milele
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Familia—Binadamu Wanaihitaji!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Ufunguo wa Maisha ya Jamaa Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
fl sura 1 kur. 4-10

Sura 1

Kuona Njia ya Kupata Furaha ya Jamaa

1, 2. Ni mambo gani mema ambayo maisha bora ya jamaa yanaweza kutoa? Kwa hiyo ni maulizo gani, yanayoweza kuulizwa?

MAMBO mengi ambayo wanadamu wanahitaji yanaweza kutimizwa katika mpango wa jamaa. Humo ndimo tunamoweza kupata mambo ambayo kwa kawaida sote tunayatamani sana: kuona kwamba unahitajiwa, unaonwa kuwa bora, unapendwa. Hali ya jamaa iliyo changamfu yaweza kutimiza mambo hayo yote katika njia ya ajabu. Yaweza kufanyiza hali ya kutumainiana, kufahamiana na kuhurumiana. Ndipo nyumba inapogeuka kuwa mahali pa kupumzika na taabu na msukosuko unaotoka nje. Watoto wanaweza kujiona wako salama na nyutu zao zaweza kusitawi sana.

2 Hayo ndiyo maisha ya jamaa ambayo tungetaka tuone yakifurahiwa. Lakini hayajileti yenyewe. Yanaweza kupatika.na namna gani? Ni kwa sababu gani leo maisha ya jamaa ni yenye taabu sana hivyo katika sehemu nyingi za ulimwengu? Ni njia gani inayoweza kuondoa huzuni katika ndoa na kuleta furaha, kuondoa jamaa isiyochangamka na yenye kutengana na kuleta jamaa yenye kuchangamka na iliyoungana?

3. Ushuhuda wa historia unafunua nini juu ya ubora wa jamaa?

3 Ikiwa unapendezwa sana na hali njema na kufanikiwa kwa jamaa yako, una sababu nzuri ya kufanya hivyo. Kikieleza namna mpango wa jamaa ulivyo wa maana sana, kitabu kinachoitwa The World Book Encyclopedia (1973) kinasema hivi:

“Jamaa ndicho chama cha kibinadamu ambacho ni cha kale sana kuliko vyote. Ndicho cha maana kuliko vyote katika njia nyingi. Ndio msingi wa jamii ya watu. Mambo yote ya ustaarabu yameendelea an yakatoweka, yakitegemea nguvu au udhaifu wa maisha ya jamaa.”

4, 5. Ni maoni gani yasiyofaa ambayo umeona katika jamaa nyingi?

4 Lakini ni jamaa ngapi leo ambazo zimeunganishwa sana na vifungo vyenye nguvu vya upendo? Ni jamaa ngapi zinazofurahia uchangamshi unaoletwa na kuonyeshana fadhili (wema), shukrani na ukarimu: Ni jamaa ngapi ambazo zimejifunza kweli ya usemi huu, “kuna furaha nyingi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea”?

5 Leo roho iliyo tofauti sana inaenea katika dunia yote. Ijapokuwa inaonekana sana katika nchi za Magharibi, inaingia vilevile katika nchi za Mashariki na mahali pengine ambapo kwa asili maisha ya jamaa yamekuwa imara sana. Mambo yanayotiwa ndani ya maoni yaliyopo sana ni haya: “Fanya unalotaka, acha wengine wafanye wanayotaka.” Adabu ni mtindo wa kale; acha watoto wachague njia yao wenyewe. ‘Usiamue mema wala mabaya.’ Katika nchi nyingi talaka, makosa ya vijana na uovu wa watu wazima yanaongezeka kwa kadiri ya kuogopesha sana. Watu wenye elimu ya mawazo, waganga wa magonjwa ya akili, makasisi (mapadri) na washauri wengine wanatoa shauri. Lakini mahali pa kutia nguvu umoja wa jamaa, washauri wengi wanaruhusu au hata wanapendekeza kufanya uasherati kuwa njia ya kuondolea kizuizi. Mavuno mabaya yanayotokana na yote kayo yanaonyesha ukweli wa usemi huu: “Chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.”

HISTORIA YATEGEMEZA MYANGO WA JAMAA

6. Yaliyotukia katika Ugiriki wa kale na Rumi yanaonyeshaje ubora wa jamaa?

6 Mambo yanayofundishwa na historia juu ya ubora wa jamaa, yanafaa kuangaliwa sana. Katika Sehemu ya Pili ya kitabu The Story of Civilization, Will Durant mwandikaji wa historia anaeleza habari ya kuvunjika kwa jamaa katika Ugiriki wa kale, kisha anaendelea kusema hivi: “Sababu kubwa iliyofanya Warumi washinde Wagiriki ilikuwa kuvunjika kwa ustaarabu wa Wagiriki kutoka ndani.” Ndipo anapoendelea kuonyesha kwamba nguvu ya Rumi ilikuwa jamaa, lakini mpango wa jamaa ulipovunjika kwa sababu ya uasherati, milki hiyo iliharibika.

7. Sababu gani watu fulani katika Milki ya Kirumi walifurahia maisha bora ya jamaa wakati wengine walipokuwa wakipata magumu makubwa?

7 Bila shaka, historia inategemeza ukweli wa usemi huu wa kale, “Kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” Lakini inaonyesha vilevile kwamba kuna chanzo kisicho cha hekima ya kibinadamu kinachoweza kutegemewa ili tupate uongozi, pamoja na matokeo ya kufanikiwa kwa mpango wa jamaa. Waandikaji wa historia wanasema kwamba, ijapokuwa Milki ya Kirumi iliharibika, “maisha ya jamaa ya Wayahudi yalikuwa mfano bora, na jamii ndogo za Wakristo zilikuwa zikiwasumbua wapagani wenye kupenda sana anasa kwa utawa na tabia zao njema.” (The Story of Civilization, Sehemu ya Tatu, uku. 366) Ni nini kilichozifanya jamaa hizo kuwa tofauti? Zilikuwa na chanzo cha uongozi kilicho tofauti, yaani, Biblia. Kwa kadiri walivyofuata shauri la Neno la Mungu, ndivyo walivyopata jamaa bora na zenye amani. Matokeo hayo yaliwafanya Warumi wenye tabia mbaya wajione kuwa wenye hatia.

8. Wakati wa kumaliza magumu, sababu gani tuisikilize Biblia?

8 Maneno yaliyotajwa katika mafungu yaliyotangulia yanatokana na Biblia vilevile. Katika kitabu hicho tunapata maneno ya Yesu Kristo yanayoonyesha kwamba kuna furaha nyingi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea, maneno ya mtume Paulo aliyeongozwa na Mungu kwamba tutavuna tunachopanda, na maneno ya Yeremia, nabii wa Mungu kwamba si juu ya mwanadamu kuelekeza hatua zake. (Matendo 20:35, NW; Wagalatia 6:7; Yeremia 10:23) Kanuni hizo za Biblia zimeonekana kuwa za kweli. Vilevile Yesu alisema hivi: “Hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake.” (Mathayo 11:19) Ikiwa shauri la Biblia linasaidia sana kumaliza magumu ya jamaa, je haifai tuisikilize kwa heshima?

9, 10. (a) Sababu gani mashauri yenye msaada na upendano wa asili hayatoshi kumwezesha mtu afurahie maisha ya jamaa yenye furaha? (b) Ni nini zaidi linalotakiwa? (Ufunuo 4:11)

9 Leo, kuna maelfu ya vitabu vinavyotoa habari za ndoa na za maisha ya jamaa. Vitabu vingi kati ya hivyo vina habari fulani inayoweza kusaidia kidogo. Hata hivyo maisha ya jamaa yanaendelea kuharibika. Jambo jingine linahitajiwa, jambo litakalotoa nguvu ya kuzuia mikazo inayoelekea sasa kuharibu mpango wa jamaa. Upendano wa asili kati ya mume na mke na kati ya wazazi na watoto unatoa nguvu. Lakini hata huo unaonekana kuwa hautoshi kuweza kuunganisha jamaa nyingi nyakati za hatari zinapofika. Ni nini zaidi linalotakiwa?

10 Linalotakiwa si uaminifu tu wa kutimiza daraka na kujitoa upate kutimiza mahitaji (lazima) ya mwenzi wa ndoa au ya watoto au ya wazazi. Pamoja na hilo, kuna uhitaji (lazima) wa kuonyesha uaminifu ulio mkubwa hata zaidi kwa Yeye ambaye Biblia inataja kuwa “Baba, ambaye kila jamaa mbinguni na duniani inaitwa kwa jina lake.” Huyo ndiye Mwanzishi wa ndoa na maisha ya jamaa, yaani, Yehova Mungu Muumba wa wanadamu.—Waefeso 3:14, 15, NW.

KUPENDEZWA KWA MUNGU NA MPANGO WA JAMAA

11-13. Kusudi la Mungu juu ya dunia na jamaa ya kibinadamu ni nini?

11 Yehova Mungu anajua mambo ambayo wanadamu wanataka naye anataka tuwe wenye furaha, kwa hiyo anatupa shauri juu ya maisha ya jamaa. Lakini kusudi lililo kubwa kuliko hilo linaonyeshwa kwa kupendezwa sana na jamaa. Biblia inaeleza kusudi hilo. Inaonyesha kwamba dunia hii haikutokea pasipo kusudi. Sisi hatukutokea pasipo kusudi. Yehova Mungu aliiumba dunia hii, akakusudia kwamba ingekuwapo milele na kwamba ingekaliwa na watu milele. Nabii Isaya aliandika hivi: “Ndiye aliyeifanya imara: hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu.”—Isaya 45 :18.

12 Ili atimize kusudi kilo, Mungu aliumba watu wawili wa kwanza akawaambia wawe na jamaa: “Mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi.” (Mwanzo 1:27, 28) Tena kusudi lake liliwataka pamoja na watoto wao wamtii na kuitunza dunia. Mwanzo 2:15 unasema hivi: “[Yehova] Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.” Mwishowe hali hizo zilizo kama bustani zingepanuliwa zienee dunia nzima. Kuitunza dunia na kutumia mali zake kungeipa jamaa ya wanadamu yenye kuenea duniani pote nafasi zisizo na mwisho za kujifunza na kufurahia kutumia uwezo wao.

13 Sasa duniani kuna watu zaidi ya 4,000,000,000, lakini watu hao wengi namna hiyo hawatimizi kusudi la Yehova la kuiumba dunia. Wingi wao hawamtii, wala hawaitunzi dunia. Badala yake, wanaiharibu, wakichafua hewa yake, maji na udongo. Kupatana na kusudi la Mungu la kwanza, yeye hakutabiri tu kwamba angezuia yote hayo, bali vilevile kwamba ‘angewaharibu hao waiharibuo nchi.’—Ufunuo 11:18.

MAULIZO TUNAYOPASWA KUYAELEKEA

14. Sababu gani tunaweza kuwa na hakika kwamba kusudi la Mungu juu ya maisha ya jamaa halitakosa kutimizwa?

14 Kusudi la Mungu juu ya dunia na maisha ya jamaa halitakosa kutimizwa. “Neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu,” anatangaza. (Isaya 55:11) Mungu alianzisha mpango wa jamaa, akatoa shauri linaloonyesha unavyopaswa kutenda. Maongozi yake yanajibu maulizo ya maana sana juu ya maisha ya jamaa— huenda mengine kati ya hayo yakakupasa wewe.

15-17. (a) Ni baadhi ya maulizo gani juu ya rnaishaya jamaa unayoona kuwa ya maana sana? (b) Sababu gani inafaa kupata majibu yenye kufurahisha kwa maulizo hayo?

15 Kwa mfano: Mtu anawezaje kumwona mwenzi wa ndoa anayemfaa? Mapatano yanawezaje kufikiwa katika ndoa juu ya mambo yenye kuleta matata? Bora akili za watu wawili kuliko za mtu mmoja. Lakini, baada ya kushauriana, ni nani kati ya hao wawili anayeamua? Mume anaweza kufanya nini ili aheshimiwe na mke wake, na kwa sababu gani hilo ni jambo la maana kwake? Kwa sababu gani mke anahitaji apendwe na mume, naye anaweza kufanya nini ili apendwe?

16 Unawaonaje watoto? Wengine wanawaona kama mfano wa cheo, msaada wa kazi ngumu au bima (amana) ya wakati wa uzee; wengine wanawaona kuwa mzigo. Lakini Biblia inawataja kuwa baraka. Ni nini linaloonyesha kama watakuwa hivyo ama hawatakuwa hivyo? Wamepaswa kuanza kufundishwa wakati gani? Je! kuweko kutiwa adabu? Ikiwa ndivyo, ya kadiri gani na ya namna gani? Je! kuwe kutopashana habari jamaa kati ya wazazi na watoto? Je! hali hiyo yaweza kutengenezwa? Zaidi ya hayo, je! yaweza, kuzuiwa isipate kutokea wakati wo wote?

17 Kupata majibu yenye kufurahisha kwa maulizo hayo kutasaidia sana kuleta furaha katika maisha ya jamaa yako. Zaidi ya hayo, kunaweza kukupa uhakika wa kwamba kuna Mmoja aliye na nguvu nyingi kuliko wote, mwenye fadhili na hekima unayeweza kuendea wakati wo wote utakapo, na anayeweza kuongoza jamaa yako kwenye furaha isiyo na mwisho.

(Zaburi 119:100-105)

[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 4]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki