Sura ya 14
Kujenga Pamoja Kijamaa kwa Ajili ya Wakati Ujao wa Milele
1. Sababu gani inafaa kufikiria wakati ujao katika kusitawisha furaha ya jamaa?
WAKATI unazidi kuendelea. Huenda wakati wa zamani ukawa na mambo mengi tunayotamani sana kukumbuka, lakini hatuwezi kuishi katika wakati wa zamani. Tunaweza kujifunza kutokana na wakati wa zamani, kutia na makosa ya zamani, lakini tunaweza kuishi katika wakati wa sasa tu. Na bado, hata ijapokuwa huenda jamaa inaendelea vizuri wakati huu, ni lazima kusema kweli kwamba wakati wa sasa ni wa muda tu; leo ni leo, upesi inakuwa kesho, na wakati wa sasa unageuka upesi kuwa wakati wa zamani. Basi, ni jambo la maana kwetu kuendelea kuutazamia wakati ujao ili jamaa iwe na furaha, tujitayarishe kwa ajili yake, tukiupangia mipango. Namna wakati huo utakavyokuwa kwetu na kwa wale walio karibu sana na sisi, itategemea sana maamuzi tunayofanya sasa.
2. (a) Sababu gani watu wengi hawataki kuufikiria wakati ujao? (b) Ikiwa tunataka wakati ujao wenye furaha, imetupasa tumsikilize nani?
2 Hayo ni matazamio gani? Mara nyingi wanadamu wengi wanaufikiria wakati ujao kuwa muda wa miaka michache tu. Wengi wanapendelea kutotazamia wakati ujao ulio mbali sana kwa sababu wanaloweza kutazamia ni mwisho usio mzuri tu, ukileta kuvunjika kwa mpango wa jamaa katika mauti. Kwa wengi, vipindi vyao vya furaha vinafunikwa upesi na masumbufu ya maisha. Lakini kwa kumsikiliza Yeye “ambaye kila jamaa mbinguni na duniani inaitwa kwa jina lake,” maisha yanaweza kuwa na maana sana.—Waefeso 3:14, 15, NW.
3. (a) Ni matazamio gani ambayo Mungu aliwekea watu wa kwanza? (b) Kwa nini mambo yaligeuka yakawa, vingine?
3 Watu wawili wa kwanza walipoumbwa, Mungu hakuwakusudia wao wala watoto wao ambao wangezaliwa wakati ujao waishi miaka michache tu yenye taabu kisha wafe. Aliwapa makao ya paradiso na kuwawekea tumaini la uzima usio na mwisho. (Mwanzo 2: 7-9, 15-17) Lakini walijipotezea wenyewe tumaini hilo, wakapotezea na watoto wao, kwa kuvunja kwa makusudi sheria ya Mungu, Yeye ambaye maisha yao yalimtegemea. Biblia inaeleza hayo katika njia hii: “Kwa mtu mmoja [Adamu] dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.”—Warumi 5:12.
4. Ni mpango gani ambao Yehova Mungu amefanya i1i kusudi lake la kwanza juu ya wanadamu litimizwe?
4 Lakini, kwa upendo Mungu alifanya mpango wa kuikomboa jamaa ya wanadamu. Mwanawe Mwenyewe, Yesu Kristo, alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kwa ajili ya watoto wote wa Adamu. (1 Timotheo 2:5, 6) Kwa njia hiyo Yesu alinunua tena au alikomboa kile ambacho Adamu alikuwa ametupotezea, na njia ikafunguliwa kwa ajili ya wale ambao wangeuamini mpango huo, wapate nafasi ile ile ya uzima ambao Mungu alikuwa ameweka mbele ya watu wawili wa kwanza. Ikiwa hapatwi mapema na ugonjwa mzito au msiba usiotazamiwa, leo, mtu anaweza kuishi miaka 70 au 80, na wachache wanaishi Zaidi kidogo ya miaka hiyo. “Bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.”—Warumi 6:23.
5-7. (a) Tukifanya mapenzi ya Mungu sasa, tunaweza kutazamia nini wakati ujao? (b) Ni ulizo gani unaloweza kuuliza juu ya kusaidia jamaa yako?
5 Hayo yanaweza kuwa na maana gani kwa jamaa yako? Kwa watu wanaozisikiliza na kuzitii amri za Mungu yanaweza kumaanisha wakati ujao wa milele. (Yohana 3:36) Katika Neno lake lisiloweza kukosa kutimizwa, Mungu anaahidi kwamba ataiondoa taratibu ya sasa ya mambo yenye kuonea, na kuagiza mambo yote ya wanadamu yasimamiwe na serikali kamilifu na ya haki ambayo yeye mwenyewe atatoa. (Danieli 2:44) Likionyesha hayo, Neno lake linatuambia kwamba yeye amekusudia “kuvikusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni na vitu vilivyomo duniani.” (Waefeso 1:10, NW) Ndiyo, ndipo kutakapokuwapo upatano katika ulimwengu wote, nayo jamaa ya wanadamu itaunganishwa duniani pote, kusiwe ugomvi wa mataifa, mgawanyiko wa kisiasa, uvunjaji wa sheria unaofanywa bila huruma na ujeuri wa vita. Jamaa zitakaa salama, “wala hapana mtu atakayewatia hofu.” (Zaburi 37:29, 34; Mika 4:3, 4) Jambo hilo litakuwa hivyo kwa sababu wote wale watakaokuwa wakiishi wakati huo watakuwa watu ambao ‘wamemfuata Mungu, kama watoto wanaopendwa,’ nao ‘watazidi kuenenda katika upendo.’—Waefeso 5:1, 2.
6 Chini ya usimamizi wa utawala wa Ufalme wa Mungu, ndipo jamaa ya wanadamu itakapofanya kazi kwa umoja katika tumaini la furaha la kuileta dunia katika hali ya paradiso ambayo Muumba alikusudia, yaani, makao ya bustani yenye kuwapatia wanadamu wote wingi wa chakula. Ndege wote wa dunia wa namna nyingi mno, samaki na wanyama, watakuwa chini ya utawala wa fadhili wa wanadamu na kuwafurahisha, maana hilo ndilo kusudi alilolisema Mungu. (Mwanzo 2:9; 1:26-28) Magonjwa, maumivu, matokeo ya uzee yenye kupunguza nguvu, wala kuogopa mauti (kifo), hakutaizuia tena jamaa ya wanadamu isifurahie maisha. Hata wale “waliomo makaburini” watarudi waje washiriki nafasi za ajabu ambako maisha yatatea wakati huo.—Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:1-5.
7 Unaweza kufanya nini ili uisaidie jamaa yako ije ione utimizo wa matumaini hayo?
TUNAHITAJI KUFANYA NINI?
8. Tunatakiwa tufanye nini iii tupate kibali ya Mungu?
8 Ye yote kati yetu asikate shauri kwa makosa kwamba, kwa kuishi tu yale tunayoona kuwa “maisha mema,” tutakuwa miongoni mwa wale watakaopata uzima katika taratibu mpya ya mambo ya Mungu. Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha katika Uyahudi, mtu mmoja alimwuliza hivi: “Nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” Jibu lilikuwa hivi: “Mpende [Yehova] Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa [nafsi] yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.” (Luka 10:25-28) Kwa wazi, mambo mengi yanatakiwa kuliko kusema tu kwamba tunamwamini Mungu, au tunakwenda mara kwa mara kwenye mikutano ambako Biblia inazungumzwa, au tunafanyia watu fulani mambo ya fadhili pindi kwa pindi. Badala yake, ile imani tunayojidai kuwa nayo inaongoza sana mawazo na tamaa na matendo yetu kila siku, siku kutwa.
9. Ni kanuni gani za Maandlko zinazoweza kutusaldia ili tuwe wenye kusawazika katika maoni yetu juu ya mambo ya kawaida ya maisha?
9 Kuukumbuka na kuuthamini uhusiano wetu na Mungu kutatusaidia tutende kwa hekima, nako kutatuhakikishia kupata kibali na msaada wake. (Mithali 4:10) Kwa kuyatazama mambo yote ya maisha kama yanavyohusiana naye na makusudi yake, tutaweza kutunza usawa mzuri kwa jinsi tunavyotumia maisha yetu. Inatupasa tufanye kazi ili tujipatie mahitaji yetu ya kimwili. Lakini Mwana wa Mungu anatukumbusha kwamba kusumbukia na kufuatia sana vitu vya kimwili hakutatuongezea maisha hata kidogo; kutafuta kwanza ufalme wake na haki yake kutayaongeza yaendelee milele. (Mathayo 6:25-33; 1 Timotheo 6:7 -12 ; Waebrania 13:5) Mungu anakusudia tuyafurahie kabisa maisha yetu ya jamaa. Lakini kujishughulisha sana na mambo ya jamaa hata kushindwa kuwapenda kikweli wale walio nje ya jamaa yetu kungekuwa kujishinda wenyewe, kungeipa jamaa yetu maoni madogo juu ya maisha, tena kungetukosesha baraka ya Mungu. Kucheza na tafrija ya jamaa kunafurahisha sana sana kunapofanywa kwa kadiri, pasipo kuruhusiwa kutuzuie kumpenda Mungu. (1 Wakorintho 7:29-31; 2 Timotheo 3:4, 5) Kwa kufanya mambo yote jamaa nzima au watu mmoja mmoja, kupatana na kanuni njema za Neno la Mungu, maisha yetu yatafurahisha sana, yakiwa na jambo la kweli ambalo limetimizwa, nasi tutakuwa tukiweka msingi mzuri kwa ajili ya wakati ujao wa milele. Basi, “lo lote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote kama kumfanyia Yehova . . . kwa maana mnajua kwamba ni kutoka kwa Yehova ndiko mtapokea zawadi ya urithi mnayoistahili.”—Wakolosai 3:18-24, NW.
KUJENGA PAMOJA KIJAMAA
10. Kuzungumza habari za Biblia nyumbani kwa kawaida, ni kwa maana kadiri gani?
10 Ikiwa washiriki wa jamaa wanataka kuendelea kufanya kazi ili wafikie miradi ile ile, ni jambo la manna sana sana, na ni lazima kweli kweli kuzungumza Neno la Mungu pamoja. Kila siku inampa mtu nafasi nyingi za kulinganisha makusudi ya Muumba na vitu vinavyoonwa na kufanywa. (Kumbukumbu la Torati 6:4-9) Inafaa kuweka kando nyakati za kawaida ili wote washiriki kusoma na kuzungumza habari za Biblia pamoja, labda kwa msaada wa vitabu vinavyoeleza Biblia. Kufanya hivyo kunaunganisha jamaa. Ndipo washiriki wa jamaa wanapoweza kutumia Neno la Mungu wasaidiane kushindana vya kufaa na magumu yanayoweza kutokea. Wazazi wanapoweka mfano mzuri, wasiruhusu vipindi hivyo vya kuzungumza Biblia pamoja na jamaa viharibiwe kwa vyepesi na mapendezi mengine, hilo linakaza katika akili za watoto ubora wa kuheshimu sana na kuthamini Neno la Mungu. Mwana wake alisema hivi: “Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa neno litokalo katika kinywa cha Mungu.”—Mathayo 4:4.
11. Kwa habari ya maendeleo ya kiroho, ni maelekeo gani ambayo yamepaswa kuepukwa katika jamaa?
11 “Kusiwe na [mgawanyiko] katika mwili,” lakini vimepaswa “viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe.” (1 Wakorintho 12:25) Na mwili wa jamaa umepaswa kuwa hivyo. Mwenzi mmoja asifikirie mno maendeleo yake mwenyewe ya kiroho katika maarifa na ufahamu hata akose kufikiria kwa unyofu wa moyo maendeleo ya kiroho ya mwenzi wake wa ndoa. Kwa mfano ikiwa mume haangalii vya kufaa mahitaji ya kiroho ya mke wake, huenda baadaye asiifikie miradi ile ile ambayo mume wake anafikia. Ikiwa wazazi hawapendezwi sana na ukuzi wa kiroho wa watoto wao, wawasaidie wajue namna kanuni za Neno la Mungu zinavyotumika na zinavyoweza kuleta furaha kubwa zaidi sana katika maisha, huenda wakaona kwamba mioyo na akili za watoto wao zinavutwa na roho ya ulimwengu unaowazunguka, roho ya kupenda mno vitu vya kimwili. Ili jamaa nzima ipate faida ya milele, kufanyeni kupokea maarifa kutoka Neno la Mungu kuwe sehemu ya kawaida, ya lazima ya maisha ya jamaa.
12. Haitupasi tuache kushirikiana na nani?
12 ‘Upendo ukianzia nyumbani’ kweli kweli, haupaswi umalizikie huko. Neno la Mungu lilitabiri kwamba hata wakati wa taratibu hii ya mambo, watumishi wake wa kweli wangekuwa jamaa kubwa ya ndugu na dada duniani pote. Anatuambia kwamba “kadiri tupatavyo nafasi,” imetupasa “tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio,” wale walio katika “ushirika mzima wa ndugu [zetu] walio katika ulimwengu.” (Wagalatia 6:10, UV; 1 Petro 5:9, NW) Kama jamaa, kukutana pamoja kwa kawaida na wale wa “jamaa” hiyo iliyo kubwa zaidi kumepaswa kuwe furaha, isiyopotezwa vyepesi kwa kupendelea mambo mengine.—Waebrania 10:23-25; Luka 21:34-36.
13. Ni daraka gani tulilo nalo juu ya watu walio nje ya kundi la Kikristo?
13 Lakini upendo wetu usionyeshwe kwa wale tu waliokwisha kuwa katika “nyumba ya Mungu,” kundi lake. (1 Timotheo 3:15) Kama Mwana wa Mungu alivyosema, tukiwapenda wale wanaotupenda tu, ndugu zetu tu, ‘tumefanya jambo gani la ziada?’ Ili tuwe kama Baba yetu wa mbinguni, inatupasa tufikie watu wote kwa moyo wote na kuonyesha fadhili na hali ya kusaidia wo wote na wote, tukitafuta kila wakati kushiriki pamoja nao habari njema za ufalme wa Mungu, tukiwa watu wa kwanza kufanya. Tunapoonyesha upendo wa kimungu katika njia hiyo kama jamaa, maisha yetu yanakuwa na maana na kusudi. Sisi sote, wazazi na watoto pamoja, tunaona maana ya kuonyesha sana upendo huo katika njia ambayo Mungu anauonyesha. (Mathayo 5:43-48; 24:14) Vilevile tunaishiriki furaha yote inayoweza kuletwa na utoaji huo wa moyo wote tu. —Matendo 20:35.
14. Ni kufuata shauri gani kunakoendeleza furaha ya jamaa?
14 Lo! matazamio ya ajabu namna gani yaliyoko mbele kwa ajili ya jamaa zinazoonyesha upendo huo! Wamejifunza kwamba njia ya kufanyia maisha ya jamaa kuwa yenye furaha ni kutumia shauri la Neno la Mungu. Yajapokuwapo magumu na mikazo ya maisha inayopata watu wote, jamaa hizo zinapata sasa hivi matokeo mema ya kufanya hivyo. Lakini wanatazamia mbele, nao hawafikirii miaka michache tu ya maisha kabla mauti (kifo) haijayakomesha yote. Kwa kuzitumaini ahadi za Mungu zisizoshindwa, kila mshiriki wa jamaa atajengwa kwa furaha kwa ajili ya wakati ujao wa milele.
15. Ni maulizo gani unayoweza kujiuliza juu ya faida za maongozi ya Maandiko yaliyoandikwa katika kitabu hiki?
15 Kitabu hiki kimeonyesha kutokana na Biblia kwamba kusudi la Mungu katika kuiumba dunia ni ili ikaliwe na watu. Yeye aliianzisha jamaa apate kutimiza kusudi hilo. Vilevile Yehova Mungu aliwapa wazazi, akina mama wazazi na watoto maongozi, na hayo nayo yameehunguzwa. Je! wewe umeweza kutumia kiasi cha kanuni hizo katika jamaa yako? Je! zimekusaidia kufanya maisha ya jamaa yako kuwa yenye furaha zaidi? Tunatumaini hivyo. Lakini wewe na jamaa yako mna tumaini gani kwa ajili ya wakati ujao?
16-18. Ni hali gani za ajabu ambazo Yehova Mungu amekusudia ziwemo katika dunia hii?
16 Je! ungependa kusaidia kuitunza dunia, kufanya mashamba yake yazae mazao mengi na majangwa yake yachanue maua? Je! ungependa kuona miiba na michongoma ikiondoka na mahali pake yakikaa mashamba ya miti yenye kuzaa matunda na misitu yenye kupendeza? Je! wewe na jamaa yako mngependa kutawala wanyama, si kwa kutumia bunduki, mijeledi (fimbo) na makomeo ya vyuma (vyuma vya kufungia milango) bali kupitia kwa upendo na kwa kutumainiana?
17 Ikiwa moyo wako unatamani sana wakati panga zitakapofuliwa kuwa majembe na mikuki kuwa miundu, wakati hawatakuwapo tena waundaji wa makombora (mizinga) wala wafanyizaji wa vita, wakati huo ndipo ungeifurahia taratibu mpya ya mambo ya Yehova. Utawala wa kisiasa wenye kuonea, pupa (tamaa mbaya) ya biashara na udanganyifu wa kidini ni mambo yatakayokuwa yamekwisha kupita. Kila jamaa itakaa katika amani chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake. Dunia hii itavuma kwa mlio wa furaha wa watoto watakaofufuliwa na nyimbo za kusisimua za ndege wengi. Nayo hewa itakuwa yenye kufurahisha sana kwa harufu nzuri ya maua badala ya kujaa uchafu unaotokana na viwanda.—Mika 4:1-4.
18 Ikiwa watumaini kwa moyo wote kumwona kilema akirukaruka kama kulungu, kuusikia ulimi wa bubu ukiimba, kuyatazama macho ya kipofu yakifunguliwa, kupata habari za kwamba masikio ya viziwi yamezibuliwa, (yamefunguliwa) kuona kwamba kunakuwa na tabasamu badala ya kuugua na kulia, na cheko inakuwa badala ya machozi na kuomboleza, afya na uzima wa milele vinakuwa badala ya maumivu na mauti (kifo), basi jitahidi, ujisaidie mwenyewe na jamaa yako, uchukue hatua ya lazima ili uishi milele katika taratibu mpya ya Yehova ambamo hali hizo zitakuwamo milele.—Ufunuo 21:1-4.
19. Wewe na jamaa yako mnawezaje kuwa kati ya wale watakaozifurahia baraka za taratibu mpya ya Mungu?
19 Je! jamaa yako itakuwa kati ya makutano ya watu wenye furaha watakaoijaa dunia wakati huo? Ni juu yako. Yafuate maagizo ambayo Yehova anatoa sasa ili yasaidie maisha ya jamaa. Fanyeni kazi pamoja kijamaa ili mwonyeshe sasa kwamba mngefaa kuingia katika namna ya maisha yatakayokuwa katika taratibu hiyo mpya. Jifunzeni Neno la Mungu, lifuateni maishani mwenu, waambieni wengine habari za tumaini la mbele. Kwa kufanya hivyo, ninyi jamaa yote mtakuwa mkijifanyia “jina zuri” pamoja na Mungu. “Jina zuri lafaa kuchaguliwa badala ya mali nyingi; kibali ni bora kuliko hata fedha na dhahabu.” Yehova hatasahau jina hilo: “Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka.” (Mithali 22:1, NW, maneno ye, pembeni; 10:7) Kwa fadhili zisizostahilika za Yehova, huenda wewe na jamaa yako mkabarikiwa mwe na wakati ujao wa milele wenye furaha iliyo bora sana.
[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 189]