Tafadhali Jiunge Nasi kwa Ajili ya Tukio la Pekee, Jumamosi, Aprili 11, 1998
MASHAHIDI WA YEHOVA wakualika kwa uchangamfu ukumbuke pamoja nao zawadi itokayo kwa Mungu ya Mwana wake, Yesu Kristo. Zawadi hiyo iliwafungulia jamii ya kibinadamu taraja la kuonea shangwe uhai udumuo milele.—Yohana 3:16.
Mwaka huu Ukumbusho wa kifo cha Yesu utaadhimishwa baada ya mshuko-jua Jumamosi, Aprili 11. Tarehe hiyo yalingana na Nisani 14 ya kalenda ya Biblia ya mwezi-luna. Tafadhali pata habari kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu ili upate kujua wakati na mahali barabara pa kukutania.
Je, wajua juu ya matukio hayo yaliyotokea wakati wa siku za mwisho za Yesu duniani?