Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 1/1 uku. 27
  • Uthabiti Huvuna Thawabu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uthabiti Huvuna Thawabu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kuwa Baba Mzuri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Kuwalea Watoto Wako Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Shangwe na Matatizo ya Kuwalea Watoto Wanane Ili Wafuate Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Uchaguzi Wangu Kati ya Baba Wawili
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 1/1 uku. 27

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Uthabiti Huvuna Thawabu

YESU alitabiri kwamba wafuasi wake wangenyanyaswa, na ndivyo mtume Paulo alivyosema, kama isemwavyo kwenye 2 Timotheo 3:12: “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa [watanyanyaswa, NW].” Lakini uthabiti katika kumtumikia Yehova Mungu huleta thawabu nyingi.

◻ Ilikuwa hivyo katika mji mmoja kwenye mwambao wa kaskazini-mashariki mwa Malaysia. Ingawa baba mmoja alikuwa mfuasi mchaji sana wa Dini ya Buddha aliyewakemea watoto wake kwa ukali, yeye hakuweza kuwazuia binti zake watatu na wana wake watatu wasijifunze Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Hata mke wake alionyesha kupendezwa na kweli. Kisha siku moja jirani alimdhihaki hivi: “Wewe waweza kushindwaje kuwadhibiti watoto wako na kuwaruhusu wawe Mashahidi wa Yehova? Watoto wangu wote hushikamana nami na Dini yetu ya Buddha ya wazazi wa kale waliokufa. Unasikitisha!”

Baba huyo alirudi nyumbani upesi akitisha kumpiga yule dada aliyeongoza mafunzo pamoja na watoto wake. Hata hivyo, watoto walimtuliza wakaendelea kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova na kuhudhuria mikutano wakiungwa mkono na mama yao.

Hata hivyo, mwishowe, baba huyo aliikusanya pamoja familia nzima mbele yake. “Chagueni,” yeye akaamuru, “kati ya mimi na kubaki nyumbani au kuwa Wakristo na kuondoka nyumba hii.” Yule mwana mwenye umri mkubwa zaidi, aliye mvulana mpole sana, alianza mara iyo hiyo kufunga mizigo ili kuondoka. “La!” baba huyo akapaaza sauti. “Kwa kuwa nyinyi nyote ni watoto waasi, ni afadhali nife.” Kisha aliondoka nyumbani kwa kasi, akifuatwa na familia, iliyomsihi asijiue mwenyewe. Akiwa amevutiwa na sihi zao, alirudi nyumbani.

Wakati ulipita. Baba huyo akaanza kuona jinsi kweli ya Biblia ilivyokuwa ikiathiri vizuri mwenendo wa watoto wake. Siku moja alikutana na rafiki yake mwenye kudhihaki, sasa akiwa mtu mwenye huzuni sana, aliyesema hivi: “Nimekatishwa tamaa sana na watoto wangu. Wananidanganya na kuniibia.” Lakini yule baba ambaye watoto wake walikuwa wakijifunza pamoja na Mashahidi wa Yehova alisema hivi: “Oh, watoto wangu ni tofauti! Wao ni wenye fadhili sana kwangu na hata wamenisaidia kulipia mkopo wa gari langu nilipokuwa bila kazi ya kuajiriwa.”

Leo, binti watatu pamoja na mama wamebatizwa. Mwana mmoja ni painia wa pekee. Na namna gani yule baba aliyekuwa mchaji sana na mkali? Sasa ni mwenye urafiki na amehudhuria Ukumbusho.

Yehova alithawabisha yule mwana na dada zake watatu pamoja na mama yao kwa ajili ya uthabiti wao Kwake. Sasa wao ni wahubiri wa Ufalme wenye bidii, wakifurahisha moyo wa Yehova.—Mithali 27:11.y

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki