Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 9/1 uku. 31
  • Wakristo wa Kweli Watanyanyaswa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakristo wa Kweli Watanyanyaswa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kuvumilia kwa Furaha Ijapokuwa Mateso
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Wenye Furaha Wajapoteswa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 9/1 uku. 31

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

Wakristo wa Kweli Watanyanyaswa

TANGU siku za Abeli, wengi wa watumishi wa Yehova wamevumilia mnyanyaso wa kidini. (Luka 11:49-51) Na haishangazi, kwa kuwa Biblia huonya kwamba “wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa [“watanyanyaswa,” NW]”! (2 Timotheo 3:12) Vivyo hivyo, leo katika zaidi ya nchi 25, Mashahidi wa Yehova wako chini ya marufuku nao huvumilia mnyanyaso.

Katika nchi ambapo Mashahidi wa Yehova wamepigwa marufuku na kunyanyaswa na watu wa dini, wahubiri wa habari njema zaidi ya 12,000 huendelea kufanya kazi kwa bidii, wakijifunza Biblia pamoja na zaidi ya watu 15,000. Bila shaka, kazi yao ya kuhubiri inafanywa kwa busara. Kwa ujumla, wanafanya mikutano yao ya Kikristo katika nyumba za watu binafsi, nao hujihadhari wanapokaribisha watu wenye kupendezwa kwenye mikutano kama hiyo.

Majuzi serikali imekuwa na mtazamo ufaao kidogo kuelekea Mashahidi, ambao sasa hufanya nyingi ya kazi yao bila kuingiliwa kijeuri. Hata hivyo, vikundi mbalimbali vya kidini vimetumia uvutano wavyo kuchochea matatizo.

Katika jiji moja umati wenye ghasia wa washupavu wa kidini zaidi ya 200 ulitembea kuelekea nyumba fulani ambamo Mashahidi wa Yehova karibu 50 walikuwa wakifanya mkutano wa kutaniko. Wengine katika kikundi hicho chenye ghasia walikuwa wamebeba mawe na kupiga kelele za shime za kidini. Kusudi lao la wazi lilikuwa kushambulia Mashahidi na kuharibu nyumba ile. Inaonekana viongozi wa kidini walikuwa wakitazama utendaji wa mikutano kwa muda fulani na kungoja wakati unaofaa kushambulia. Umati huo wenye ghasia ulikuwa karibu tu kuingia katika nyumba ile polisi 15 walipofika na kuamuru umati utawanyike. Hilo lilishangaza Mashahidi, kwa kuwa hakuna yeyote wao alikuwa amepata wakati wa kuita polisi.

Hata hivyo, kwenye pindi nyingine, wapinzani wamefaulu zaidi. Mashahidi kadhaa wameletwa mahakamani na kuhukumiwa kifungo. Kesi moja ya mahakama imekuwa ikiahirishwa kwa miaka kadhaa, na inaonekana kwamba viongozi wa mashtaka walikuwa wamepoteza hamu ya kuifanya. Hata hivyo, kwa uchochezi wa kasisi wa mahali hapo, jambo hilo lilipelekwa tena mahakamani, na Shahidi huyo akafungwa gerezani.

Katika sehemu nyingine kikundi cha Mashahidi kilikutana katika nyumba ya binafsi ili kufanya ukumbusho wa Mlo wa Jioni wa Bwana. Jioni hiyo baadaye polisi kadhaa wakamshika mwenye nyumba hiyo na mzee aliyekuwa ameongoza mkutano huo. Walipigwa sana kwenye kituo cha polisi. Wakahojiwa kwa njia ya ukatili kwa muda wa saa kadhaa. Mmoja wa Mashahidi pia alivumilia kuteswa kwa kutiwa ndani ya kisima chenye maji baridi.

Kwa nini polisi walikuwa wakiendeleza shambulizi kama hilo? Tena, kikundi cha washupavu wa kidini, kwa msaada wa kasisi wa mahali hapo, kilichochea tendo la polisi. Baadaye mkubwa wa polisi akafunua kwamba hao walishikwa bila idhini yake. Wakaomba msamaha, na watu mmoja-mmoja waliohusika katika kuwapiga wakaadhibiwa.

Duniani pote Mashahidi wa Yehova wanaendelea kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu, hata wakikabili upinzani wenye jeuri. Wao hufuata shauri hili la Yesu: “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.”—Mathayo 10:16.

[Picha katika ukurasa wa31]

Abeli alikuwa wa kwanza kunyanyasway

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki