Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 4/1 kur. 4-8
  • Ni Faida Gani Zaweza Kupatikana kwa Kuzungumza Dini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Faida Gani Zaweza Kupatikana kwa Kuzungumza Dini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kusikiliza na Kujifunza’
  • Kutoa Ushahidi kwa Mazungumzo
  • Mazungumzo Yenye Amani, Yenye Kujenga
  • Mazungumzo Yenye Matokeo Sana
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Sababu Inayofanya Wewe Upaswe Kupendezwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 4/1 kur. 4-8

Ni Faida Gani Zaweza Kupatikana kwa Kuzungumza Dini?

WAZAZI hungoja kwa hamu nyingi yale maneno ya kwanza mtoto wao asemayo. Wanaposikia herufi fulani zinazorudiwa-rudiwa miongoni mwa mgugumo, labda “Mama” au “Baba,” mioyo yao hufurika kwa furaha. Mara moja wanashiriki habari hizi na rafiki na jirani vilevile. Kuwasiliana kwa kwanza kwa mtoto ni habari njema kwelikweli iletayo furaha.

Yale makelele, kuona, na minuso inayochukuliwa na hisi za mtoto mchanga hutokeza mwitikio. Bila shaka, miitikio hutofautiana. Lakini ikiwa, baada ya kipindi cha wakati, kitoto kichanga kilikosa kuitikia misisimuo hii, wazazi waweza kuhofu kwa kufaa kwamba ukuzi wa mtoto wao huenda ukawa na kasoro.

Vitoto huitikia vizuri zaidi kwa watu vijuavyo. Mama anapomshika mtoto, kwa kawaida tabasamu kubwa hutokea. Hata hivyo, mguso wa mtu wa ukoo aliyetembelea unaweza kumtoza machozi, hata kukataa kwa kusumbua kushikwa naye. Watu wa ukoo wengi ambao hupatwa na jambo hili hawaachi. Kadiri mtoto awajuavyo vizuri zaidi, wanafurahi kizuizi cha kutojulikana kiondokapo, na tabasamu ya kitoto polepole huonekana.

Vivyo hivyo, watu wazima wengi husitasita kuzungumza itikadi zao za kidini waziwazi pamoja na mtu wasiyemjua kwa muda mrefu. Huenda wasielewe kwa nini mgeni angetaka kuzungumza juu ya habari ya binafsi—dini. Tokeo ni kwamba wanaruhusu kizuizi kiingie kati yao na wale wazungumzao juu ya Muumba. Wao hukataa hata kuzungumza kile ambacho ni silika ya binadamu, ile tamaa ya kuabudu.

Kwa kweli, twapaswa kupendezwa na kujifunza juu ya Muumba wetu, na kuzungumza na wengine kwaweza kutuweka katika hali ya kujifunza. Ndivyo ilivyo kwa sababu kwa muda mrefu Mungu amehusianishwa na mawasiliano ya waziwazi. Ebu tuone jinsi gani.

‘Kusikiliza na Kujifunza’

Mawasiliano ya kwanza ya Mungu na binadamu yalikuwa pamoja na Adamu katika bustani ya Edeni. Hata hivyo, baada ya Adamu na Hawa kufanya dhambi, waliamua kujificha Mungu alipowaita, alipotaka kuwasiliana nao zaidi. (Mwanzo 3:8-13) Hata hivyo, Biblia imerekodi mambo hususa ya wanaume na wanawake waliokaribisha mawasiliano pamoja na Mungu.

Mungu aliwasiliana na Noa kuhusu uharibifu wa ulimwengu mwovu uliokuwa ukija wa siku yake, hivyo Noa akawa “mjumbe wa haki.” (2 Petro 2:5) Akiwa msemaji wa Mungu kwa kizazi chake, Noa hakuonyesha tu imani katika kushughulika kwa Mungu na wanadamu bali pia alijitangaza peupe kuwa upande wa Yehova. Noa aliona mwitikio gani? Kwa sikitiko, watu wengi wa wakati wake ‘hawakutambua, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote.’ (Mathayo 24:37-39) Lakini sisi twafurahi kwamba washiriki saba wa familia ya Noa walisikiliza, wakatii maagizo ya Mungu, nao wakaokoka Gharika ya ulimwenguni pote. Kutoka kwao wanadamu wote wanaoishi leo wametokana nao.

Baadaye, Mungu aliwasiliana na taifa zima la watu, Israeli ya kale. Kupitia Musa, Mungu akawapa zile Amri Kumi na sheria nyinginezo karibu 600 zenye kutaka utii kama zile Amri Kumi. Yehova alitazamia Waisraeli wazitii zote. Musa aliagiza kwamba kila miaka saba, wakati wa Sikukuu ya Vibanda, Sheria ya Mungu ilipaswa isomwe kwa sauti kubwa. “Wakusanye watu,” yeye akaagiza, “wanaume na wanawake na watoto, na mgeni wako aliyemo malangoni mwako.” Kwa kusudi gani? “Wapate kusikia [“kusikiliza,” New World Translation] na kujifunza kumcha BWANA, Mungu wenu, na kuangalia kutenda maneno yote ya torati hii.” Wote walipaswa kusikiliza na kujifunza. Wazia jinsi ni lazima wawe walifurahia kuzungumza yale waliyosikia!—Kumbukumbu la Torati 31:10-12.

Zaidi ya karne tano baadaye, mfalme Yehoshafati wa Yudea aliwapanga wakuu na Walawi katika kampeni ya kurudisha ibada safi ya Yehova. Wanaume hawa walisafiri kotekote katika majiji yote ya Yudea wakiwafundisha wakaaji sheria za Yehova. Kwa kufanya sheria hizo zizungumzwe peupe, mfalme alionyesha moyo mkuu kwa ibada ya kweli. Kwa upande wa raia wake, walipaswa kusikiliza na kujifunza.—2 Mambo ya Nyakati 17:1-6, 9.

Kutoa Ushahidi kwa Mazungumzo

Mungu alimtoa Mwanaye mwenyewe, Yesu, duniani atumike akiwa Msemaji Wake. (Yohana 1:14) Wanafunzi watatu wa Yesu walipoona mgeuko-sura mbele yao, walisikia sauti ya Mungu mwenyewe ikitangaza: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.” (Mathayo 17:5) Wao walitii kwa utayari.

Vivyo hivyo, Yesu aliwaagiza mitume wake watangaze makusudi ya Mungu kwa wengine. Lakini ilipobaki karibu miezi sita ya huduma, Yesu alijulisha kwamba kazi ya kuhubiri Ufalme wa mbinguni ilikuwa nyingi sana hivi kwamba wanafunzi wengi wangehitajiwa. Aliwafundisha 70 kati yao jinsi ya kuzungumza juu ya Ufalme wa Mungu pamoja na watu wasiowajua halafu akawatuma kueneza ujumbe huo peupe. (Luka 10:1, 2, 9) Muda mfupi kabla hajarudi kwa Baba yake mbinguni, Yesu aliwasihi wafuasi wake wachukue hatua ya kwanza ya kuzungumza na wengine juu ya ujumbe huu, hata kuwaamuru hivi: “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, . . . na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi.” (Mathayo 28:19, 20) Ulimwenguni pote, Wakristo wa kweli leo wanatimiza utume huo kwa kuzungumza habari njema za Ufalme wa Mungu pamoja na jirani zao. Mazungumzo haya huwasaidia kutoa ushahidi wa ile kweli kuhusu Muumba, Yehova.—Mathayo 24:14.

Mazungumzo Yenye Amani, Yenye Kujenga

Ni katika njia gani wanafunzi wa Yesu walikuwa wazungumze itikadi zao pamoja na wengine? Hawakuwa wawakasirishe wapinzani, wala hawakuwa wabishane na wapinzani. Badala ya hilo, walikuwa watafute-tafute wale waliokubali habari njema, kisha watoe uthibitisho wa Maandiko ya kuiunga mkono. Bila shaka, Mungu aliona mwitikio wa wale waliokutana na wanafunzi wa Mwanaye, kama vile Yesu alivyotangaza: “Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma.” (Mathayo 10:40) Ilikuwa kumkataa Mungu kama nini wakati wengi wa watu walioishi wakati wa Yesu walikataa ujumbe wake!

“Haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi,” mtume Paulo Mkristo ashauri. “Bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli.” (2 Timotheo 2:24, 25) Jinsi Paulo alivyotangaza habari njema kwa watu wa Athene, Ugiriki, inatoa kielelezo chema. Yeye alihojiana na Wayahudi katika masinagogi yao. Kila siku sokoni alizungumza na “wale waliokutana naye.” Ingawa bila shaka wengine walipenda tu kusikiliza mawazo mapya, Paulo alizungumza kwa wazi na kwa upole. Yeye alizungumza na wasikilizaji wake ujumbe wa Mungu, ambao uliwahimiza watubu. Mwitikio wao ulikuwa sawa na ule wa watu leo. “Wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.” Paulo hakusisitiza kurefusha mazungumzo. Akiwa amehubiri ujumbe wake, yeye “akaondoka akawaacha.”—Matendo 17:16-34.

Baadaye, Paulo akawaambia washiriki wa kutaniko la Kikristo katika Efeso kwamba ‘hakujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa, bali aliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba.’ Tayari, alikuwa ‘amewashuhudia Wayahudi na Wayunani wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.’—Matendo 20:20, 21.

Vielelezo hivi vya Kimaandiko vyafunua jinsi watumishi waaminifu wa Mungu katika nyakati za Biblia walivyozungumzia dini. Hivyo leo, Mashahidi wa Yehova kwa utii huzungumza dini pamoja na jirani zao.

Mazungumzo Yenye Matokeo Sana

‘Sikia Neno la Mungu.’ ‘Sikiliza amri zake.’ Kusihi huko hupatikana katika Biblia mara nyingi jinsi gani! Wewe unaweza kuitikia mwongozo huu wa Kibiblia Mashahidi wa Yehova wazungumzapo na wewe wakati ujao. Sikiliza ujumbe wanaokuletea kutoka katika Biblia. Ujumbe huu sio wa kisiasa bali unatangaza serikali ya kimbingu ya Mungu, Ufalme wake. Hii ni njia ya Mungu ya kuondoa visababu vya magombano ya siku hizi. (Danieli 2:44) Baadaye utawala huu wa Mungu kutoka mbinguni utapanga dunia yote ifanywe kuwa paradiso kama vile bustani ya Edeni.

Polisi mmoja wa upelelezi alikataa mara nyingi kusikiliza Mashahidi wa Yehova walipozungumza naye kuhusu Biblia. Lakini kukiwa na ongezeko la uhalifu ambao ilimbidi kukabili, alishangazwa na uhakika wa maisha. Hivyo akamwambia Shahidi aliyemtembelea baadaye kwamba angefanya uchunguzi wa uthibitisho wa ujumbe wa Biblia. Mazungumzo ya kawaida yakaanzishwa. Ingawa polisi huyo alihama mara nyingi, Mashahidi walimtafuta kwa furaha katika kila makao mapya ili waendelee na mazungumzo hayo. Mwishowe polisi huyo akasema: “Ule uthibitisho niliokuwa nikitafuta ulikuwamo humo ndani ya Maandiko Matakatifu muda wote. Ikiwa Mashahidi hao hawangestahimili kuzungumza nami, bado ningekuwa huko nikishangaa maana ya maisha ni nini. Uhakika ni kwamba nimejifunza kweli, nami nitatumia maisha yangu yote nikiwatafuta wale wanaomtafuta Mungu kama nilivyokuwa nikimtafuta.”

Wasikilizaji wenye kupendezwa kwa unyoofu wanataka kujua zaidi. Wanatazamia kwa haki sababu za itikadi zinazotolewa. (1 Petro 3:15) Kama vile mtoto mchanga kila mara aulizavyo wazazi wake maswali na kuwatazamia kuyajibu, huenda wewe watazamia kwa haki Mashahidi wakupe majibu yenye maana. Waweza kuwa na hakika kwamba wao watarudi kwa furaha na kuzungumza ujumbe wa Biblia zaidi pamoja nawe.

Huenda ukawa tayari unajua machache kuhusu Biblia. Huenda unatambua kwamba yale Mungu anakutazamia ufanye yatahusisha mabadiliko fulani katika njia yako ya maisha. Usisite-site kufuatia mambo kwa sababu ya woga wa kwamba matakwa ya Mungu yatakugharimu mambo mengi mno. Hayo yatakuletea tu furaha ya kweli. Utathamini jambo hili ufanyapo maendeleo hatua kwa hatua.

Kwanza kabisa, fikiria Yehova ni nani, yale anayokutazamia uyafanye, na yale anayotoa. Waulize Mashahidi wakuonyeshe yale Biblia isemayo kuhusu mambo haya. Hakikisha yale wasemayo katika nakala yako ya Biblia. Kujifunza kwamba Mashahidi wana kufikiri kuzuri katika yale wanayotoa kuwa kweli kuhusu dini, bila shaka utataka kuchunguza zaidi mambo mengine mengi mazuri wanayoweza kushiriki pamoja nawe katika Maandiko.—Mithali 27:17.

Unakaribishwa uwaone Mashahidi katika mahali pao pa kukutania, Jumba la Ufalme. Hapo utasikia mazungumzo yenye faida ya Neno la Mungu. Utaona jinsi wale waliopo wanavyofurahia kuzungumza na mmoja na mwenzake kuhusu makusudi ya Mungu. Waruhusu Mashahidi hawa wakusaidie ujifunze kweli kuhusu mapenzi ya Mungu kwetu leo. Itikia mwaliko wa Mungu wa kuzungumza juu ya ibada ya kweli nawe upokee ukubali wake, hata uhai wa milele katika Paradiso.—Malaki 3:16; Yohana 17:3.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Noa alizungumza waziwazi kuhusu kusudi la Mungu

[Picha katika ukurasa wa 7]

Mashahidi wa Yehova hufundisha kweli za Biblia kwa wengine, kama Paulo alivyofanya katika Athene ya kale

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki