Sauti za Kuamini
WAKATI karne iliyopita ilipokwisha, sauti zenye kutegemeza sayansi, falsafa, na kukataa dini zilikuwa zikiathiri vibaya imani katika Mungu na uvuvio wa Biblia.
Lakini si sauti hizo pekee zilizosikiwa. Wachunguzi wengi waliona kwamba mengi yangeweza kusemwa katika kuunga mkono imani katika Mungu badala ya kukataa kuwapo kwake. Uchunguzi wao pia ulifunua uthibitisho mwingi kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililovuviwa.
Sauti moja kuu ilikuwa ya C. T. Russell. Mamilioni walisoma buku lake la 1886 The Divine Plan of the Ages. Sura yenye uzito mwingi sana ndani yalo ilikuwa “Kuwapo kwa Muumba Mwenye Akili Zaidi ya Wote Kumethibitishwa.”
Katika miongo iliyofuata, Russell aliandika makala, trakti, na vitabu vilivyotoa sababu zenye nguvu za kuamini katika Mungu na Biblia. Hivi vilichapishwa na Watch Tower Bible and Tract Society. Msimamizi wayo wa pili, J. F. Rutherford, aliandika Creation (1927) na vitabu vingine vilivyotegemeza sauti hiyo ya kuamini.
Karibuni sosaiti imetayarisha habari za ziada katika mambo haya. Mashahidi wa Yehova wanaweza kukuandalia habari kama hizi uzifikirie kwa makini.
Ikiwa ungependa habari zaidi au ungependa kutembelewa na mtu fulani ili aongoze funzo la Biblia nyumbani pamoja na wewe bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 2.