Ni Nani wa Kulaumiwa kwa Vita?
JE, MUNGU ni wa kulaumiwa kwa vita vinavyopiganwa na jamii ya kibinadamu? “La, Mungu hataki vita.” Hivyo ndivyo Martin Niemöller, kasisi Mprotestanti Mjerumani ajulikanaye sana, alivyojibu swali hilo muda mfupi baada ya mwisho wa Vita ya Ulimwengu 2. Maelezo yake yalichapishwa katika 1946 katika kitabu kiitwacho Ach Gott vom Himmel sieh darein—Sechs Predigten (Ee Mungu, Tazama Kutoka Mbinguni—Mahubiri Sita).a Hicho kitabu chataarifu hivi:
“Yeyote yule atakaye kumlaumu Mungu kwa [vita] hajui, au hataki kujua, Neno la Mungu. Bila shaka, ni jambo jingine ikiwa sisi Wakristo tuna hatia ya kadiri kubwa ya vita vinavyoendelea. Nasi hatuwezi kuepuka jambo hili kwa urahisi sana. . . . Pia yaweza kukumbukwa kwa usahihi kwamba makanisa ya Kikristo yamejitoa yenyewe tena na tena, kwa muda wa enzi zote ambazo zimepita, katika kubariki vita, majeshi, na silaha na kwamba yalisali kwa njia isiyopatana hata kidogo na ukristo yakiomba uharibifu wa maadui wayo vitani. Yote hayo ni makosa yetu na makosa ya babu zetu, lakini Mungu si wa kulaumiwa hata kidogo. Na sisi Wakristo wa leo tunaaibika mbele ya lile lenye kuitwa farakano isivyofaa kama wale Wanafunzi wa Biblia Wenye Bidii [Mashahidi wa Yehova], walioingia kambi za mateso kwa mamia na maelfu na [hata] wakafa kwa sababu walikataa utumishi wa kijeshi nao wakakataa kuua wanadamu.”
Leo, miaka ipatayo 50 baada ya Vita ya Ulimwengu 2, maneno ya Niemöller yanawaandalia watu wenye kupenda amani, jambo linalostahili kufikiriwa kwa uangalifu. La, Mungu si wa kulaumiwa kwa umwagaji-damu wa mataifa! Kwa kweli, kupitia waabudu wake wa kweli, ambao hujitenga na mapambano ya ulimwengu, Mungu anajulisha mwisho ulio karibu wa vita vyote.—Zaburi 46:9; Yohana 17:16.
[Maelezo ya Chini]
a Baadaye mahubiri ya Martin Niemöller yalichapishwa katika Kiingereza katika kitabu kiitwacho Of Guilt and Hope. Hata hivyo, fasiri ya Kiingereza inatofautiana na maandishi-awali ya Kijerumani, kwa sababu hiyo, nukuu hili limetafsiriwa moja kwa moja kutoka Kijerumani.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
Picha ya USAF