Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 8/15 uku. 30
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Siku ya Hukumu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Mwige Yehova—Dhihirisha Haki na Uadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 8/15 uku. 30

Je, Wakumbuka?

Je, umefikiria kwa uangalifu matoleo ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa umefanya hivyo, utaliona kuwa jambo lenye kupendeza kukumbuka yafuatayo:

◻ Kwa nini fundisho la kuamuliwa kimbele yatakayompata mtu halipatani na akili?

Ikiwa Mungu alijua kimbele na kuagiza kimbele kutumbukia kwa Adamu katika dhambi, basi Yehova alipata kuwa chanzo cha dhambi alipomwumba mwanadamu naye angekuwa ndiye chanzo cha uovu wote na kuteseka kwa wanadamu. Hilo haliwezi kupatanishwa na uhakika wa kwamba Yehova ni Mungu mwenye upendo na achukiaye uovu. (Zaburi 33:5; Mithali 15:9; 1 Yohana 4:8)—4/15, ukurasa 7, 8.

◻ Katika utimizo wa Isaya 2:2-4, watu kutoka mataifa mengi wanafanya nini?

Wanapomiminika katika nyumba ya Yehova ya ibada, pia wanaepuka ‘kujifunza vita’ kwa sababu wameweka uhakika wao katika ulinzi wa majeshi ya Mungu ya kimbingu, ambayo yako tayari kuangamiza maadui wote wa amani.—4/15, ukurasa wa 30.

◻ Ni nani walio mashujaa wa Mungu wanaosemwa katika Yoeli 3:10, 11?

Kwenye Biblia, Mungu wa kweli anaitwa “Yehova wa majeshi” mara 280. (2 Wafalme 3:14) Majeshi hayo ni majeshi ya kimalaika ya kimbingu, ambayo yako tayari kutekeleza amri ya Yehova.—5/1, ukurasa wa 23.

◻ Ni somo gani tuwezalo kujifunza kutokana na Yehova kumtaka Yobu asali kwa niaba ya wale waliofanya dhambi dhidi yake? (Ayubu 42:8)

Kabla ya kumrudishia Yobu hali nzuri ya afya, Yehova alimtaka asali kwa niaba ya wale waliofanya dhambi dhidi yake. Hilo laonyesha kwamba Yehova hutaka kwamba tuwasamehe wale wafanyao dhambi dhidi yetu kabla ya dhambi zetu wenyewe kuweza kusamehewa. (Mathayo 6:12; Waefeso 4:32)—5/1, ukurasa wa 31.

◻ Yakobo alimaanisha nini aliposema hivi: “Acheni uvumilivu uwe na kazi yao ikiwa kamili”? (Yakobo 1:4)

Uvumilivu una kazi ya kufanya, “kazi” fulani. Mgawo wake ni kutufanya tuwe kamili katika mambo yote. Kwa sababu hiyo, kwa kuruhusu majaribu yaendelee hadi mwisho wake, bila kujaribu kwa vyovyote kutumia njia zisizo za Kimaandiko ili kuyakomesha upesi, imani yetu inajaribiwa na kutakaswa.—5/15, ukurasa wa 16.

◻ Kwa nini Mungu amengoja kwa muda mrefu hivyo kutatua matatizo ya wanadamu?

Maoni ya Yehova ya wakati hutofautiana na yetu. Kwa Mungu aliye wa milele, wakati wa tangu kuumbwa kwa Adamu hadi sasa hata haujumliki kuwa juma moja. (2 Petro 3:8) Lakini hata tuwe na maoni gani juu ya wakati, kila siku ipitayo hutuleta karibu zaidi na siku ya kutetewa kwa Yehova.—6/1, ukurasa wa 5, 6.

◻ Ni nini ambacho huwachochea Mashahidi wa Yehova?

Ufundishaji wa Yehova umetokeza watu wa pekee, walioelimishwa kupendana na kuwapenda jirani zao kama wajipendavyo wenyewe. (Isaya 54:13) Upendo ndio huwachochea Mashahidi wa Yehova waendelee kuhubiri ujapokuwa ubaridi au mnyanyaso. (Mathayo 22:36-40; 1 Wakorintho 13:1-8)—6/15, ukurasa wa 20.

◻ Yamaanisha nini maneno haya ya Yesu: “Jikakamueni wenyewe kisulubu ili mwingie ndani kupitia mlango mwembamba”? (Luka 13:24)

Maneno ya Yesu yadokeza kung’ang’ana, kujitahidi sana. Maneno yake yaonyesha pia kwamba watu fulani wanaweza kutafuta sana ‘kupitia mlango mwembamba’ wakati wao uwafaao na kwa mwendo wa kustarehe wanaopendelea. Kwa hiyo kila mmoja wetu aweza kujiuliza, ‘Je, mimi najikaza kwa bidii yenye kuendelea?’—6/15, ukurasa wa 31.

◻ Wenye kufufuliwa ‘watahukumiwaje kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na vitendo vyao’? (Ufunuo 20:12)

Hati-kunjo hizo si rekodi ya vitendo vyao vya wakati uliopita; walipokufa, waliondolewa hatia ya dhambi walizofanya maishani mwao. (Waroma 6:7, 23) Hata hivyo, wanadamu wenye kufufuliwa bado watakuwa chini ya dhambi ya Kiadamu. Basi, ni lazima iwe kwamba hati-kunjo hizo zitaeleza kikamili maagizo ya kimungu ambayo wote lazima wafuate ili wanufaike kikamili na dhabihu ya Yesu Kristo.—7/1, ukurasa wa 22.

◻ Ni masomo gani yaliyo katika mfano wa Yesu kuhusu Msamaria mwenye ujirani? (Luka 10:30-37)

Mfano wa Yesu waonyesha kwamba, mtu aliye mnyoofu kwa kweli ni yule ambaye hutii si sheria za Mungu tu, bali pia huiga sifa zake. (Waefeso 5:1) Pia waonyesha kwamba ujirani wapaswa kushinda vizuizi vya kitaifa, kitamaduni, na kidini. (Wagalatia 6:10)—7/1, ukurasa wa 31.

◻ Ni maeneo gani matatu ambayo katika hayo waweza kuwajua watoto wako na kuwaandalia mwongozo wa kimzazi?

(1) Wasaidie watoto wako wachague aina ya kazi ya kimwili ifaayo; (2) watayarishe kukabiliana na mikazo ya kihisia-moyo shuleni na kazini; (3) waonyeshe jinsi ya kutosheleza mahitaji yao ya kiroho.—7/15, ukurasa wa 4.

◻ Mungu alipumzika “siku ya saba” kwa kusudi gani? (Mwanzo 2:1-3)

Mungu hakupumzika kwa sababu ya kuchoka. Badala yake, aliacha kabisa kazi ya kuumba vitu vya kidunia ili aruhusu kazi yake isitawi na kufikia utukufu kamili, na kumletea sifa na heshima.—7/15, ukurasa wa 18.

◻ Ni njia zipi tatu ambazo katika hizo twaweza kudhihirisha haki?

Kwanza, lazima tujipatanishe na viwango vya Mungu vya adili. (Isaya 1:17) Pili, twadhihirisha haki tunapotendea wengine vile tunavyotaka Yehova atutendee. (Zaburi 130:3, 4) Tatu, twaonyesha haki ya kimungu tunaposhiriki kwa bidii katika shughuli ya kuhubiri. (Mithali 3:27)—8/1, ukurasa wa  14, 15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki