Tukio Usilopaswa Kukosa
“Kila zawadi njema na kila upaji mkamilifu” hutoka kwa Mungu, Baba yetu wa kimbingu. (Yak. 1:17, NW) Zawadi kubwa kupita zote ambayo Mungu amewapa wanadamu wenye dhambi ni uandalizi wa kuondolewa dhambi kupitia Mwana wake mzaliwa-pekee, Yesu Kristo. Kifo cha Yesu akiwa Mfidi wetu hufanya tuweze kupata uhai udumuo milele katika dunia iliyo paradiso. Kwenye Luka 22:19, twaamuriwa tukikumbuke kifo chake.
Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ushiriki pamoja nao kutii amri ya Yesu. Mwadhimisho huu wa kila mwaka utakuwa baada ya jua kushuka kwenye tarehe inayolingana na Nisani 14 kwenye kalenda-mwezi ya Biblia, itakayokuwa Jumanne, Aprili 2, 1996. Tia alama tarehe hii ili usiisahau. Mashahidi wa Yehova katika eneo lako watakuambia mahali na wakati hasa wa mkutano huo.