Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 8/15 uku. 32
  • “Ni Nani Aliyeyazaa Matone ya Umande?”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ni Nani Aliyeyazaa Matone ya Umande?”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 8/15 uku. 32

“Ni Nani Aliyeyazaa Matone ya Umande?”

MWANDISHI wa habari wa karne ya 19 alifafanua matone ya umande kuwa “vito vya umajimaji vya dunia, vilivyofanyizwa kwa hewa.” Muumba wetu alimuuliza mzee wa ukoo wa kale, Yobu hivi: “Ni nani aliyeyazaa matone ya umande?” (Ayubu 38:28) Mungu alikuwa akimkumbusha Yobu juu ya asili ya kimungu ya umande wenye thamani.

Mbali na uzuri wake unaometameta kama kito, katika Biblia umande unahusianishwa na baraka, uzazi, wingi, na kuhifadhiwa kwa hai. (Mwanzo 27:28; Kumbukumbu la Torati 33:13, 28; Zekaria 8:12) Wakati wa majira yenye joto ya Israeli, yasiyo na mvua, “umande wa Heremoni” ulihifadhi mimea ya nchi na hivyo ukihifadhi watu wake. Vilele vyenye msitu na barafu vya Mlima Heremoni bado vyatokeza mvuke wa usiku unaogeuzwa kuwa umande mwingi. Mtunga-zaburi Daudi alilinganisha burudisho liletwalo na umande huu na hisi nzuri ya kuishi kwa muungano pamoja na waabudu wenzake wa Yehova.—Zaburi 133:3.

Maagizo ya nabii Musa kwa Israeli yalikuwa yenye uanana na yenye kuburudisha, kama matone ya umande. Yeye alisema: “Maneno yangu yatatona-tona kama umande; kama manyunyu juu ya majani mabichi.” (Kumbukumbu la Torati 32:2) Leo, Mashahidi wa Yehova wanatangaza habari njema zenye kutoa uhai kuhusu Ufalme wa Mungu hadi kwenye miisho ya dunia. (Mathayo 24:14) Mungu anatoa mwaliko huu: “‘Njoo!’ Na acha yeyote anayeona kiu aje; acha yeyote atakaye achukue maji ya uhai bure.” (Ufunuo 22:17) Mamilioni ya watu wa mataifa yote wanakubali toleo hilo la burudisho la kiroho kutoka kwa Mungu, ambalo laweza kutegemeza uhai milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki