Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 2/15 kur. 23-26
  • Jamhuri ya Dominika—Ingali Wazi kwa Uvumbuzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jamhuri ya Dominika—Ingali Wazi kwa Uvumbuzi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Uvumbuzi wa Aina Nyingine
  • Baraka za Kufikilia
  • Itikio Zuri la Wachanga
  • “Wavumbuzi” Kutoka Nchi Nyinginezo
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 2/15 kur. 23-26

Jamhuri ya Dominika—Ingali Wazi kwa Uvumbuzi

AKIWA kijana, Christopher Columbus alianza maisha ya baharia yaliyomwongoza hatimaye kwenye uvumbuzi wa visiwa vijulikanavyo leo kama West Indies. Katika Desemba 1492, chombo chake mashuhuri, Santa María, kilikwama mwambani karibu na pwani ya kaskazini ya kisiwa cha Española, kijulikanacho leo kuwa kisiwa cha Hispaniola, ambacho Haiti na Jamhuri ya Dominika hushiriki. Huko Columbus alianzisha makao ya kwanza ya Wazungu, ngome iliyojengwa haraka-haraka, akaiita La Navidad. Kisiwa hiki kikawa kitovu cha uvumbuzi wake mwingi zaidi.

Columbus alivumbua kwamba kisiwa hicho kilikaliwa na watu wenye sura ya kupendeza sana, wenye kutumainika, na wakaribishaji-wageni, Wahindi wa Taino. Wakati huo kulikuwa na karibu 100,000 ya wao. Hata hivyo, chini ya kutendwa vibaya na wavamizi, ambao haja yao kubwa ilikuwa kutafuta dhahabu, hesabu ya wakaaji ilipungua haraka. Kufikia 1570 yaripotiwa kulikuwa na Wahindi wa Taino karibu 500 tu waliobaki.

Leo, Jamhuri ya Dominika inakaliwa na watu wa jamii na rangi nyingi, ambao wazazi wao wa zamani walihamia hapa. Hata hivyo, wanaonekana kuwa na sifa nyingi nzuri za Wataino, wakiwa hasa watu wenye urafiki na wenye kuchukua mambo kirahisi. Jambo hili, pamoja na imani yenye unyoofu katika Mungu na kuistahi Biblia, limefanya kazi ya kuhubiri na kufundisha ya Mashahidi wa Yehova iwe yenye mafanikio sana katika nchi hii.

Uvumbuzi wa Aina Nyingine

Wamishonari wa kwanza wa Watch Tower, Lennart na Virginia Johnson, walifika Jamhuri ya Dominika wakati wa utawala wa mabavu wa Trujillo. Kwa furaha yao, walivumbua kwamba wengi waliitikia haraka na kwa nia nzuri ujumbe wao wa Biblia. Hata hivyo, hili halikupendeza wenye mamlaka na washauri wao wa kidini. Upesi wimbi la mnyanyaso likatokea, na imani ya Mashahidi hao wa mapema wa Dominika ilijaribiwa sana. Mpaka siku ya leo, uaminifu mshikamanifu na imani yao—hata kifo—bado inasimuliwa sana.

Mashahidi wa Yehova, ambao sasa hesabu yao ni karibu 16,000 katika nchi hiyo, wanajulikana vizuri. Wakati mfupi uliopita, vituo vitano vya televisheni vilionyesha kotekote nchini vidio ya Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name.a

Jambo hili lilieneza sana kazi ya Mashahidi si katika majiji makubwa zaidi tu bali pia katika miji midogo zaidi na katika sehemu fulani za mashambani. Kwa kufuatia, walipanga kampeni ya pekee ili kufikilia na kupeleka habari njema za Ufalme hadi kwenye maeneo haya ya mashambani.

Baraka za Kufikilia

Mashahidi wengi wachanga, wenye nguvu, na bidii walijitolea kutumia vipindi vya miezi miwili wakihubiri katika maeneo haya ya mbali. Jitihada zao zilithawabishwa sana. Katika eneo moja Mashahidi wawili walivumbua kupendezwa kusiko kawaida. Kwa kuwa ulikuwa wakati wa kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu, wa kila mwaka, walifanya mipango na kukaribisha watu waje. Jumba lilijaa, nao wakaongoza mkutano huo. Wakati ulipokwisha, walishangaa sana kugundua kwamba, kulikuwa na kikundi kingine kikubwa cha watu nje ya jumba waliokuwa wakingoja kuingia. Kwa hiyo waliwakaribisha ndani na kurudia programu hiyo. Sasa kuna kutaniko.

Utu wenye ukarimu na wa urafiki wa watu hao mara nyingi huwavuta kushiriki na washiriki wa familia zao na wengine kweli za Biblia wanazojifunza. Mwanafunzi mmoja wa Biblia alikuwa akifurika kwa shangwe alipostahili hatimaye kushiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba. Tayari alikuwa akiongoza mafunzo matano ya Biblia katika ujirani wake, lakini alifurahi kuwa na ushiriki mkubwa zaidi katika huduma.

Kukiwa na eneo kubwa lisilotembelewa kwa kawaida na wahubiri wa Ufalme, jitihada inafanywa kuhubiri kwa watu kwenye mabasi na wale wanaokuja majijini kufanya biashara au kununua vitu. Hili limeongoza kwenye matokeo yenye kuleta furaha, kama ilivyoonyeshwa na jambo lililoonwa kulingana na barua iliyopokewa na ofisi ya tawi. Ilikuwa kutoka kwa wanaume wawili katika eneo la mashambani, walioomba funzo la Biblia. Wakati Shahidi alipowatembelea, kumbe “wanaume” hao walikuwa na umri wa miaka 10 na 11. Lakini walipataje kujua kuhusu mpango wa kujifunza Biblia? Mtu fulani kutoka kijiji hicho alikuja kwenye jiji kuu kufanya biashara. Alikutana na Shahidi barabarani, aliyempa trakti na kumtolea funzo la Biblia nyumbani bila malipo. Aliporudi kijijini mwake, mtu huyu akampa msichana jirani wa umri wa miaka 12 trakti hiyo na kumwambia juu ya mpango wa kujifunza Biblia. Halafu, msichana huyu akapitisha ujumbe huo kwa wale wavulana wawili, walioandika barua mara moja. Funzo la Biblia lilianzishwa pamoja na wavulana hao, msichana huyo, mtu huyo, na watoto wake wawili.

Itikio Zuri la Wachanga

Kwa kweli, inaonekana kwamba wachanga, waliolelewa katika kweli na wengineo vilevile, wanachukua ibada yao ya Mungu kwa uzito. Kwa kielelezo, Tamar na dada yake Keila wote wawili walibatizwa wakiwa na umri wa miaka 10 wakaingia katika huduma ya upainia ya wakati wote kufikia miaka 11. Wendy Carolina alikuwa na umri wa miaka 12 alifananisha wakfu wake kwa ubatizo wa maji, na miaka miwili baadaye, katika 1985, akaanza upainia wa kawaida. Leo yeye ni mwalimu wa Biblia mwenye matokeo, akiwa bado anafurahia huduma ya wakati wote. Jovanny mchanga, aliyebatizwa akiwa na umri wa miaka 10 na kuwa painia wa kawaida akiwa na umri wa miaka 11, anaongoza mafunzo manne ya Biblia nyumbani. Wakati Rey mwenye umri wa miaka kumi alipogundua kwamba muuzaji wa vitabu vilivyotumiwa alikuwa na kijitabu kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, Rey alimwomba mama yake amnunulie kijitabu hicho. Alikisoma chote. Utafutaji wake wa fasihi za Biblia nyinginezo ulimwongoza hatimaye kwenye ofisi ya tawi. Leo anafurahia huduma ya wakati wote, na mama yake pia anamtumikia Mungu.

Ni nini kimesaidia hawa na wachanga wengineo kuthamini ubora wa mambo ya kiroho? Katika visa vingi mwongozo mzuri wa wazazi ulikuwa na fungu muhimu. Ilikuwa hivyo na Josué, ambaye wazazi wake Wakristo ni walimu wa shule. Mwangalizi asafiriye alipodokeza kwamba wazazi wajaribu kusaidia angaa mmoja wa watoto wao kuchukua huduma ya wakati wote, walielekeza uangalifu kwa Josué. Akiwa mwanafunzi mwenye kutokeza, Josué alipewa malipo ya elimu ya serikali ili ajifunze uhandisi. Baada ya mwaka mmoja na nusu akiwa katika chuo kikuu, yeye alikubali mwaliko wa kujiunga na kazi ya ujenzi kwenye makao makuu tata ya Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Dominika. Wazazi wake walionyesha kuridhika sana kwa kumtoa mwana wao kwenye utumishi wa Yehova.

“Wavumbuzi” Kutoka Nchi Nyinginezo

Maneno ya Yesu kwamba “mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache” yaweza kutumiwa kuhusu shamba hapa. (Mathayo 9:37) Uhitaji mkubwa na itikio zuri limesukuma Mashahidi kutoka nchi nyinginezo waje washiriki katika kuvumbua hazina za kweli za siku ya kisasa za eneo hilo—watafutaji kweli wenye mioyo mieupe.

Kutoka kisiwa cha jirani cha Puerto Riko kumetoka familia za Mashahidi waliopata uradhi wa kweli wakitumika katika maeneo tofauti ya Jamhuri ya Dominika. Akasema kichwa cha familia mmoja: “Kuweza kueleza imani na tumaini lako kwa masikio yenye usikivu kwa kweli hufanya kweli iwe hai!” Walipojua juu ya uhitaji wa hapa, Cecilia kutoka Sweden na Nia kutoka Marekani walijiunga pamoja na wahudumu kadhaa wengine wachanga wa wakati wote. Wanatumika katika sehemu ya ndani sana mahali penye joto na hali ya hewa ya kadiri. Vivyo hivyo, kule juu kwenye milima iliyofunikwa na misunobari ambako kuna ubaridi, familia mbili za Wakanada zilijiunga na familia ya Wadominika iliyokuwa imerudi kutoka Marekani. Wao ni sehemu ya kutaniko dogo nao wanaweza kufikia watu ambao bado hawajatembelewa na Mashahidi wa Yehova kwa miaka kumi.

Alfredo na Lourdes na watoto wao watano waliorudi kutoka New York City na wanashirikiana na kutaniko dogo katika mmojawapo miji ya pwani ya watalii yenye kupendeza. Wao hushangilia kuweza kushiriki katika kutafuta wale wenye mioyo minyoofu na kusaidia kutaniko kuongezeka. Roland, mwendesha kompyuta kutoka Austria, na mkeye, Yuta, wanaishi katika upande wa kusini wa nchi penye joto na pakavu. Wamepata shangwe ya kuona kutaniko jipya likifanyizwa tangu wafike. Katika mji wa jirani, kikundi cha dada mapainia watatu na mume na mke waliooana kutoka California waliripoti kwamba walikuwa na maombi mengi sana ya mafunzo ya Biblia hivi kwamba hawangeweza kuyaongoza yote. Kwa hiyo waliwatia moyo wale wenye kupendezwa wahudhurie mikutano kwenye Jumba la Ufalme la hapo na kutiwa katika orodha ya kungojea mafunzo ya Biblia. Ndugu ya Yuta, Stefan, anatumika kwa uaminifu pamoja na kutaniko dogo katika mji wenye kupendeza wa Samaná, upande wa kaskazini-mashariki. Katika miaka miwili tu, hesabu ya wahubiri wa Ufalme huko imeongezeka maradufu.

Upendo na bidii iliyoonyeshwa na hawa na wengineo ambao wamekuja kusaidia ni ya kusifiwa sana. Wamekubali mwito si wa kuhamia nchi mpya tu yenye utamaduni na desturi tofauti bali pia, katika visa vingi, wa kujifunza lugha mpya ili kutunza mahitaji ya kiroho ya watu wenye mfano wa kondoo. Jitihada zao zimetokeza itikio chanya kutoka kwa watu wa hapo.

Familia fulani za Wadominika zimeacha hali nzuri ya majiji makubwa na kwenda mashambani. Wote wanathawabishwa sana na shangwe ya kuvumbua hazina halisi za watafutaji wa kweli wenye mioyo mieupe.

Watafutaji wa hazina wa karne ya 15 hawakuleta baraka, bali utumwa na kuteseka kusikoelezeka kwa wenyeji Wataino. Hata Columbus mwenyewe hakufaidika na hazina za Bara za Amerika. Hatimaye alikamatwa na kuondolewa kutoka kisiwa hicho alichovumbua na kurudishwa Hispania akiwa amefungwa minyororo.

Leo aina tofauti ya uvumbuzi inaendelea, na hazina yenye thamani zaidi inapatikana. Watu wa Yehova wanajishughulisha kutafuta watu wenye mioyo mieupe wanaoitikia habari njema za Ufalme. Tokeo ni kwamba umati wenye kuongezeka daima unafurahia uhuru ambao Neno la Mungu pekee laweza kuleta. (Yohana 8:32) Wanatazamia wakati ambapo nchi hii ya milima, maporomoko ya maji yenye kupendeza, pwani zenye kupendeza, na mapango yenye kupendeza itakapokuwa, si kisiwa-paradiso tu, bali sehemu ya ulimwengu mpya inayotia ndani dunia nzima.—2 Petro 3:13.

[Maelezo ya Chini]

a Iliyotokezwa na Watch Tower Bible and Tract Society.

[Ramani katika ukurasa wa 24]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Jamhuri ya Dominika

[Picha katika ukurasa wa 24, 25]

Wachanga wanavumbua thamani ya mambo ya kiroho kwa kufuatia utumishi wa wakati wote

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki