Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 8/15 uku. 31
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Ajapo Katika Utukufu wa Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Jinsi Kugeuka Umbo kwa Kristo Kwakuathiri Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Siri Unayoweza Kuwaambia Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Siri Ambayo Wakristo Hawathubutu Kuweka!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 8/15 uku. 31

Je, Wakumbuka?

Je, umepata matoleo ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi kuwa yenye thamani ya kutumika kwako? Hivyo basi kwa nini usijaribu kumbukumbu yako kwa maswali yafuatayo?

◻ Har–Magedoni itakuwaje? (Ufunuo 16:14, 16)

Haitakuwa apokalipsi ya kinyuklia wala msiba wenye kuchochewa na wanadamu. La, hii ni vita ya Mungu ya kumaliza vita vyote vya kibinadamu, kuangamiza wote wale waendelezao vita hivyo, na kuleta amani ya kweli kwa wale wapendao amani. Haitachelewa. (Habakuki 2:3)—4/15, ukurasa wa 17.

◻ Ni aina gani ya arusi ambayo humheshimu Yehova?

Arusi ambayo pande za kiroho zakaziwa kuliko njia za kilimwengu itamheshimu Yehova kikweli. Wakristo watafurahia hiyo pindi ikiwa wataepuka desturi, ushirikina, na mazidio ya kilimwengu yaliyoshuka; ikiwa hawaiachi iingilie utendaji wa kawaida wa kitheokrasi; na ikiwa wanadhihirisha kiasi badala ya wonyesho wa kujivuna.—4/15, ukurasa wa 26.

◻ Ni nini humtambulisha mtu mwenye uaminifu-maadili?

Mtu mwenye uaminifu-maadili aweza kutumainiwa, si na mwanadamu mwenzake tu, bali pia la maana zaidi, aweza kutumainiwa na Mungu. Usafi wake wa moyo unaonwa katika matendo yake. Yeye hana unafiki. Si mwenye vipengee wala si mfisadi. (2 Wakorintho 4:2)—5/1, ukurasa wa 6.

◻ Kwa nini Yeremia alisema: “Ni vema mwanadamu aichukue nira wakati wa ujana wake”? (Maombolezo 3:27)

Kujifunza kukabiliana na majaribu wakati wa ujana husaidia kutayarisha mtu kukabili magumu ya utu uzima. (2 Timotheo 3:12) Manufaa za uaminifu ni nyingi kuliko kitulizo chochote cha kipindi fulani ambacho kuridhiana huenda kukaleta.—5/1, ukurasa wa 32.

◻ Jambo gani lilifananisha kimbele kuonekana kwa Musa na Eliya katika ono la mgeuko-umbo?

Katika kikao cha mgeuko-umbo, Musa na Eliya walikuwa mifano ifaayo ya ndugu watiwa-mafuta wa Yesu. Kwamba wao, kama vile Yesu, “walionekana wakiwa na utukufu” ilionyesha kwamba Wakristo waaminifu watiwa-mafuta ‘wangetukuzwa pamoja’ na Yesu katika mpango wa kimbingu wa Ufalme. (Luka 9:30, 31; Waroma 8:17; 2 Wathesalonike 1:10)—5/15, ukurasa wa 12, 14.

◻ “Siri takatifu” ya Mungu ni nini? (1 Wakorintho 2:7)

“Siri takatifu” ya Mungu huelekezewa Yesu Kristo. (Waefeso 1:9, 10) Lakini, hiyo si utambulisho tu wa Yesu akiwa Mesiya aliyeahidiwa. Yahusisha serikali ya kimbingu, Ufalme wa Kimesiya wa Mungu, yatia ndani fungu ambalo Yesu amegawiwa katika kusudi la Mungu.—6/1, ukurasa wa 13.

◻ Mkristo anapaswa kuonaje kuzidi kwa umri au ugonjwa?

Badala ya kuona majaribu kama hayo yakimwekea mipaka utumishi wake kwa Yehova, apaswa kuyaona kuwa fursa ya kuongeza utegemeo wake kwa Yehova. Pia apaswa kukumbuka kwamba thamani ya Mkristo haipimwi kwa kiwango chake cha utendaji tu, bali pia kwa imani na kina cha upendo wake. (Marko 12:41-44)—6/1, ukurasa wa 26.

◻ Yehova alionyeshaje hekima yake kubwa kwa kutumia wanadamu kuandika Biblia badala ya malaika?

Ikiwa ingekosa kabisa kikolezo cha kibinadamu, huenda ikawa tungekuwa na tatizo la kuelewa ujumbe wa Biblia. Pia, Biblia ina uchangamfu, mambo tofauti-tofauti, na uvutio ambao kikolezo cha kibinadamu huipatia.—6/15, ukurasa wa 8.

◻ Ni nini siri ya kupata furaha ya familia?

Siri yapatikana katika kurasa za Neno la Mungu, Biblia, na katika kuzitumia kanuni zake, kama vile, kujidhibiti, kutambua ukichwa, uwasiliano mzuri, na upendo.—6/15, ukurasa wa 23, 24.

◻ Uponyaji uliofanywa na Yesu ulikuwaje tofauti kabisa na ule unaofanywa kwa kawaida na wale wanaodai eti wana nguvu za uponyaji leo?

Hakukuwa na wonyesho wa kihisia-moyo wenye nguvu kwa upande wa umati na hakukuwa na wonyesho wa kutazamisha wenye kichaa kwa upande wa Yesu. Kwa kuongeza, Yesu hakushindwa kamwe kuponya waliokuwa na kasoro za mwili kwa kisingizio kwamba upaji wao wa kifedha haukuwa wenye ukarimu vya kutosha au kwamba walikosa imani.—7/1, ukurasa wa 5.

◻ Yehova amewasaidiaje watu wake kuwa na sehemu katika kusudi lake la kimungu kwa habari ya jina lake na Ufalme wake?

Kwanza, Yehova amewakabidhi watu wake ile kweli. Pili, aliwapa roho yake takatifu. Na tatu, tuna udugu wa ulimwenguni pote na mpango wa kitengenezo wa Yehova kwa ajili ya ibada.—7/1, ukurasa wa 19, 20.

◻ Wema wa adili ni nini?

Wema wa adili ni ubora wa kiadili, wema, kutenda na kufikiri ifaavyo. Si sifa baridi bali sifa tendaji, yenye kujenga. Wema wa adili hutia ndani zaidi ya kuepuka dhambi; humaanisha kufuatia lililo jema. (1 Timotheo 6:11)—7/15, ukurasa wa 14.

◻ Ni urithi gani ulio wa thamani zaidi ambao wazazi waweza kuwapa watoto wao?

Urithi ulio wa thamani zaidi ni kielelezo chao wenyewe katika kuonyesha upendo kwa wengine. Kwa kutokeza, watoto huhitaji kuona na kusikia wazazi wao wakisema na kuonyesha upendo wa kweli wa Mungu katika kila jambo wafanyalo.—7/15, ukurasa wa 22.

◻ Ni mambo gani yaliyo muhimu katika kuongoza funzo la familia lenye mafanikio?

Funzo la familia linapaswa kuwa la kawaida. Ni lazima ‘ununue wakati’ kwa ajili ya funzo. (Waefeso 5:15-17) Fanya vipindi vya funzo kuwa vya kupendeza kwa watoto kwa kufanya Biblia ipendeze. Ili watoto wafurahie funzo, ni lazima wahisi wamehusishwa.—8/1, ukurasa wa 26, 28.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki