“Ni Kazi ya Yehova”
Hicho kilikuwa ndicho kichwa cha makala iliyokuwa katika gazeti El Norte la Monterrey City, Mexico. Makala hiyo ilihusu Jumba jipya la Kusanyiko la Mashahidi wa Yehova.
Monterrey ni jiji lililo na idadi ya watu 2,300,000 (kutia ndani viunga) katika sehemu ya kaskazini ya Mexico, na lina watangazaji wa Ufalme 19,200. Kwa karibu mwaka mmoja na nusu, Mashahidi waliunganisha jitihada zao kujenga Jumba la Kusanyiko maridadi na lenye kufaa lenye kisafisha hewa na viti vyenye kustarehesha 3,000. Mashahidi wa huko walikuwa na shangwe mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova alipotoa hotuba ya kuweka wakfu. Programu ilitia ndani historia fupi ya kazi katika Monterrey, na kulikuwako na mahoji pamoja na wale walioshiriki katika ujenzi. Kisha wale 4,500 waliohudhuria mkutano huo walifurahia hotuba ya kuweka wakfu.
Hili ni jumba la tatu kati ya Majumba ya Kusanyiko ya majuzi ambayo yamejengwa katika Mexico katika kile ambacho kimefafanuliwa kuwa kampeni ya kupata “Majumba ya Ufalme na Majumba ya Kusanyiko, Mengi, Makubwa, na Yaliyo Bora.”
Kukiwa na watangazaji zaidi ya 443,000 katika Mexico, na hudhurio la 1,492,500 kwenye Ukumbusho katika 1995, kwa hakika Majumba ya Kusanyiko mapya, kama lile katika Monterrey, yataendeleza kusudi la kimungu.