Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 12/15 uku. 32
  • “Amani ya Mungu ipitayo akili zote”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Amani ya Mungu ipitayo akili zote”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 12/15 uku. 32

“Amani ya Mungu ipitayo akili zote”

KATIKA historia yote, watumishi wa Mungu waaminifu wamepatwa na mikazo mikubwa ya kihisia-moyo. Hili ni kweli zaidi kama nini leo, tunapoishi katika “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo”! (2 Timotheo 3:1, NW) Mtume Paulo aliwashauri Wakristo wamtupie Yehova mahangaiko yao kupitia sala. Kukiwa na tokeo gani? “Amani ya Mungu, ipitayo akili zote itawahifadhi [“italinda,” NW] mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”—Wafilipi 4:7.

Hii “amani ya Mungu” ni nini? Ni utulivu unaoletwa na kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Muumba. Uhusiano huo wa karibu hutupa uhakikisho wa kwamba, ijapokuwa tuna mikazo, Yehova “hatawaacha watu wake, wala hatawatoroka wale walio wake.”—Zaburi 94:14, Today’s English Version.

Hii haimaanishi kwamba hatuwezi kupatwa na msiba. “Mateso ya mwenye haki ni mengi,” akaandika mtunga-zaburi. (Zaburi 34:19) Lakini amani ya Mungu yaweza kusaidia. Jinsi gani?

Amani ya Mungu ‘hupita akili zote,’ akaandika Paulo—au kama ifafanuliwavyo na Concordant Version, hiyo “imepita hali yoyote ya akili.” Hangaiko laweza kutufanya tupatwe na hisia-moyo nyingi na zenye kuhuzunisha sana. (Mhubiri 7:7) Hata hivyo, amani ya Mungu yaweza kututuliza, hasa tunapohitaji “nguvu ipitayo iliyo ya kawaida.”—2 Wakorintho 4:7, NW; 2 Timotheo 1:7.

Zaidi ya hayo, amani ya Mungu ni ulinzi. Yaweza ‘kulinda mioyo yenu na nia zenu,’ kama vile Paulo alivyowaandikia Wafilipi. Neno la Kigiriki lililotafsiriwa ‘kulinda’ ni usemi wa kijeshi ambao huleta wazo la walinzi wakilinda mchana na usiku. Kwa njia iyo hiyo, amani ya Mungu yaweza kuwa kama mlinzi wa mioyo na akili zetu muda wa saa 24.—1 Wakorintho 10:13; linganisha Waefeso 4:26.

Tunapofikiria mikazo yenye ushindani tunayokabili leo, je, hatupaswi kushukuru kwa ajili ya amani ya Mungu?—Zaburi 18:2; linganisha Kutoka 40:38.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki