Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 9/1 uku. 32
  • ‘Kama Tu Kila Mtu Angalikuwa Kama Wao!’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kama Tu Kila Mtu Angalikuwa Kama Wao!’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 9/1 uku. 32

‘Kama Tu Kila Mtu Angalikuwa Kama Wao!’

Haya yalikuwa maneno ya mwandikaji katika gazeti la Luxembourg liitwalo Letzebuerger Journal. Alikuwa akizungumza juu ya nani?

Alikuwa ameenda Poland kuhudhuria sherehe ya mwaka wa 50 ya kukombolewa kwa Auschwitz naye akasema kwamba kikundi kimoja kilichokuwa kimeteseka sana huko hakikutajwa kamwe. Kwenye gazeti la Februari 2, 1995, alitambulisha kikundi hicho kuwa Mashahidi wa Yehova, na akaandika hivi: “Wala kizuizi kibaya sana au kambi ya mateso iliyo mbaya sana, wala tisho la kufa njaa kambini wala kuuawa kwa shoka au kukatwa kichwa hakungewafanya wakane imani yao.” Yeye aliendelea kusema hivi: “Hata polisi wakatili wa SS walistaajabishwa na ujasiri ambao Mashahidi wa Yehova walikuwa nao hadi kifo.”

Mashahidi wa Yehova hawakutaka kufa. Lakini, kama vile Wakristo katika karne ya kwanza, maelfu yao walichagua kufa badala ya kuridhiana kanuni za Kikristo. Imani kama hiyo iliwatia alama ya kuwa tofauti kabisa katika siku zenye huzuni za Utawala wa Nazi.

Mwandikaji huyo alimalizia hivi: “Kama tu watu wote wangalikuwa kama Mashahidi wa Yehova!” Kama wangalikuwa, vita ya ulimwengu ya pili haingalitokea kamwe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki