Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 4/15 uku. 30
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Elimu—Itumie Kumsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Wewe Peke Yako Ni Mwaminifu-Mshikamanifu”
    Mkaribie Yehova
  • Watazame Wale Waaminifu-Washikamanifu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 4/15 uku. 30

Je, Wakumbuka?

Je, umeona matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kuwa yenye msaada kwako? Basi kwa nini usitahini kumbukumbu lako kwa maswali yafuatayo:

◻ Twaweza kujifunza somo gani kutokana na anguko la Waamoni? (Sefania 2:9, 10)

Yehova halioni kuwa jambo dogo kuonyesha uhasama kwa fadhili yake, na kwa wakati wake, atachukua hatua, kama alivyofanya katika nyakati za kale. (Linganisha Zaburi 2:6-12.)—12/15, ukurasa 10.

◻ Ni katika njia gani ambazo Wakristo wana amani?

Kwanza, wana “amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana [wao] Yesu Kristo.” (Warumi 5:1) Pili, wana amani miongoni mwao wenyewe kwa kusitawisha “hekima itokayo juu,” ambayo “kwanza ni safi, tena ni ya amani.” (Yakobo 3:17)—1/1, ukurasa 11.

◻ Neno la Mungu lafananishwa na vitu gani, nalo hili lawaje lenye msaada kwetu?

Neno la Mungu linafananishwa na maziwa yenye lishe, chakula kigumu, maji yenye kuburudisha na yenye kusafisha, kioo, na upanga mkali. Kuelewa kinachodokezwa na maneno hayo kwamsaidia mhudumu kuitumia Biblia kwa ustadi.—1/1, ukurasa 29.

◻ Elimu yenye usawaziko yapaswa itusaidie kufanya nini?

Kusoma vizuri, kuandika maandishi yawezayo kusomeka, kukua kiakili na kiadili, na kujipatia mazoezi kwa vitendo yanayohitajiwa kwa maisha ya kila siku na utumishi mtakatifu wenye matokeo.—2/1, ukurasa 10.

◻ Ni somo gani lenye thamani kuhusu elimu tunaloweza kujifunza kutoka kwa Yesu?

Elimu yapasa itumiwe, si kujitukuza wenyewe, bali ili kumletea sifa Mwelimishaji mkuu, Yehova Mungu. (Yohana 7:18)—2/1, ukurasa 10.

◻ Ufalme wa Mungu ni nini?

Ufalme ni serikali ya kimbingu iliyosimamishwa na Mungu inayotimiza mapenzi ya Mungu na kuondolea mbali matokeo ya dhambi na kifo na kurudisha hali za uadilifu duniani. (Danieli 2:44; Ufunuo 11:15; 12:10)—2/1, ukurasa 16.

◻ Biblia inaandaaje elimu inayohitajiwa kuleta mwisho wenye kudumu wa jeuri?

Kupitia Neno lake, Biblia, Yehova hufundisha watu kuwa wapenda amani na uadilifu. (Isaya 48:17, 18) Neno la Mungu lina nguvu ya kufikia na kugusa moyo wa mtu na kubadili kufikiri kwake na tabia zake. (Waebrania 4:12)—2/15, ukurasa 6.

◻ Ni katika njia gani unabii wa Isaya sura ya 35 unavyoweza kusemwa kuwa na utimizo wa mara tatu?

Unabii wa Isaya ulikuwa na utimizo wa kwanza wakati Wayahudi waliporudi kutoka utekwa wa Babiloni katika 537 K.W.K. Una utimizo wa kiroho leo tangu kuachiliwa kwa Israeli wa kiroho kutoka utekwa wa Babiloni Mkubwa. Na utakuwa na utimizo wa tatu kuhusiana na uhakikisho wa Kibiblia wa hali halisi za paradiso duniani. (Zaburi 37:10, 11; Ufunuo 21:4, 5)—2/15, ukurasa 17.

◻ Upendezi wa kibinafsi wa Mungu kwa wanadamu ulionyeshwaje katika miujiza iliyofanywa na Mwanaye, Yesu?

Kwa kuwa Yesu “hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda,” huruma yake nyororo yaonyesha hangaiko lenye kugusa moyo la Yehova kwa kila mmoja wa watumishi wake. (Yohana 5:19)—3/1, ukurasa 5.

◻ Ni nini linalomaanishwa na usemi wa Yesu “makaburi ya ukumbusho” unaotumiwa kwenye Yohana 5:28, 29, NW?

Neno la Kigiriki mne·mei’on (kaburi la ukumbusho) hudokeza kwamba Yehova hukumbuka rekodi ya mtu aliyekufa, kutia ndani tabia zake zilizorithiwa na kumbukumbu lake kamili. Hili hutoa uthibitisho wenye nguvu kwamba Mungu hujali wanadamu wakiwa mtu mmoja-mmoja!—3/1, ukurasa 6.

◻ Ni ujumbe gani wenye onyo katika unabii wa Sefania ulio na msaada wenye kutumika kwetu?

Leo si wakati wa kuacha shaka zikue mioyoni mwetu na kuahirisha akilini kuja kwa siku ya Yehova. Pia, twapaswa kulinda dhidi ya matokeo yenye kudhoofisha ya kutojali. (Sefania 1:12, 13; 3:8)—3/1 ukurasa 17.

◻ Kwa nini uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu hutokeza ugumu?

Kwa sababu uaminifu-mshikamanifu hupingana na mapendezi ya kibinafsi tuliyorithi kutoka kwa wazazi wetu. (Mwanzo 8:21; Warumi 7:19) La maana zaidi, Shetani na roho wake waovu wameazimia kuvunja uaminifu-mshikamanifu wetu kwa Mungu. (Waefeso 6:12; 1 Petro 5:8)—3/15, ukurasa 10.

◻ Ni katika sehemu zipi nne tunazopaswa kukabili ugumu wa uaminifu-mshikamanifu, na ni nini kitakachotusaidia kufanya hivyo?

Sehemu hizo nne ni uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova, tengenezo lake, kwa kutaniko, na kwa wenzi wetu wa ndoa. Msaada mmoja wa kukabili magumu haya ni kujua kwamba ugumu wa uaminifu-mshikamanifu wahusiana na kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova.—3/15, ukurasa 20.

◻ Ni somo gani tuwezalo kujifunza kutokana na ono la Daudi katika kujaribu kurudisha sanduku la agano Yerusalemu? (2 Samweli 6:2-7)

Daudi alipuuza maagizo ambayo Yehova alikuwa ametoa kuhusu kubeba lile Sanduku, na jambo hili lilileta msiba. Somo ni kwamba hatupaswi kamwe kumlaumu Yehova kwa ajili ya matatizo yetu yatokeayo kwa sababu twapuuza maagizo yake yaliyo wazi. (Mithali 19:3)—4/1, kurasa 28, 29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki