Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 10/1 kur. 3-8
  • Wenye Furaha Wajapoteswa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wenye Furaha Wajapoteswa!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Shabaha ya Ibilisi
  • Sababu ya Yehova Kuruhusu Mateso
  • Sababu ya Kuwa Wenye Furaha Tujapoteswa
  • Tuzidi Kusonga Mbele Tukiwa Washika Ukamilifu
  • Ni Wenye Furaha Ingawa Wanateswa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Wakristo Wanaelekeana na Mateso kwa Uvumilivu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • ‘Ninyi ni Wenye Furaha Wakati Watu Wanawatesa Ninyi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kunyanyaswa kwa Ajili ya Uadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 10/1 kur. 3-8

Wenye Furaha Wajapoteswa!

“Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa ufalme wa mbingu ni wao.”​—MATHAYO 5:10, NW.

1. Nero Mfalme wa Kiroma alitokeza mateso gani?

WAKIWA wamevikwa ngozi za wanyama, waliraruliwa na mbwa wakaangamia, au wakapigiliwa misumari wenye misalaba, au wakapewa maangamizi ya kutupwa kwenye miali ya moto kuungua, wapate kuwa kama mwanga wa usiku, wakati mchana ulipokuwa umekwisha.” Ndivyo alivyoandika Tasitu Mwanahistoria Mroma. (The Annals, Kitabu cha XV, fungu la 44) Wenye kupatwa na hayo walikuwa akina nani? Ni Wakristo​—wanafunzi wa Yesu Kristo. Uvumi ulionyesha kwamba Mfalme Nero ndiye aliyesimamia uteketezaji wa Roma kwa moto (mwaka wa 64 W.K.), naye alijaribu kusingizia wafuasi wa Yesu kuwa wenye hatia ya kufanya hivyo. Kwa njia hiyo yakatokezwa mateso ya kwanza kati ya mateso mbalimbali waliyotendwa Wakristo wakati Roma ya kale ilipokuwa ikisitawi sana.

2. (a) Yesu Kristo alisema nini juu ya wale ‘wanaoteswa kwa ajili ya haki’? (b) Ili Mashahidi wa Yehova wawe wenye furaha wajapoteswa, ni lazima wajue nini?

2 Wakristo hao wa kwanza waliwezaje kuvumilia mateso hayo ya kinyama? Mashahidi wa Yehova wa zamani na wa sasa wameonaje uwezekano wa kuwa wenye furaha wanapoendelea kusumbuliwa au kuumizwa kwa makusudi kwa kusudi la kuifagilia mbali imani yao ya kidini? (2 Wathesalonike 1:3-5) Yesu Kristo alisema: “Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa wafalme wa mbingu ni wao.” (Mathayo 5:10, NW) Lakini, ili Mashahidi wa Yehova wawe wenye furaha wajapoteswa, ni lazima wajue (1) shabaha ya Ibilisi ya kuleta mateso juu yao; (2) kwa sababu gani Yehova anaruhusu kuwe na dhiki hiyo; (3) kwa sababu gani watumishi wa Mungu wanaweza kuwa wenye furaha wajapoteswa; (4) linaloweza kufanywa ili kujitayarishia mateso; na (5) namna mateso yanavyoweza kukabiliwa kwa uvumilivu.

Shabaha ya Ibilisi

3, 4. (a) Ni nani hasa anayechochea mateso wanayopata Mashahidi wa Yehova? (b) Yesu alitambulishaje mchochezi mkuu wa mateso haya?

3 Watawala Waroma hawakuwa na sababu ya kwamba wangetendwa ubaya wo wote na Wakristo wa kweli wenye kupenda amani. Mashahidi hao wa Yehova walikuwa wakizitolea utii wa kiasi “mamlaka zilizo kuu” za kiserikali na ‘wakamtolea Kaisari vitu vya Kaisari, lakini vitu vya Mungu wakamtolea Mungu.’ (Warumi 13:1-7; Mathayo 22:21, NW) Wafalme wa Roma hawakujua kwamba mtu fulani wa kujificha alikuwa muda wote huo akiendelea kuchochea chuki juu ya Mashahidi wa Yehova, akawa akifanya hivyo zamani hizo za nyuma mpaka kwa “Habili, yule mwenye haki.” (Mathayo 23:33-36; Waebrania 11:4, 32-40; 12:1) Mchochezi huyo mwovu wa mateso hayo si mwingine, bali mpaka leo hii hii ni Shetani yule Ibilisi. Akiwa mpinzani wa Mungu, na wa watu wa Yehova, yeye “kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.”​—1 Petro 5:8.

4 Yesu aliwaambia wanafunzi wake mara nyingi kwamba wangeteswa. Kwa mfano, alisema hivi: “Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa wao wamenitesa mimi [na kweli walifanya hivyo], watawatesa ninyi pia.” (Yohana 15:20, NW; 16:2; Mathayo 10:22, 23) Zaidi ya hilo, Kristo alieleza wazi ili kusiwe na shaka juu ya mwenye kuchochea mateso hayo wakati alipoliambia hivi moja la yale “makundi saba”: “Tazameni! Yule Ibilisi ataendelea kutupa wengine kati ya ninyi ndani ya gereza ili mpate kutiwa kikamili kwenye jaribu.” (Ufunuo 1:1, 4; 2:10, NW) Hata hivyo, shabaha ya Ibilisi ni nini katika kuwatesa Mashahidi wa Yehova?

5. Shabaha ya Ibilisi ni nini katika kuleta mateso juu ya watumishi wa Yehova?

5 Shabaha ya Shetani katika kuleta mkazo na mateso juu ya watumishi wa Yehova ni kuwalazimisha waache imani yao kwa kukubaliana na wapinzani wao. Anataka kuangamiza uhusiano wenye thamani kubwa walio nao pamoja na Baba yao wa kimbingu. Pale pale mwanzoni wakati dhambi ilipoingia, Yehova Mungu alitabiri uadui kati ya “nyoka” na “mwanamke” wa Mungu wa mfano, na kati ya “uzao” wao! (Mwanzo 3:14, 15) Pasipo shaka Yesu alitambulisha nyoka huyo kuwa ni Shetani na akawaambia watesi Wake kwamba walikuwa ‘wametoka kwa baba yao Ibilisi,’ na kwa hiyo walikuwa wa “uzao” wa Mpinzani huyo. (Yohana 8:31-59) Katika hizi “siku za mwisho” wakati wa Ibilisi ni mfupi na hasira yake ni kubwa kweli kweli. (2 Timotheo 3:1-5; Ufunuo 12:7-17) Kwa hiyo uadui kati ya “uzao” huo wa pande mbili unaendelea, na kila mtu duniani lazima mwishowe ajipange ama upande wa uzao wa kimungu au wa uzao wa kiibilisi. (Linganisha 1 Yohana 3 :10.) Kwa hiyo, ikiwa mtu anamtumikia Yehova Mungu kwa uaminifu, huyo tayari amekwisha kuwa au atakuwa akiletewa mateso. Shetani Ibilisi atahakikisha jambo hilo linatukia.​—2 Timotheo 3:12,

6. Shetani ametokeza suala gani kuu na ametia mashaka juu ya jambo gani kuhusu wanadamu?

6 Shetani ametokeza suala la enzi kuu ya ulimwengu mzima, na ametokeza shaka la kwamba wanadamu hawawezi kushika ukamilifu wanapotiwa chini ya jaribu. Kwa mfano, ukamilifu kwa Mungu ndilo suala lililotokezewa ubishi wakati Shetani alipochochea mateso juu ya yule mtu aliyeitwa Ayubu, ambaye mke wake na “wafariji” watatu wake walitumikia kusudi la Ibilisi kwa kujua au bila kujua. (Ayubu 1:8–2:9;16:2; 19:22, 28) Kama vile kisa cha Ayubu kinavyoonyesha wazi, Ibilisi alimtolea Yehova mwito wa ushindani, akidai kwamba hakuna mwanadamu angebaki mwaminifu kwa Mungu kama Shetani anaruhusiwa kumjaribu. Basi, Ibilisi anatesa Mashahidi wa Yehova ili avunje ukamilifu wao na kuthibitisha kwamba mwito wake wa ushindani ni wa kweli.

7. Ni nini kinachotosha kufanya Mkristo awe amekubali kukana imani yake, lakini Yesu alitendaje aliposhawishwa hivyo?

7 Shetani anajua kwamba ‘tendo moja la ibada’ analopewa linatosha kufanya Mkristo awe amekubali kukana imani yake na kuunga mkono mwito wa ushindani wa Ibilisi wa kwamba wanadamu hawawezi kubaki waaminifu kwa Mungu wakiwa chini ya jaribu au mateso. Wakati Ibilisi alipomwonyesha Yesu “falme zote za ulimwengu na utukufu wazo,” mtesi huyo aliye mkubwa zaidi alisema nini? “Vitu vyote hivi nitakupa wewe ikiwa utaanguka na kufanya tendo moja la kuniabudu mimi.” Lakini Yesu alipokataa kwa uthabiti, hatua hiyo iliunga mkono ibada ya kweli, ikatetea upande wa Yehova wa lile suala linalohusu enzi kuu ya ulimwengu mzima na akaonyesha Ibilisi ni mwongo.​—Mathayo 4:8-11, NW.

8, 9. (a) Wakristo wa kwanza walionyeshaje kwamba hawangempa Shetani ‘tendo moja la ibada’? (b) Ni kwa njia gani Wakristo fulani wa karne ya 20 wamejaribiwa kwa namna iyo hiyo, nao wamechukua msimamo gani?

8 Basi, ilifaa sana kwamba Wakristo waaminifu wa kwanza wakakataa kufanya ‘tendo moja la kuabudu’ ambalo lingaliunga mkono upande wa Shetani wa lile suala kuu! Wafuasi washikamanifu wa Kristo walikataa kuchoma uvumba kumtukuza mfalme Mroma, ingawa kukataa kwao kulifanya wauawe. Kuhusu jambo hilo, Daniel P. Mannix aliandika hivi: “Ni Wakristo wachache sana waliokubali kutenda tofauti na imani yao, ingawa mara nyingi madhabahu yenye moto uliokuwa ukiwaka ilikuwa ikiwekwa katika uwanja wa michezo na mapigano ili waweze kuitumia. Jambo la pekee lililotakwa kwa mfungwa ni kudokoa kwa vidole kiasi kidogo sana cha uvumba na kukiangusha-angusha juu ya mwali wa moto. Halafu alipewa Hati ya Utoaji Dhabihu na kuachiliwa huru. Pia alielezwa kwa makini kwamba yeye hakuwa akiabudu mfalme kwa kufanya hivyo; alikuwa akiutambua tu uungu wa mfalme akiwa ndiye kichwa cha serikali ya Kiroma. Hata hivyo, kama kuna Wakristo waliotumia nafasi hiyo ya kuokoa maisha yao, walikuwa wachache kabisa.” (Those About to Die, ukurasa wa 137) ‘Tendo moja tu la kuabudu’ kwa njia hiyo lingalitosha kumridhisha Shetani.

9 Wakristo fulani wa karne ya 20 wamejaribiwa vivyo hivyo. Tangu wakati wa kuwakamata Mashahidi wa Yehova na muda wote wa kuwatia kizuizini mara nyingi katika kambi za mateso za Nazi, jitihada zilifanywa kuwalazimisha wamkane Yehova na wakatae kuendeleza uhusiano wao na watu wake. Kwa kusudi hilo Wanazi walitayarisha tangazo lenye azimio ambalo Mashahidi walipewa watie sahihi ndipo waweze kuachwa huru. Jambo la pekee lililotakwa kwa mtu ni sahihi yake. Hata hivyo, ni Mashahidi wachache tu waliotia sahihi.

10. Kwa sababu gani lingekuwa jambo la kukosa hekima kukubali kukana imani kidogo kwa tumaini la kupata uhuru wa kuhubiri?

10 Kwa sababu tunajua kusudi la Shetani la kufanya Mashahidi wa Yehova wateswe, tusijiache kamwe tushindwe na kishawishi cho chote cha kiibilisi cha kuepa suala fulani ili tuepuke matata. Hata tusiweke akilini kiwazo chenye makosa cha kwamba, tukikubali kukana imani kwa kiasi kidogo tu, hiyo itatuweka huru upesi ili tukafanye kazi ya kuhubiri. Kukubali kuacha ukamilifu wetu kwa njia yo yote kunaweza kutuletea anguko la kabisa. (Linganisha Mathayo 13:21; Wagalatia 6:12.) Wakati kukubaliana na wapinzani kunapohusu kufanya ‘tendo moja la kuabudu,’ tunakuwa hatufai tena kuwakilisha faida za Ufalme wa Yehova. Tuwe na uhakika wa kwamba tendo moja tu la kuvunja ukamilifu wetu lingemletea Ibilisi furaha kubwa, na hakika sisi hatutaki kumfurahisha. Bali, tunajaribu kufanya moyo wa Yehova uwe na shangwe kwa kushika ukamilifu kwa njia ambayo itampa jibu la kumtolea yule Mchekaji Mkuu mwenye madharau.​—Mithali 27:11.

Sababu ya Yehova Kuruhusu Mateso

11. Ni kwa sababu gani hasa Yehova anaruhusu watu wake wateswe?

11 Baba yetu wa kimbingu angeweza kuzuia watu wake wasipatwe na mateso akitaka. Lakini yeye anachagua kuyaruhusu yawepo, nasi tukijua sababu yake tutasaidiwa kuwa wenye furaha tujapoteswa. Kila shahidi wa Yehova anayeendeleza ukamilifu chini ya jaribu lenye kuchochewa na Ibilisi anaonyesha Shetani ni mwongo na kutoa ushuhuda wa kwamba hata mwanadamu asiye mkamilifu anaweza kubaki mwaminifu kwa Mungu ajapojaribiwa au kuteswa vibaya sana. Mtu aliye mshikamanifu anatetea upande wa Mungu wa lile suala na kuunga mkono haki ya Yehova ya kutawala akiwa Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Mzima. Ni furaha iliyoje kuongezea ushuhuda wa kwamba “yeye atawala kwa kuwapita wote”!—Zaburi 47:9, Today’s English Version.

12, 13. Ni kwa sababu gani ya ziada Yehova anaruhusu Wakristo wateswe, na ni nani kati yao watakaokuwa na nafasi yenye kudumu katika mpango wa Mungu?

12 Pia Yehova anaruhusu mateso ili ajaribu ushikamanifu wa wale ambao wamejiweka wakf kwake. Amekusanya pamoja “watu wa milki ya pekee” ili watu hao waliopakwa mafuta kwa roho waweze ‘kutangaza pote sifa bora zake.’ (1 Petro 2:9, NW) Pia Mungu ‘anatikisa mataifa yote’ ili “vitu vinavyotamanika vya mataifa yote,” yaani, watu wenye kibali ya kimungu​—waweze kuingizwa ndani ya “nyumba” yake ya ibada na kuijaza utukufu. (Hagai 2:7, NW; linganisha Zekaria 8:23.) Kwa hiyo, watu walio na tumaini la kimbingu na wengine wanaotazamia uzima wa milele katika dunia-Paradiso wamekuwa Wakristo waliojiweka wakf na wakawa Mashahidi wa Yehova.​—Luka 23:43, NW; Ufunuo 7:1-17.

13 Lakini ni nani kati ya Wakristo wote hao waliojiweka wakf watakaokuwa mwishowe sehemu ya “mbingu mpya” na “dunia mpya” zilizoahidiwa? (Ufunuo 21:1, NW) Si kila mmoja wao. (Zaburi 15:1-5; Mathayo 22:14) Wale watakaokuwa si waaminifu hawatakuwa na nafasi yenye kudumu katika mpango wa Mungu. Kwa hiyo, ijapokuwa Yehova siye anayesababisha mateso, yeye anayaruhusu ili kuchuja (kuchunga) wasio washikamanifu watoke kati ya watu wake, kwa upande mwingine akihifadhi kati yao watu mmoja mmoja wenye ushikamanifu usiotiliwa mashaka na wenye kumpenda Mungu kwa moyo wote. (Mathayo 22:37, 38; 25:31-33; 2 Wakorintho 13:5) Sisi na tuwe kati ya wale wanaovumilia mateso kwa uaminifu na hivyo tuendelee kuwa na “pendeleo la kumtolea [Yehova Mungu] utumishi mtakatifu bila woga tukiwa na ushikamanifu na uadilifu mbele zake siku zetu zote”​—hata milele.​—Luka 1:68, 69, 74, 75, NW.

Sababu ya Kuwa Wenye Furaha Tujapoteswa

14. Yesu alitaja wazi kwamba ni sababu gani ya kuwa wenye furaha tujapoteswa?

14 Lile tumaini la Ufalme lilitajwa wazi na Yesu Kristo aliposema hivi: “Wenye furaha ni walioteswa kwa ajili ya Uadilifu; maana wao ndio ufalme wa mbingu!” (Mathayo 5:10, The Emphatic Diaglott) Ndiyo, zawadi nzuri ajabu inayowangoja wafuasi wa Yesu waliopakwa mafuta ambao watavumilia mateso kwa uaminifu ni kuwa na ushirika pamoja na Kristo katika Ufalme wa kimbingu. (Luka 12:32; Ufunuo 2:10; 14:1; 20:6) Nao mashahidi waaminifu wa Yehova walio na matumaini ya kidunia wana taraja zuri sana la kupata uzima wa milele katika dunia-Paradiso. (Luka 23:43, NW; Yohana 10:16; 17:3; Ufunuo 7:9, 10, 14) Basi, kwa uhakika tunaweza kuwa wenye furaha tujapoteswa ikiwa tutakumbuka lile tumaini la Ufalme.​—Warumi 12:12.

15. Enzi kuu ya Yehova imeshikanaje na ule Ufalme, na hayo yote yanahusikaje katika kutuletea furaha tujapoteswa?

15 Enzi kuu ya ulimwengu mzima ya Yehova imeshikana na Ufalme kwa njia isiyoweza kutenganishwa nao, kwa maana kupitia huo yeye atalitakasa jina lake takatifu. Sisi tulio mashahidi waaminifu wa Yehova na watangazaji wa Ufalme, tunaiunga mkono enzi kuu yake na hivyo tuna sababu ya ziada ya kuwa na furaha hata tunapokuwa katikati ya dhiki. (Isaya 43:10-12; Mathayo 6:9, 10) Kwa hiyo, kwa msaada wa Mungu na tuendeleze ukamilifu kwa Mungu na hivyo tuonyeshe Ibilisi ni mwongo asiyeweza kuhakikisha dai lake la kwamba hakuna mwanadamu angebaki mwaminifu kwa Yehova akiwa chini ya jaribu. (Ayubu 27:5) Kila Mkristo mwenye kuteswa anaweza kuwa mwenye furaha sana anapouunga mkono upande wa Yehova wa lile suala kuu!—Linganisha Matendo 4:24.

16. Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba dhamiri safi inasaidia kutuletea furaha tujapoteswa?

16 Dhamiri safi pia inawaletea furaha watangazaji wa Ufalme wenye kuteswa walio washikamanifu. Ijapokuwa inaelekea mtu mwenye kujiita Mkristo atapatwa na aibu na kusumbuka sana akilini anapotaabishwa kwa sababu ya kufanya kosa, mtu anakuwa na haki ya kuwa na furaha nyingi ikiwa anataabikia uadilifu akiwa shahidi mwaminifu wa Yehova na mfuasi wa Yesu Kristo. Hivyo, hata walipokwisha kupigwa mijeledi, mitume wa Yesu “walienda zao kutoka mbele ya Sanhedrini, wakifanya shangwe kwa sababu walikuwa wamehesabiwa wanastahili kudharauliwa kwa ajili ya jina [la Kristo].” (Matendo 5:40, 41, NW) Vivyo hivyo, baada ya Paulo na Sila kupigwa na kufungwa gerezani huko Filipi, hawakununa wala kusumbuliwa na dhamiri, kama kwamba walikuwa wamefanya kosa. Badala ya hivyo, karibu na usiku wa manane “walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu.” (Matendo 16:22-25) Kwa hiyo, ingawa shahidi wa Yehova hapaswi kamwe kujiendesha kwa njia itakayomletea adhabu ya kuwa mwenye hatia au kuwa mwuaji mwenye kusumbuliwa na dhamiri, kuwa mwivi, mtenda uovu au mwenye kujiingiza-ingiza katika mambo ya watu, anaweza kufurahi ikiwa anataabikia uadilifu.​—1 Petro 2:11,12; 3:13,14; 4:15,16.

17. Ni nini hasa kitakachoongeza furaha yetu tunapoteswa kwa kuwa wafuasi wenye kuunga mkono Ufalme?

17 Hasa kumpendeza Yehova na kumtukuza kutatuongezea furaha tunapoteswa kwa sababu ya kuwa wafuasi wenye kuunga Ufalme mkono. Hata tunapotaabishwa-taabishwa vibaya sana, tunahitajiwa kabisa ‘kutembea kwa kusudi la kumpendeza Mungu’ ili tuweze kuwa na furaha inayoendelea tukiwa watumishi wa Yehova. (1 Wathesalonike 4:1, NW) Zaidi ya hilo, tunapotaabika kwa sababu ya kuwa Wakristo, inatupasa ‘kuliungama jina hilo kwa utukuzo wa Mungu.’ Ebu fikiria hilo! Zaidi ya kumpendeza Yehova, wakati tunapovumilia mateso kwa uaminifu ‘tunaendelea kumtukuza Mungu.’ (1 Petro 4:16, The New English Bible; New World Translation) Ni kichocheo chenye kufurahisha kama nini kuvumilia mateso kwa ushujaa!

Tuzidi Kusonga Mbele Tukiwa Washika Ukamilifu

18. Inawapasa Mashahidi wa Yehova waoneje juu ya kushika ukamilifu wao kwa Mungu?

18 Basi, ni wazi kwamba Mashahidi wa Yehova wana sababu zinazofaa za kuwa wenye furaha wajapoteswa. Kwa hiyo, kwa msaada wa Mungu na tushike azimio letu kama mtunga zaburi Daudi, aliyetangaza hivi: “Kwa habari yangu mimi, katika ukamilifu wangu mimi nitatembea.”​—Zaburi 26:11, NW.

19. Sasa ni maulizo gani yanayojitokeza yafikiriwe?

19 Tukiwa Wakristo waaminifu, tunaweza kufurahi tujapoteswa kwa sababu tunaijua shabaha ya Ibilisi katika kutuletea dhiki hiyo. Tunatambua pia sababu ya Yehova Mungu kuruhusu watu wake wateswe. Hata hivyo, ingawa tuna sababu hizo za kufurahi tujapoelekeana na mateso, tunaweza kufanya nini tujitayarishe kuelekeana nayo? Na ni kwa njia gani tunaweza kuelekeana na mateso makali sana au hata ya kinyama tuweze kuyavumilia?

Maulizo ya Kujikumbusha

□ Shabaha ya Ibilisi ni nini katika kuletea Mashahidi wa Yehova mateso?

◻ Shetani ametokeza suala gani kuu, na ametokeza mashaka gani juu ya wanadamu?

◻ Kwa sababu gani Yehova anaruhusu watu wake wateswe?

◻ Yesu Kristo alitaja waziwazi sababu gani ya kuwa wenye furaha ‘tunapoteswa kwa ajili ya uadilifu’?

◻ Ni nini kinachotuongezea furaha tunapoteswa kwa sababu sisi ni watumishi wa Yehova?

[Picha katika ukurasa wa 5]

Yesu aliposhawishwa, alikataa kumpa Shetani hata tendo moja la ibada

[Picha katika ukurasa wa 8]

Lile tumaini la ufalme linatoa sababu inayofaa ya kuwa wenye furaha yajapokuwako mateso

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki