Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 2/15 uku. 3
  • Je, Unafikiria Ndoa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unafikiria Ndoa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Ndoa Inaweza Kustahimili Msukosuko?
    Amkeni!—2006
  • Ndoa Inaweza Kufanikiwa Katika Ulimwengu wa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Ikiwa Ndoa Imo Katika Hatua ya Kuvunjika
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kuwekea Nyumba Yako Msingi Mzuri
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 2/15 uku. 3

Je, Unafikiria Ndoa?

Tukilinganisha hali ya talaka ya tufeni pote na tetemeko la dunia, Marekani ingekuwa ndiyo kitovu cha talaka. Katika mwaka wa hivi majuzi, zaidi ya ndoa milioni moja zilivunjika huko—wastani wa ndoa mbili kila dakika. Lakini labda wajua kwamba si Marekani pekee iliyo na matatizo ya ndoa.

KULINGANA na uchunguzi mmoja, viwango vya talaka katika Kanada, Uingereza na Wales, Ufaransa, Ugiriki, na Uholanzi vimeongezeka zaidi ya maradufu tangu 1970.

Tuna kila sababu ya kuamini kwamba wenzi wengi hufunga ndoa kwa sababu wanapendana na wanataka kuishi pamoja kwa muda wote wa maisha yao. Hata hivyo, kwa kusikitisha, ndoto ya kuwa na ndoa yenye furaha mara nyingi huthibitika kuwa hivyo tu, yaani, ndoto. Wanapozinduka na kufikiria mambo kihalisi, wengi wamesema kwamba walifunga ndoa mapema sana au hawakufunga ndoa na mtu awafaaye au mambo yote mawili.

Kwa nini ndoa nyingi huvunjika? “Sababu kuu ni kukosa kujitayarisha,” asema mtungaji wa kitabu kimoja kuhusu uchumba. Yeye aongezea kusema: “Ninaposhughulika na wenzi wa ndoa wanaopambana na msononeko wa ndoa, mimi hulemewa na hisia za namna mbili—huruma na hasira. Nahisi huruma kwa sababu ndoto yao ya kuwa na uhusiano wenye kutosheleza haijatimizwa. Nahisi hasira kwa sababu ya kutokujua kwao ugumu wa jambo hilo.”

Kwa kweli, wengi hufunga ndoa bila kujua jinsi ya kuifanikisha. Hata hivyo, jambo hilo halishangazi. Mwelimishaji mmoja alitoa maoni haya: “Ni wangapi kati ya vijana wetu huenda chuoni kujifunza juu ya tabia ya panya na mijusi, lakini hukosa kujifunza juu ya tabia ya watu wawili wanaoitwa mume na mke?”

Je, unafikiria ndoa—uwezekano wa kuoa baadaye au juu ya ndoa yako sasa? Ikiwa ndivyo, wapaswa kujua kwamba uhusiano halisi wa maisha ni tofauti na ule unaoonyeshwa kwenye sinema, maonyesho ya televisheni na vitabu vya mahaba. Wakati uleule, ndoa ya watu wawili wakomavu ambao kwa kweli wanapendana yaweza kuonwa kuwa baraka kutoka kwa Mungu. (Mithali 18:22; 19:14) Basi je, waweza kuwaje na uhakika kwamba uko tayari kutimiza matakwa ya ndoa? Ni mambo gani unayopaswa kuchunguza unapochagua mwenzi? Au ikiwa tayari umeoa au kuolewa, waweza kuongezaje uwezekano wa kupata furaha ya kudumu katika ndoa yako?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki