Tukio Lenye Maana Zaidi Katika Historia
Kwa nini? Tukio hilo lilikuwa kifo cha Yesu Kristo.
Lilitumikia kuitetea enzi kuu ya Mungu na likathibitisha kwamba mwanadamu angeweza kudumisha uaminifu-maadili mkamilifu kwa Mungu. Liliifungulia ainabinadamu taraja la kupata uhai wa milele katika hali za paradiso. Yesu mwenyewe ndiye aliyeanzisha ukumbusho wa kifo chake usiku kabla ya yeye kufa.
Ilikuwa sherehe sahili. Katika hiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, 20, NW. Je! wewe utakumbuka? Mashahidi wa Yehova wanakualika ujiunge pamoja nao katika kuadhimisha tukio hilo la maana zaidi katika historia. Mwaka huu tarehe ni Jumanne, Aprili 6, baada ya jua kushuka.
Tafadhali pata habari kutoka kwa Jumba la Ufalme lililo karibu na wewe juu ya wakati na mahali barabara. Sadaka za fedha hazichukuliwi, na wageni wanaalikwa wasikilize hotuba yenye kuarifu na kutazama zile taratibu sahili.