Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 3/1 uku. 32
  • “Kabla ya Milima”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kabla ya Milima”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 3/1 uku. 32

“Kabla ya Milima”

“WEWE umekuwa kao letu katika vizazi vyote. Kabla ya milima kuzaliwa au wewe kutokeza dunia na ulimwengu, kutoka umilele hadi umilele wewe ndiwe Mungu.” (Zaburi 90:1, 2, New International Version) Maneno hayo yalielekezwa kwa Muumba wetu, nayo ni yenye kufariji kama nini—hasa leo, wakati hakuna chochote kinachoonekana kuwa thabiti!

Katika hali ya kiuchumi yenye kuharibika, wachache huhisi uhakika kuhusu wakati ujao. Ongezeko lenye kutisha la uhalifu na utumizi mbaya wa dawa za kulevya limebadili majiji mengine kuwa sehemu za kupigiwa vita. Hata ule mpango wa zamani za kale, familia, unadhoofika. Tunasikia juu ya mambo mapya kama vile familia za ugoni-jinsia-moja. Familia za mzazi mmoja zinakua katika idadi, mzazi mmoja akilazimika kukabiliana na mkazo mwingi. Amani ya familia nyingi imevunjwa-vunjwa na machukizo, kama vile kupigwa kwa mwenzi wa ndoa na kutendwa vibaya kwa watoto.

Ni nani atakayetuongoza kupitia nyakati hizi ngumu? Bila shaka, hakuna ukosefu wa shauri kutoka kwa wasaikolojia, wafunzi, na wengine, lakini mengi ya mashauri hayo yanapingana. Kwa kizazi kizima katika Magharibi, Dakt. Benjamin Spock alikuwa ndiye mshauri mkuu katika jambo la kuwaelimisha watoto. Halafu akakiri kwamba shauri lake lilikuwa la kimakosa!

Ni jambo la hekima zaidi kama nini kuwa na Mungu akiwa “kao letu”! Katika nyakati hizi zenye msukosuko, yeye ndiye mwamba wenye uthabiti, aliyekuwako “kutoka umilele hadi umilele.” Alisema hivi juu yake mwenyewe kupitia nabii Malaki: “Mimi ni Yehova: mimi sikubadilika.” (Malaki 3:6, NW) Viwango vya Mungu, kama vilivyorekodiwa katika Biblia, vinategemeka kabisa. Alikuwako “kabla ya milima,” na shauri lake, linalopatikana katika Maandiko Matakatifu, linategemea hekima yake ya milele. Ndilo jambo tunalohitaji barabara ili kupata furaha na mafanikio.

Kwa hiyo, ni jambo la hekima kuwa na uhakika katika Neno la Mungu, Biblia. Jifunze hiyo ili kufaidika na hekima ya Mungu. Tumaini yale unayojifunza, na uiache kuwa nuru ya kukuongoza kuelekea kwenye kijia cha uhai. (Zaburi 119:105) Wale tu wafanyao hivyo ndio walio na sababu ya kuwa na uhakika katika wakati ujao na amani ya akili ya kweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki