Wakati “Haidhuru Upepo Unaelekea Wapi”
“MTU asipojua anaelekea bandari ipi, haidhuru upepo unaelekea wapi.” Maneno hayo, yaliyosemwa na mwanafalsafa Mroma wa karne ya kwanza Lucius Annaeus Seneca, yanathibitisha kweli hii iliyojulikana kwa muda mrefu: Ili maisha yawe na mwongozo, miradi ni ya maana.
Hata hivyo, mara nyingi maisha ni kama kutangatanga baharini. Wengi wanaridhika tu na kuepa miamba na vizingia vya maisha ya kila siku. Bila kujua wanakoelekea wao huwa kama mawimbi ya bahari ‘yanayosukumwa mbele na upepo dakika moja na kurudishwa nyuma dakika ifuatayo.’ (Yakobo 1:6, “Phillips”) Kwa watu kama hao, “haidhuru upepo unaelekea wapi.”
Biblia huandaa vielelezo vya wale waliokuwa wakijiwekea miradi, hivyo wakitumika kuwa vielelezo vya kuigwa kwa Wakristo leo. Musa “alikaza macho kuelekea malipo ya thawabu.” (Waebrania 11:26, “NW”) Paulo aliandika hivi: “Nakimbia mbele kabisa kuuelekea mradi ili kushinda thawabu.” Aliwatia moyo waamini wenzake “wawe na mtazamo uo huo.”—Wafilipi 3:14, 15, “Today’s English Version.”
Macho yetu yakiwa yamekazwa kikiki kwenye ahadi za Biblia, na tuige imani ya wanaume hao waliokuwa wenye miradi.—Linganisha Waebrania 13:7.